Nani Fisadi-CCM ama Serikali?

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,967
22,476
CCM Kuongeza kiwango cha MadiniBy Mike Mushi | Published 11/26/2005 | Habari Mpya |
CCM Kuongeza kiwango cha Madini


shein-2005-52.jpg

Chama Cha Mapinduzi kinakusudia kuongeza kiwango cha thamani ya madini kutoka asilimia 0.3 ya hivi sasa hadi kufikia asilimia 3 iwapo chama hicho kitashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk Ali Mohamed Shein amesema pamoja na kuongeza viwango vya madini hayo pia serikali ijayo itahakikisha inatengeneza vito vya madini hapa hapa nchini ili kuweza kuuza madini kwa tija.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Londoni wilayani Manyoni.

Amesema suala la madini limepewa kipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005-2010 kutokana na ukweli kwamba sekta ya madini inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua uchumi wa nchi.

Amewaambia wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa ili kufanikisha azma hiyo serikali itatoa mikopo na elimu kwa wachimbaji wadogo wadogo kwa njia ya semina na mikutano ili waweze kujua namna ya kuchimba madini hayo kitalaam.

�Baada ya kupewa mikopo, mpewe elimu kwa njia ya semina, mikutano au warsha mjue namna ya kuchimba madini hayo kitalaam�. Aliwaeleza wananchi hao ambao wengi wao ni wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu katika eneo hilo.

Dk. Shein amethibitisha kuwa serikali ya awamu ya nne itaendelea kukaribisha wawekezaji wakubwa katika sekta ya madini na pia itaangalia upya sera yake ya madini ili iweze kuwanufaisha wadau wote.

Amesisitiza wananchi wakichague Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndio chama pekee kinachoonyesha jitihada za kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kuweza kupambana na umasikini hali ambayo hatmae itawafanya kuwa na maisha bora.

Katika hatua nyingine Mgombea Mwenza huyo amewataka wachimbaji wadogo wa madini nchini kutumia fedha wanazozipata kwa kujijenga kimaisha kwa kuwa na nyumba bora, kutunza afya zao na kusomesha watoto na sio kwa anasa.

�Fedha ni fedheha, zikiwa nyingi zinachanganya kidogo hujui utazifanyia nini, unaishia sehemu ukiulizwa wewe nani na wewe unauliza pia wewe nani. Huo si utumiaji mzuri wa fedha�. Alisema Dk Shein

�Hata hivyo starehe zikizidi inachangia maambukizi ya ukimwi hilo nalo ni tatizo tukitambua ukimwi sasa ni janga la kitaifa. Hivyo hamna budi kuwa waangalifu na matumizi ya fedha�. Aliongeza.
 
CCM Kuongeza kiwango cha MadiniBy Mike Mushi | Published 11/26/2005 | Habari Mpya |
CCM Kuongeza kiwango cha Madini


shein-2005-52.jpg

Chama Cha Mapinduzi kinakusudia kuongeza kiwango cha thamani ya madini kutoka asilimia 0.3 ya hivi sasa hadi kufikia asilimia 3 iwapo chama hicho kitashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk Ali Mohamed Shein amesema pamoja na kuongeza viwango vya madini hayo pia serikali ijayo itahakikisha inatengeneza vito vya madini hapa hapa nchini ili kuweza kuuza madini kwa tija.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Londoni wilayani Manyoni.

Amesema suala la madini limepewa kipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005-2010 kutokana na ukweli kwamba sekta ya madini inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua uchumi wa nchi.

Amewaambia wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa ili kufanikisha azma hiyo serikali itatoa mikopo na elimu kwa wachimbaji wadogo wadogo kwa njia ya semina na mikutano ili waweze kujua namna ya kuchimba madini hayo kitalaam.

�Baada ya kupewa mikopo, mpewe elimu kwa njia ya semina, mikutano au warsha mjue namna ya kuchimba madini hayo kitalaam�. Aliwaeleza wananchi hao ambao wengi wao ni wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu katika eneo hilo.

Dk. Shein amethibitisha kuwa serikali ya awamu ya nne itaendelea kukaribisha wawekezaji wakubwa katika sekta ya madini na pia itaangalia upya sera yake ya madini ili iweze kuwanufaisha wadau wote.

Amesisitiza wananchi wakichague Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndio chama pekee kinachoonyesha jitihada za kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kuweza kupambana na umasikini hali ambayo hatmae itawafanya kuwa na maisha bora.

Katika hatua nyingine Mgombea Mwenza huyo amewataka wachimbaji wadogo wa madini nchini kutumia fedha wanazozipata kwa kujijenga kimaisha kwa kuwa na nyumba bora, kutunza afya zao na kusomesha watoto na sio kwa anasa.

�Fedha ni fedheha, zikiwa nyingi zinachanganya kidogo hujui utazifanyia nini, unaishia sehemu ukiulizwa wewe nani na wewe unauliza pia wewe nani. Huo si utumiaji mzuri wa fedha�. Alisema Dk Shein

�Hata hivyo starehe zikizidi inachangia maambukizi ya ukimwi hilo nalo ni tatizo tukitambua ukimwi sasa ni janga la kitaifa. Hivyo hamna budi kuwa waangalifu na matumizi ya fedha�. Aliongeza.

Kumbe ni CCM ndiyo inayopanga bei za madini? Je watajitetea kuwa wanamaanisha ni utekelezaji wa sera zao pale wanapochanganya kati ya majukumu ya chama na yale ya serkali? And if thats the case then CCM ni Mafisadi?
Kwanini mali nyingi za Umma wamezichukua kwa madai ni za CCM?
Wapi tofauti kati ya chama na serikali pale inapokuja kwenye masuala ya utaifa?
Swali:
1)Nani fisadi?

a)CCM

b)serikali

c)CCM na Serikali

d)hakuna tofauti kwani serikali inatokana na CCM

e)Yote hapo juu yaweza kuwa majibu

Mjadala uanze!
 
Wote tunaweza tukawaita mafisadi na pia tunaweza tukasema pia none of them, inategemea reference yetu tunataka iwe wapi. Kama ni kulinganisha chama na chama au serikali na serikali, then wanaweza wakaitwa collectively mafisadi, otherwise ni vema ku-pinpoint individuals ndani yake waliojijengea hiyo tabia. Tatizo ni kuwa ni wengi mno.
 
Chama cha mafisadi ndio kimeshika utamu. Kwa hiyo kama viongozi wa serikali wanatoka katika chama cha mafisadi basi serikali pia imejaa mafisadi na ni fisadi pia. Utakuwaje sio fisadi kama mafisadi wanaachiwa wanapeta tu bila kuchukuliwa hatua zozote?
 
MAFISADI ni wanachama wachache wa chama cha mapinduzi ambao wamefuzu na kupata degree za utapeli na kutumia professional hiyo katika kuhakikisha wanawateka nyara wanachama wote wa CCM, hili wawasaidie kushika dola na kuwa na baraka za kuongoza serikali.

Hawa watu mara nyingi huwa hawana huruma siyo tu kwa wananchi, pia kwa wanachama wenzao.

Hii huwa mara nyingi inahitaji elimu ya kutosha hasahasa kwa watu wanaotumika.

Kuna wazee vijijini ni wanachama wa CCM lakini ni hoehae hawajui hili wala lile. wao sana sana ni wakereketwa na wanadamudamu hila Mafisadi huwa hawaoni huruma kwa hao wazeee.

Kazi kwetu ni kutoa Elimu kwa wana CCM wanaowaabudu hili waweze kuwaona kuwa kumbe ni MAFISADI.

Sula la kupanga bei na kusaini mikataba ni serikali ya CC ambapo baaadhi ya migodi ukifuatilia pamoja na kwamba signature ni ya mkanada lakini anayemiliki ni FISADI wa CCM, then anaweza kuadjust muda wowote.
 
baba akiwa fisadi kwa mtoto inakuwa sio dhambi

CCM Wamekuwa wakikanusha kuwa wao sio mafisadi!
Na ni wazi kuwa Serikali inatoa viongozi wake kutoka kwenye chama kinachotawala!
Sasa ina maana wakishaingia serikalini wao sio wana CCM tena?
Na kutokana na kauli yako hapo juu inaelekea unataka kusema kuwa CCM ni baba na Serikali ni mtoto?
 
Chama Cha Mapinduzi kinakusudia kuongeza kiwango cha thamani ya madini kutoka asilimia 0.3 ya hivi sasa hadi kufikia asilimia 3 iwapo chama hicho kitashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.

PIA NI WAKATI WA KUFUATILIA KAMA NI KWELI HILO HAPO JUU LIMEFANYIKA!
JE HIYO 0.3-3% LIMEFANYIWA KAZI? Na je baada ya kupanda huko kwa thamani..Nani mfaidika? CCM peke yao ama Taifa kwa ujumla?
TUNATAKA USHAHIDI NA SI HOTUBA!
 
Wote tunaweza tukawaita mafisadi na pia tunaweza tukasema pia none of them, inategemea reference yetu tunataka iwe wapi. Kama ni kulinganisha chama na chama au serikali na serikali, then wanaweza wakaitwa collectively mafisadi, otherwise ni vema ku-pinpoint individuals ndani yake waliojijengea hiyo tabia. Tatizo ni kuwa ni wengi mno.

Walisema watapandisha thamani ya madini kutoka aslimia 0.3 hadi kufikia asilamia 3!
Waweke data hapa na watuonyeshe kama hizo pesa zimefanya nini kwa wananchi!
 
Walisema watapandisha thamani ya madini kutoka aslimia 0.3 hadi kufikia asilamia 3!
Waweke data hapa na watuonyeshe kama hizo pesa zimefanya nini kwa wananchi!

Kuna habari nyingine zenye utata kuwa CCM inaendelea kupinga kwamba wao si mafisadi!

Kauli hizo za kuchanganya zimedaiwa kutolewa na wale wanaodai kuwa Mafisadi ni aibu kupokelewa na wana CCM huko majimboni mwao!

Kwi kwi kwi kwi..Wastake ncheke!

NB: Ngoja nikaitafute niilete hapa!
 
Hii hapa!

`Mapokezi ya Chenge aibu`

2008-05-10 11:37:18
Na Pendo Fundisha,PST, Mbeya


Baadhi ya wakazi wa Mbeya na viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa, wamelaani mapokezi ya Mbunge wa Bariadi Magharibi, Bw. Andrew Chenge (CCM) na wanachama wake kwa madai kuwa yanakidhalilisha chama hicho na kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete.

Walisema hakuna sababu za msingi za kuwafanyia mapokezi makubwa watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, kwa kuwa kwa kufanya hivyo wanazorotesha juhudi za chama hicho na serikali katika vita yake dhidi ya ufisadi.

Mapokezi ya aina hiyo ni ya pili kufanyika baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu Bw. Edward Lowassa kujiuzulu wadhifa wake baada ya kuhusishwa katika kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond iliyodaiwa kupata zabuni kwa njia ya utata.

Baada ya kujiuzulu kwake Februari mwaka huu, Bw. Lowassa alifanyiwa mapokezi makubwa jimboni kwake Monduli, mkoani Arusha.

Bw. Chenge alijiuzulu wadhifa wa Waziri wa Miundombinu mapema mwezi uliopita, baada ya kufichuliwa kwa habari kwamba anamiliki zaidi ya Sh. Bilioni 1.2 ambazo zimehifadhiwa katika akaunti moja nje ya nchi. Fedha hizo zinadhaniwa kuwa zilipatikana kifisadi katika \'dili\' la ununuzi wa rada ghali ambayo kimsingi Tanzania ilikuwa haiihitaji.

Baada ya kujiuzulu Bw. Chenge wiki hii alikwenda jimboni kwake na kupokelewa na msafara mkubwa wa magari na wapiga kura wake wakiwemo makada wa vyama.

Wakizungumza juzi jioni walipokuwa wakiangalia taarifa za habari katika televisheni mbalimbali zilizokuwa zikionyesha mapokezi hayo yaliyohudhuriwa na baadhi ya makada wa CCM wakiwa katika makundi, walidai huo ni udhalilishaji wa chama hicho na viongozi wake.

Wakiongea na PST baadhi ya viongozi hao walidai kuwa imekuwa ni kejeli kwa serikali pale viongozi wa ngazi za juu waliokumbwa na tuhuma za ufisadi na kujiuzulu na kukimbilia katika majimbo yao kujisafisha.

``Kwa kweli wananchi, hususan wanachama wa CCM mnapaswa sasa kugeuka na kuangalia ni nini kinachofanywa na viongozi wa ngazi za juu, na si tu kujipanga katika barabara na ofisi za chama kwa ajili ya mapokezi ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Mnajidhalilisha kwa kunufaisha mafisadi na nyinyi wananchi wenye maisha duni mkizidi kupandishiwa gharama za maisha,`` alisema kiongozi mmoja.

Walisema wananchi walikuwa wakisubiri kauli ya serikali kupitia kwa Rais Kikwete dhidi ya hatua za makusudi zinazochukuliwa dhidi yao, lakini kila kukicha wanawasikia watuhumiwa wakikimbilia majimboni kwao na vyama vyao vikiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika mapokezi na kwenye mikutano ya hadhara.

Naye mwananchama wa CUF, mkazi wa kitongoji cha Majengo, Bw. Augustino Amani, alisema serikali ilipaswa kufumbua macho na kuwaeleza wananchi hatma inayochukuliwa dhidi ya watu wanaotuhumiwa na ufisadi.

Alisema kwa sasa serikali inapaswa kuwa wazi kwa wananchi na si kuwanyonya kwa kuwapandishia gharama za maisha kutokana na gharama za bidhaa hususan, mafuta, mazao ya chakula kama mahindi na kumfanya mwananchi mwenye kipato cha chini kushindwa kumudu kupanda kwa gharama hizo.

  • SOURCE: Nipashe
 
Tumshagundua MFISADI NA MAFIA NI SERIKALI YETU NA CHAMA CHA CCM!
 
jmushi ....y do u ask and then answer and give conslusion urself?
if u knew the answer from the beggining y ask?
and if u dont know the answer....y conclude?
 
jmushi ....y do u ask and then answer and give conslusion urself?
if u knew the answer from the beggining y ask?
and if u dont know the answer....y conclude?

Ofcourse i do so unless proven otherwise.Kwani huoni CCM inataka kujisafisha huku ikitufanya tuamini yenyewe ni safi na wakati na hao hao MAFISADI MAFIOSO wako kwenye madaraka kotekote?Mwenyekiti wa CCM si ndiye rais?Sasa unamletea nani vijikauli vya kishenzi?Kaa kushoto kama hauna hoja za kupinga na usinijie na vijikauli vya kipuuzi kama baadhi yenu mnavyofanya hapa JF kwa majina lukuki!Mimi niko hapa na I SWEAR TO GOD hakuna ku turn BACK!For better or worse i am well prepared!Kima haingaliwi USONI this time around gayujini
 
jmushi, ukiongea ungejaribu kupangilia paragraph ili watu wakuelewe kirahisi kile unachikisema.
kwa ghafla nilishindwa kuelewa kama unanimaanisha mie nilikujia na vijikauli vya kipuuzi au hivyo vijikauli vya kipuuzi vinatoka kwa kikwete, kwa sababu umekusanya hoja mbili tofauti kwenye paragragh moja.
dont be too defensive, unapofunzwa kitu jaribu kuelewa, na ukishindwa kuelewa uliza. sio kukurupuka na kuita vijikauli vya kipumbavu au majina lukuki wanayokuja nayo watu hapa.
hakuna mtu alokwambia uondoke JF to begin with, inashangaza kuona unamuapa mungu kuwa wewe upo hapa na hakuna ku turn back.
polepole ndugu usije ukaanza kupigana na kivuli chako mwenyewe. sie kila anayekukosoa adui wako. na sie kila anayekuitikia ni mwema wako.
 
jmushi, ukiongea ungejaribu kupangilia paragraph ili watu wakuelewe kirahisi kile unachikisema.
kwa ghafla nilishindwa kuelewa kama unanimaanisha mie nilikujia na vijikauli vya kipuuzi au hivyo vijikauli vya kipuuzi vinatoka kwa kikwete, kwa sababu umekusanya hoja mbili tofauti kwenye paragragh moja.
dont be too defensive, unapofunzwa kitu jaribu kuelewa, na ukishindwa kuelewa uliza. sio kukurupuka na kuita vijikauli vya kipumbavu au majina lukuki wanayokuja nayo watu hapa.
hakuna mtu alokwambia uondoke JF to begin with, inashangaza kuona unamuapa mungu kuwa wewe upo hapa na hakuna ku turn back.
polepole ndugu usije ukaanza kupigana na kivuli chako mwenyewe. sie kila anayekukosoa adui wako. na sie kila anayekuitikia ni mwema wako.

Huna haja ya kuniambia nani ni nani...Watu mutajionyesha wenyewe tu!Nani kakwambia nimekimbia?Kwani si kuna watu hapa wenye uhusiano na Familia ya Ballali ambao hawataki azungumziwe kwasababu amekufa na hali yake ilikuwa mbaya sana?Usinletee kizunguzungu hapa na kusema unanifunza...Hapa tutajifunza tu!Nimeshalalamika kuhusu maandshi yangu!Nikirekebisha bado saa nyingine yanabaki kama kituko!Who knows whats going on?
 
Huna haja ya kuniambia nani ni nani...Watu mutajionyesha wenyewe tu!Nani kakwambia nimekimbia?Kwani si kuna watu hapa wenye uhusiano na Familia ya Ballali ambao hawataki azungumziwe kwasababu amekufa na hali yake ilikuwa mbaya sana?Usinletee kizunguzungu hapa na kusema unanifunza...Hapa tutajifunza tu!Nimeshalalamika kuhusu maandshi yangu!Nikirekebisha bado saa nyingine yanabaki kama kituko!Who knows whats going on?

Hao ndugu zao kina Ballali ni wangapi hapa jamvini? baba una matatizo wewe sasa.
 
nilichokisema na balali kinahusiana nini?
na nilikwambia umekimbia? usikurupuke, soma taratibu kilichoandikwa, jipange, jenga hoja, kisha ndo andika.
na hiyo ya kuwa umelalamika maandishi yako ndo unataka kutuambia wewe unaogopwa sana kiasi cha kuwa maandishi yako yamekuwa tempered with! gosh what an imagination
 
Wakati naondoka kwa muda nilikuwa niko kwenye mjadala wa Ballali.Jasusi hakupenda jinsi mjadala ulivyokuwa ukienda kutokana na uhusiano wake wa karibu ama undugu na familia ya Ballali.Na kuna wengi tu wali sympathise naye.Nikatukanwa.Nikaamua kukaa pembeni.Mijadala ikaendelea...Na sasa nimerudi..Ila nataka ujue jambo moja.Kama jinsi ilivyo kwa Ballali ambaye ana watu wenye kumwonea huruma hapa JF...Na mimi pia nina haki ya kufanya hivyo lakini mapenzi yangu kwa Taifa yamezidi nguvu.Kwa mfano ilikuwa ikiniwia vigumu sana kujadili issue ya EPA bila ya kumtaja mama Meghji ambaye hata familia yangu inamweshimu na watoto zake kina Mahir,Nyangu na Jamila ni watu safi sani na nimesoma nao na pia kuwa marafiki wa hapa na pale.Marehemu Mzee Ramdhani alikuwa kipenzi na licha a matatizo ya kifamilia yaliyotokana na majukumu...Bado tuliendelea kuwaheshimu wote...Pamoja na Mama Meghji mwenyewe.Sasa mimi siwezi kuwa na huruma na hawa watu?Ninatumia pia nafasi hii kumuomba mama Meghji afanye kila awezalo ili kuweza kujiondoa kwenye mijadala hii ya Mafisadi kwasababu ya heshma.Ila sijaamua kuchukua uamuzi wa kumtetea Mama kama wengine walivyofanya kwa Ballali hadi hapo kutakapokuwa na ukweli wenye kukubalika machoni mwa wananchi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom