Nani awajibike kwa uteuzi unaogongana wa wakuu wa wilaya na wakurugenzi? watumishi hewa watakwisha?

iparamasa

JF-Expert Member
Nov 14, 2013
13,438
14,916
Najiuliza tu....kama ngazi ya juu kabisa ya uteuzi inachanganya mambo kwenye uteuzi wa watu wasiozidi 300, je kuna dalili za wafanyakazi hewa kuisha? Maana binafsi naona ka hewa kalikuwa kametengenezwa.

Pia mbona hatusikii mtu katumbuliwa kwa uzembe huu
 
Ungejua tu hili neno "watumishi hewa" ni sifa ya kutosha na imemjengea imani kiongozi aliyelibua kwa anawaongoza usinge hangaika kuja na hii hoja yako.
 
Najiuliza tu....kama ngazi ya juu kabisa ya uteuzi inachanganya mambo kwenye uteuzi wa watu wasiozidi 300, je kuna dalili za wafanyakazi hewa kuisha? Maana binafsi naona ka hewa kalikuwa kametengenezwa.

Pia mbona hatusikii mtu katumbuliwa kwa uzembe huu
Wanapika wenyewe wanaunguza wenyewe kwa hiyo haina shida sisi tutakula tu hata wasivyoivisha
 
Nikivuta hisia namwona Mhe.Simbachawane usoni yuko neutral lakini moyoni analia. Analia kwa sababu watu muhimu wa kufanya nao kazi wengi wao hawajui hata pakuanzia. Amesukumiwa watu tu==eti makada==hv ktk local gvt hakuna watumishi wenye sifa halafu makada==wengi sana==sidhani kama una la kufanya, kaa kimya, umia ndani kwa ndani, ukionyesha kutoridhika, utatumbuliwa. Simbachawene unajua kwamba hao wateule ambao hawana sifa watakaribishwa na maafisa wa halmashauri waliokata tamaa (demoralised). Vyeo walivyostahili kuvipata wao kwa mujibu wa sheria na kanuni za utumishi, leo wanaletewa strangers!! Kazi unayo mheshimiwa. Huko Kuna enda kutokea mambo mawili== ama wakurugenzi watakuwa maboya yaani wataendeshwa na maafisa wazoefu na madiwani au watakuwa ma dikteta kulazimisha mambo yaende watakavyo. Yote yatakuwa na matokeo hasi kwa wakurugenzi hao na kwa halmashauri. Jiandae kisaikolojia mhe. Simbachawene na mm nakuombea Mungu akulinnde na dhoruba ijayo. Pole Sana.
 
Kama namuona Simbachawene anavyofikiria hatma yake. Kwa hali hii mzee unatumbuliwa mapeeeeema. Pole sana. Najua ulijipanga ili kujipambanua kwamba wewe ni bora na unaweza kuongoza vizuri wizara kubwa kuliko zoote.
 
Mi naona siku zote tangu nyuma ndivyo walikuwa wanachaguana hivyo na sijapata ona ccm wanampa mtu cheo bila kujiridhisha chama chake lakini nimeshangaa sana mwaka huu watu wengi wanahoji kana kwamba utaratibu huo ni mpya Katk nchi hii. Binafisi nasema utaratibu huo upo tangu enzi na enzi haujaanza leo. Asante
 
Mi naona siku zote tangu nyuma ndivyo walikuwa wanachaguana hivyo na sijapata ona ccm wanampa mtu cheo bila kujiridhisha chama chake lakini nimeshangaa sana mwaka huu watu wengi wanahoji kana kwamba utaratibu huo ni mpya Katk nchi hii. Binafisi nasema utaratibu huo upo tangu enzi na enzi haujaanza leo. Asante


Kwa kifupi:utaratibu wa mwaka huu ni mpya...
 
Kama namuona Simbachawene anavyofikiria hatma yake. Kwa hali hii mzee unatumbuliwa mapeeeeema. Pole sana. Najua ulijipanga ili kujipambanua kwamba wewe ni bora na unaweza kuongoza vizuri wizara kubwa kuliko zoote.

Yeye Simbachawene ndiye amependekeza wateuliwa na anataka aanze na watu wake kwa hiyo tusubiri KAZI TU.
 
Hawezi kupata shida. Ni makada wenzake. Watajadili kichama na kuamua kichama kwa manufaa ya chama....
 
Yeye Simbachawene ndiye amependekeza wateuliwa na anataka aanze na watu wake kwa hiyo tusubiri KAZI TU.
Hivi alimpendekeza na huyu:
13627019_1094739947252578_3140010939220737602_n.jpg
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom