jamadari
JF-Expert Member
- Feb 13, 2010
- 295
- 92
Marmo awaponda wanaokusudia kuandamana kuhusu Richmond
Tuesday, 02 March 2010 08:38
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo (pichani), amewashangaa wanaharakati wanaotaka kuandamana kupinga maamuzi ya Bunge juu ya sakata la Richmond na kubeza azma yao hiyo kwa kusema kuwa haitaleta mabadiliko yoyote.
Waziri Marmo aliyasema hayo alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari ofisini kwake jijini jana.
Alisema Bunge limekwishamaliza kazi baada ya kuridhishwa na utekelezaji wa Serikali dhidi ya maazimio 23 ya Bunge katika suala la Richmond na kwamba yale ambayo hayajatekelezwa, yanashughulikiwa na mamlaka husika serikalini.
Alionya kuwa Bunge linafanyakazi chini ya kanuni zake ambazo alisema ni kama sheria za nchi.
Alipoulizwa iwapo Serikali itakutana na wanaharakati ili kujadili suala hilo, alijibu Sisi tunajaribu kuwaelimisha lakini hatudhani kama maandamano yatatatua jambo lolote," alisisitiza.
Kuhusu Kampuni ya Kupakia na Kupakua Makontena katika bandari ya Dar es Salaam (Ticts) na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), alisema mambo hayo bado yanashughulikiwa na Serikali.
Muungano wa asasi za Kiraia zinazotetea Usawa wa Jinsia, Haki za Binadamu, Maendeleo ya Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi (FemAct), unawataka wanaharakati hao kuandamana kwa lengo la kuonyesha kutoridhishwa na Bunge.
Wanaharakati hao wanadai kuwa Bunge halikutimiza wajibu katika taarifa zilizofikishwa katika mkutano wake wa 18, kwa kuwa hawakuweka bayana kasoro za Bunge katika kushughulikia masuala ya Richmond, Kampuni ya Ticts, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu ulioathiri binadamu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Loliondo.
Taarifa ya Loliondo haikuwasilishwa bungeni wakati ile ya Ticts na TRL hazikujadiliwa kutokana na kile kilichoelezwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa taarifa hizo zilikuwa hazijaiva.
Taarifa hizo zimepangwa kuwasilishwa na kujadiliwa katika Mkutano wa 19 wa Bunge uliopangwa kufanyika Aprili, mwaka huu.
CHANZO: NIPASHE
Tuesday, 02 March 2010 08:38
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo (pichani), amewashangaa wanaharakati wanaotaka kuandamana kupinga maamuzi ya Bunge juu ya sakata la Richmond na kubeza azma yao hiyo kwa kusema kuwa haitaleta mabadiliko yoyote.
Waziri Marmo aliyasema hayo alipokuwa akijibu maswali ya waandishi wa habari ofisini kwake jijini jana.
Alisema Bunge limekwishamaliza kazi baada ya kuridhishwa na utekelezaji wa Serikali dhidi ya maazimio 23 ya Bunge katika suala la Richmond na kwamba yale ambayo hayajatekelezwa, yanashughulikiwa na mamlaka husika serikalini.
Alionya kuwa Bunge linafanyakazi chini ya kanuni zake ambazo alisema ni kama sheria za nchi.
Alipoulizwa iwapo Serikali itakutana na wanaharakati ili kujadili suala hilo, alijibu Sisi tunajaribu kuwaelimisha lakini hatudhani kama maandamano yatatatua jambo lolote," alisisitiza.
Kuhusu Kampuni ya Kupakia na Kupakua Makontena katika bandari ya Dar es Salaam (Ticts) na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL), alisema mambo hayo bado yanashughulikiwa na Serikali.
Muungano wa asasi za Kiraia zinazotetea Usawa wa Jinsia, Haki za Binadamu, Maendeleo ya Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi (FemAct), unawataka wanaharakati hao kuandamana kwa lengo la kuonyesha kutoridhishwa na Bunge.
Wanaharakati hao wanadai kuwa Bunge halikutimiza wajibu katika taarifa zilizofikishwa katika mkutano wake wa 18, kwa kuwa hawakuweka bayana kasoro za Bunge katika kushughulikia masuala ya Richmond, Kampuni ya Ticts, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu ulioathiri binadamu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Loliondo.
Taarifa ya Loliondo haikuwasilishwa bungeni wakati ile ya Ticts na TRL hazikujadiliwa kutokana na kile kilichoelezwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuwa taarifa hizo zilikuwa hazijaiva.
Taarifa hizo zimepangwa kuwasilishwa na kujadiliwa katika Mkutano wa 19 wa Bunge uliopangwa kufanyika Aprili, mwaka huu.
CHANZO: NIPASHE