Nani atakuja kutufidia sisi kama nchi kutokana na mradi usio na tija wa SGR?

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Kwakweli huu mradi kila nikiuangalia na complications zake huwa nakuna kichwa sana na kujiuliza kina nani walipendekeza mradi wa aina hii?

Pamoja na usanifu wake kujikita kwenye gharama za juu bado sijawahi kuona faida ya mradi huu na sijui kama utakuja kukamilika. Mbaya zaidi umeshatushinda kuuendeleza kwa wakati.

Kiukweli nchi yetu ni masikini sana na hakukuwa na tija yoyote kubuni mradi ambao utakula zaidi ya trilioni 7 Tshs fedha za awali huku ukiwa hauna maana kwa nchi.

Hivi ni mizigo kiasi gani itakayo kuwa inapita kwenye hiyo reli hadi tuigharamie hivyo?

Bomba la mafuta limefeli na sasa Uganda ameamua kuegemea Kenya zaidi, serikali yetu bado haijatueleza ni kwanini? Huu mradi utakuwa unatumiwa na watu wa kanda ya ziwa kusafirisha matikiti maji?

Yani Rais Magufuli kwakuwa ana nguvu ya kutumia fedha za nchi basi amekuwa akizitumia kwa utaratibu mbovu kweli.

Sioni pia tija kwenye daraja la coco beach baada ya serikali kuhamia Dodoma, sioni tija yoyote kwenye daraja la huko sijui busisi kanda ya ziwa dah yani watanzania wengi wanataabika ili kugharamia miradi isiyo na tija yoyote ile.
 
Mkiona Kenya wanafanya kitu msikimbilie kuwaiga mtapotea. Kenya wako tayari kuingia hasara ili nyie muwaige na muwaingie hasara mara kumi zaidi ili mfilisike na kutopea kwenye ufukara mkuu
 
tumeshindwa kuiendesha reli ya kati na Tazara kwa tija tutaiweza hiyo ya umeme? huwa namuonea huruma jiwe siku zote kwani analenga kupatia sifa ndio maana anatumia mabavu
Tazara wana treni mbili. Ordinary na Express. Express ni ya wazambia ordinary ya watanzania. Hiyo express inaondoka ijumaa kutoka dar ndo wanapanda wageni wote( wazungu, wachina, wakorea etc) hiyo ya ordinary inatoka dar jumanne ni kichefuchefu. Kwanza ni chafu, mbovu, inaharibika ovyo njiani. Watanzania nani aliwaroga et?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umetumia haki yako ya kikatiba na kifikra katika kutueleza jinsi gani bado unahitaji elimu zaidi kwenye masuala ya uwekezaji wa kitaifa!
Huwezi kunifundisha kitu kuhusu haya mambo. Pia huwezi kuelewa nilicholalamikia na naelewa nyie wapiga makofi wa awamu hii kila kitu anachotoa Magufuli nyie kazi yenu ni kupokea bila kuhoji.
 
Mkiona Kenya wanafanya kitu msikimbilie kuwaiga mtapotea. Kenya wako tayari kuingia hasara ili nyie muwaige na muwaingie hasara mara kumi zaidi ili mfilisike na kutopea kwenye ufukara mkuu
Kenya mbali na kuweka kipande kifupi ila inaweza kuwa na tija kidogo mbali na kuwa inawatoa jasho kweli kweli.
 
G Sam,
Serikali haipati hasara in Magufuli s voice,Hahaha utadhani serikali ina mtambo wa kuzalisha fedha,au yeye anatuona watanzania ni robots?
 
Back
Top Bottom