Bombadier Mama
Member
- Feb 3, 2018
- 13
- 6
NANI ATAKAYEOKOA TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania ni Taasisi ya serikali iliyoundwa kwa sheria ya Nguvu za Atomiki Na. 7 ya mwaka 2003. Tume hii inayo majukumu makubwa mawili yakiwa ni kusimamia matumizi salama ya vifaa vyote vinavyotoa mionzi ayonisha na isiyoayonisha kwa ajili ya usalama wa wagonjwa, wafanyakazi, wananchi na mazingira kwa ujumla na kuishauri serikali matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Taifa.
Itakumbukwa kwamba mnamo Juni 2016 Mkurugenzi Mkuu wa Tume hii Prof. Iddi Nyangarika Mkilaha alifariki kwa kujipiga risasi nyumbani kwake jijini Dar es salaam na kufanya Tume kuongozwa na kaimu Mkurugenzi Mkuu aliyekuwa ameteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Tume mpaka Septemba 2016 ambapo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilipoleta Kaimu Mkurugenzi Mkuu kutoka Jeshi la Wananchi Brigedia Jenerali Fulgence Simon Msafiri kukaimu nafasi hiyo mpaka sasa.
Ijulikane wazi kuwa tangu kupewa nafasi ya kukaimu Mkugenzi huyu Mkuu sasa ni zaidi ya mwaka mmoja kama inavyojieleza hapo juu. Mkurugenzi huyu amekuwa akifanya mabadiliko mbalimbali katika Tume ambayo mengi ya mabadiliko hayo yamekuwa ni kwa manufaa yake binafsi pamoja na baadhi ya viongozi ambao amekuwa akiambatana nao katika kufanya maamuzi ambayo yamekuwa yakiumiza Taasisi pamoja na wafanyakazi na kuwapunguzia morali za kufanya kazi hii ikiwa ni pamoja na kuhamisha wafanyakazi na wengine kuwafukuza kazi bila hata sababu za msingi na kufuata taratibu za utumishi wa umma.
Aidha yapo mambo ambayo wanaohusika na usimamizi wa TUME hii muhimu kwa maendeleo na usalama wa Taifa katika matumizi ya teknolojia ya nyuklia wanatakiwa kuyangalia kwa ukaribu ili kuifanya Tume hii itimize majukumu yake ya msingi katika ofisi zake ambazo ni Arusha Makao Makuu, Dar es salaam, Zanzibar, Mpaka wa Namanga, Mpaka wa Sirali, Ruvuma, Mtwara,Mpaka wa Holili, Mpaka wa Tarakea, Mpaka wa Tunduma, Mpaka wa Rusumo, Mpaka wa mutukula, Mpaka wa Horohoro na Bandari ya Tanga. Ijulikane pia kuwa ukiacha ofisi ya Makao makuu na Ruvuma ofisi zingine zote zinajishughulisha zaidi na usimamizi wa viwango vya mionzi kwenye vyakula vya binadamu na mifungo ambavyo vinaingizwa na kutolewa nje ya nchi ambayo ni sehemu ndogo ya majukumu ya msingi ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania.
Yapo mambo ambayo ni vizuri kuyaonyesha ambayo yanaendelea katika TUME ili wanahusika waweze kuyafanyia kazi kama itapendeza ni kama ifuatavyo
i. Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Wafanyakazi,
ii. Uwepo wa chama cha wafanyakazi na uanachama wa wafanyakazi,
iii. Kutokufanyika kwa vikao vya Baraza la Wafanyakazi,
iv. Fukuza fukuza ya wafanyakazi kwa makosa ya kusingiziwa
v. Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Bodi ya wakurugenzi, na
vi. Uhamisho wa wafanyakazi usio na tija
vii. Ufisadi ndani ya Tume
Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Wafanyakazi
Kumekuwa na mahusiano mabaya na uoga kati ya watumishi wa Tume na timu ndogo ya menejimenti (Kaimu Mkurugenzi mkuu, Mkurugenzi wa utawala na fedha na Mwanasheria wa Tume) na wafanyakazi wengine kwamba wafanyakazi wanatakiwa kufanya lile ambalo hawa wanalitaka liwe vinginevyo utakuwa mhanga katika utumishi wako katika tume hii. Hili limepelekea mpaka hata vikao vya mikutano kati ya wafanyakazi na Menejimenti vimekuwa ni vya maagizo tu na hakuna kutoa mawazo wala kuuliza swali ukifanya hivyo unakuwa unatafuta tatizo katika utumishi wako. Aidha imepelekea hata wageni wa wizara wanapotembelea TUME hii kukosa kujua ukweli wa hali ya TUME maana ripoti za uongo zimekuwa zikitolewa kuwa mahusiano kati utawala na wafanyakazi ni mazuri na akitokea mfanyakazi akauliza swali katika ugeni huo basi atengemee mambo mawili kuhamishwa makao makuu au kufukuzwa kazi. Jambo hili limechangiwa kwa sehemu kubwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia hususani Naibu Katibu Mkuu (Sayansi) ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila ambaye alitoa maelekezo yasiyo sahihi kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu. Tunaomba Wizara iliangalie upya suala hili katika Tume ili kufanya tume ifanye kazi kwa mafanikio na kurejesha morali ya wafanyakazi ya kufanya kazi kwa ufanisi na si kwa vitisho ambavyo vinaendelea ambavyo havina tija kwenye Tume na Taifa kwa ujumla. Tunashauri uchunguzi ufanyike ubaini ukweli wa jambo hili.
Uwepo wa chama cha wafanyakazi na uanachama wa wafanyakazi
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania ni moja ya Taasisi za utafiti na zinazojishughulisha na mambo ya Sayansi na Teknolojia ikiwepo ukaguzi wa vifaa na majengo yanayotumika vifaa vinavyotoa Mionzi ya Nguvu za Atomiki (geji zinazotumika katika utafiti wa madini na gesi, mashine za uchunguzi na matibabu ya kansa kwa mionzi, mashine za X-ray, mashine za CT na mashine zinazotumika viwandani na katika matengenezo ya barabara ambazo zinatoa mionzi, n.k) hivyo kuifanya wafanyakazi wake kuwa chini ya Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Ufundi Stadi, Habari na Utafiti (RAAWU). Tangu Kaimu Mkurugenzi Mkuu aanze kazi Septemba 2016 amekuwa akifanya kazi ya kuwatoa wafanyakazi kwenye chama cha wafanyakazi kwa kigezo cha kuwapa madaraka ya ukuu wa Idara, Vitengo na Ukurugenzi. Jambo ambalo UTUMISHI kupitia nyaraka mbalimbali lilishatolewa maelekezo katika utekelezaji wako. Hili lilifanya viongozi wa chama cha wafanyakazi Tawi, Mkoa, Kanda na Taifa kumshauri Kaimu Mkurugenzi Mkuu kutokuwatoa wafanyakazi katika chama kwa kuwa ni haki yao ya msingi ila tu pale anapowateua kwa nafasi ya uongozi katika taasisi basi waache nafasi za uongozi katika chama na kutumikia nafasi zao za uteuzi lakini waendelee kuwa wanachama wa chama cha wafanyakazi kwa mujibu wa sheria. Pamoja na ushauri huo Kaimu Mkurugenzi Mkuu hakuwa tayari kubadili msimamo wake wa kuwatoa wafanyakazi kwenye chama jambo ambalo lilifanya aingie kwenye mgogoro na viongozi wa Tawi wa chama cha wafanyakazi kwa kuwahusisha na tuhuma ambazo sio za kweli ikafikia wengine kuwahamisha kutoka kwenye Tume na viongozi wengine kuwaondoa makao makuu na kuwapeleka ofisi za kanda na mipakani kama adhabu. Moja ya viongozi walihamishwa katika Tume ni Katibu wa Chama Tawi ambaye alihamishwa mwezi Aprili 2017. Mahusiano mabaya na chama hayakuishia hapo bali yaliendelea mpaka ilipofika mwezi Oktoba 2017 alimfukuza kazi Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi kwa kosa la kutumia simu ya ofisi kwa mawasiliano na wafanyakazi katika kutimiza majukumu yake ya Chama cha wafanyakazi. Kutokana na unyanyasaji huu kwa viongozi wa chama cha wafanyakazi viongozi wengine wa chama katika Halmashauri ya Chama Tawi waliomba kuachia nafasi zao za uongozi na kubaki wanachama wa kawaida ili kuepusha migongano katika Tume. Mpaka tarehe ya ujumbe huu kuanzia Oktoba 2017 hakuna kiongozi hata mmoja wa chama cha wafanyakazi maana mwenyekiti ndio alibaki ambaye amefukuzwa kazi. Kutokana na mgogoro huo hakujafanyika kikao chochote cha Baraza la Wafanyakazi tangu Aprili 2017 mpaka sasa na nyaraka mbalimbali zimelazimishwa kupitishwa bila ushiriki wa baraza la wafanyakazi. Hili pia wanaohusika na usimamizi wa utendaji wa TUME wanaweza kulifuatilia na kujua ukweli wake.
Kutokufanyika kwa vikao vya Baraza la Wafanyakazi
Kaimu Mkurugenzi Mkuu amekuwa akiendesha Tume bila kuwepo kwa vikao vya mabaraza ya wafanyakazi kutoka mwezi Aprili 2017 alipofanya kikao cha mwisho kwa dakika tatu (3) na kuwalipa wajumbe zaidi ya Ishirini na Tano (25) kila mmoja 150,000/= ambayo kwa upande mmoja yalikuwa ni matumizi mabaya ya fedha ya serikali ila kwa kuwa kulipa au kutokulipa ni maamuzi yake na timu yake hili lilifanyika. Vikao hivyo vya Baraza havijafanyika mpaka sasa ni zaidi ya vikao vitatu kutokana na mgogoro wa kutokutaka chama cha wafanyakazi katika Tume. Hali kadhalika jambo hili linaweza kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kujua ukweli wake na wahusika wenye dhamana ya kusimamia utendaji wa Tume. Ijulikane wazi kwamba kuwa kutokufanyika vikao hivi ni kupunguza ushirikishwaji wa wafanyakazi katika utendaji kazi wa Tume na kujua mwenendo wa utendaji kazi na matumizi ya Tume kwa ujumla na kupunguza uwajibikaji kwa viongozi wa Tume.
Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Bodi ya wakurugenzi
Kila taasisi ya serikali ikiwa ni pamoja na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi katika kutimiza majukumu yake. Naomba ijulikane wazi kuwa kumekuwa na mahusiano yasiyo sawia kati ya Menejimenti ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania inayoongozwa na Brigedia Jenerali Fulgence Msafiri kwa zaidi ya miezi mitano na Bodi ya wakurugenzi ya Tume ambayo imepelekea kutokufanyika kwa vikao vya Bodi ya wakurugenzi tangu kikao cha mwisho kilichokaliwa mwezi Julai 2017. Kwa kawaida vikao vya bodi za wakurugenzi hutanguliwa na vikao vya Baraza la wafanyakazi lakini kikao hiki kilifanyika bila vikao vya Baraza kutokana na mahusiano mabaya kati ya menejimenti ya Tume na uongozi wa chama cha wafanyakazi ambapo Mkurugenzi mkuu amehamisha viongozi wote na kuwafukuza kazi viongozi wa chama cha wafanyakazi katika Tume. Tunaomba wanaohusika kufanya uchunguzi wa mahusiano kati ya Bodi na Menejimenti ya Tume hii ili kuokoa Tume hii iweze kutimiza majukumu yake ya kisheria kwa kulinda, kusimamia matumizi salama ya nguvu za Atomiki Tanzania kwa wagonjwa, wafanyakazi , wananchi na mazingira kwa ujumla.
Uhamisho wa wafanyakazi usio na tija
Ukirejea maelezo ya awali kwenye utangulizi utakumbuka kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu huyu amehamishiwa Tume kuanzia mwezi Septemba 2016. Kuanzia mwezi Novemba 2016 kumekuwa na uhamisho usio wa kawaida na tija kwenye Tume na Taifa, aidha wafanyakazi na wengine kufukuzwa kazi kwa sababu zisizokuwa na msingi wowote. Naomba nitoe mfano wa mkaguzi mkuu wa ndani kuhamishiwa ofisi ya Zanzibar kuwa mhasibu wa kawaida kwa kuhoji na kuibua maovu ya menejimenti hii ya watu watatu. Wafanyakazi wawili waliofukuzwa kazi katika kipindi hiki, Mfanyakazi Mmoja ni dereva ambaye alifukuzwa kazi kwa kosa la kuendesha gari akiwa na leseni iliyokwisha muda wa matumizi bila onyo lolote. Mfanyakazi wa pili ni mhudumu wa ofisi ambaye pia ni Kaimu Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi ambaye alifukuzwa kazi kwa kosa la kupigia simu wafanyakazi wenzake watatu kupitia kwa mhudumu anayeruhusu kupiga simu za nje ya Tume bila onyo lolote, hii ni mifano tu ya wafanyakazi waliofukuzwa kazi mpaka sasa. Ifahamike kuwa Tume hii imekuwa na upungufu wa wafanyakazi kwa miaka mingi tangu kuanzishwa kwake na pia upungufu wa fedha za kufanyia kazi, aidha kwa kipindi mpaka oktoba 2017 Mkurugenzi huyu amehamisha zaidi ya wafanyakazi kumi na tano ndani ya vituo vya kazi vya Tume na wafanyakazi watatu nje ya Taasisi. Hivi sasa Tume ina mradi mkubwa wa ujenzi wa Maabara baada ya kupata msaada wa vifaa vya kisasa kutoka Umoja wa Ulaya (European Union). Pamoja na vifaa hivyo, umoja huo wa ulaya ulitoa mafunzo kwa baadhi ya wafanyakazi wa Tume ili kuboresha usimamizi wa matumizi salama ya nguvu za atomiki, lakini baadhi ya wafanyakazi hao wamehamishiwa nje ya Tume huku uongozi ukidai kuwepo kwa upungufu wa wataalamu katika kutekeleza majukumu yake. Tunaomba pia wanaohusika na usimamizi wa Tume hii kufanya uchunguzi wa tija wa uhamisho huu wa wafanyakazi kwa Tume na Taifa kwa ujumla.
Mambo haya yote yamefanya wafanyakazi wa Tume kufanya kazi katika mazingira magumu na wasiwasi na hivyo kupunguza ufanisi wa kazi zao za kila siku. Bidii za makusudi zifanyike na wahusika pamoja na wizara husika kuiponya Tume hii. Kwa kufanya ukaguzi na uchunguzi wa mambo hayo yapo mambo mengine yanayoweza kujulikana kwa kuwa maamuzi mengi katika Tume yanafanyika kwa maslahi ya kundi dogo la wenye maslahi na maamuzi hayo kuhusu wafanyakazi.
Ufisadi ndani ya Tume ya Nguvu za Atomiki
Baada ya ziara ya Waziri Joyce Ndalichako mapema 2017, gazeti la Habari Leo la 3 Aprili 2017 liliandika “Ndalichako anusa ufisadi tume ya nguvu ya atomiki”. Ikumbukwe kwamba pamoja na mambo yote yaliyotangulia kusemwa hapo juu timu hii hii ya watu watatu imekua ikichukua fedha za serikali na kuzielekeza kwenye mifuko yao binafsi kwenye manunuzi mbalimbali mfamo magari, hongo kwa wageni ,kujinunulia likizo zao bila ulazima wowote, kumtengenezea kaimu mkurugenzi mkuu safari zisizo na tija ikiongozwa na ofisi ya mwanasheria wa Tume na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala ambao ndio maswaiba wa Brigedia Jenerali Fulgency Simon Msafiri. Kitengo cha upimaji wa vyakula ndicho kinaongoza kwa mapato japo ukaribu wa mwanasheria wa Tume na Mkuu wa kitengo cha upimaji wa sampuli za vyakula una ishara ya ufisadi. Vilevile kumuweka mwanadada mchumi ambae hana uwezo kwenye kitengo cha fedha na mipango ili waweze kudhibiti wanapofanya ufujaji. Yapo mambo mengi ambayo tunaamini yakichunguzwa Tume ya Nguvu za Atomiki itakombolewa na kufikia malengo ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda
WAFANYAKAZI TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA
Sehemu ya pili: ===>> Nani atakayeokoa tume ya nguvu za atomiki Tanzania
Sehemu ya tatu: ===>> Nani atakayeokoa tume ya nguvu za atomiki Tanzania
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania ni Taasisi ya serikali iliyoundwa kwa sheria ya Nguvu za Atomiki Na. 7 ya mwaka 2003. Tume hii inayo majukumu makubwa mawili yakiwa ni kusimamia matumizi salama ya vifaa vyote vinavyotoa mionzi ayonisha na isiyoayonisha kwa ajili ya usalama wa wagonjwa, wafanyakazi, wananchi na mazingira kwa ujumla na kuishauri serikali matumizi ya teknolojia ya nyuklia kwenye maeneo mbalimbali kwa ajili ya maendeleo endelevu ya Taifa.
Itakumbukwa kwamba mnamo Juni 2016 Mkurugenzi Mkuu wa Tume hii Prof. Iddi Nyangarika Mkilaha alifariki kwa kujipiga risasi nyumbani kwake jijini Dar es salaam na kufanya Tume kuongozwa na kaimu Mkurugenzi Mkuu aliyekuwa ameteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Tume mpaka Septemba 2016 ambapo Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilipoleta Kaimu Mkurugenzi Mkuu kutoka Jeshi la Wananchi Brigedia Jenerali Fulgence Simon Msafiri kukaimu nafasi hiyo mpaka sasa.
Ijulikane wazi kuwa tangu kupewa nafasi ya kukaimu Mkugenzi huyu Mkuu sasa ni zaidi ya mwaka mmoja kama inavyojieleza hapo juu. Mkurugenzi huyu amekuwa akifanya mabadiliko mbalimbali katika Tume ambayo mengi ya mabadiliko hayo yamekuwa ni kwa manufaa yake binafsi pamoja na baadhi ya viongozi ambao amekuwa akiambatana nao katika kufanya maamuzi ambayo yamekuwa yakiumiza Taasisi pamoja na wafanyakazi na kuwapunguzia morali za kufanya kazi hii ikiwa ni pamoja na kuhamisha wafanyakazi na wengine kuwafukuza kazi bila hata sababu za msingi na kufuata taratibu za utumishi wa umma.
Aidha yapo mambo ambayo wanaohusika na usimamizi wa TUME hii muhimu kwa maendeleo na usalama wa Taifa katika matumizi ya teknolojia ya nyuklia wanatakiwa kuyangalia kwa ukaribu ili kuifanya Tume hii itimize majukumu yake ya msingi katika ofisi zake ambazo ni Arusha Makao Makuu, Dar es salaam, Zanzibar, Mpaka wa Namanga, Mpaka wa Sirali, Ruvuma, Mtwara,Mpaka wa Holili, Mpaka wa Tarakea, Mpaka wa Tunduma, Mpaka wa Rusumo, Mpaka wa mutukula, Mpaka wa Horohoro na Bandari ya Tanga. Ijulikane pia kuwa ukiacha ofisi ya Makao makuu na Ruvuma ofisi zingine zote zinajishughulisha zaidi na usimamizi wa viwango vya mionzi kwenye vyakula vya binadamu na mifungo ambavyo vinaingizwa na kutolewa nje ya nchi ambayo ni sehemu ndogo ya majukumu ya msingi ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania.
Yapo mambo ambayo ni vizuri kuyaonyesha ambayo yanaendelea katika TUME ili wanahusika waweze kuyafanyia kazi kama itapendeza ni kama ifuatavyo
i. Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Wafanyakazi,
ii. Uwepo wa chama cha wafanyakazi na uanachama wa wafanyakazi,
iii. Kutokufanyika kwa vikao vya Baraza la Wafanyakazi,
iv. Fukuza fukuza ya wafanyakazi kwa makosa ya kusingiziwa
v. Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Bodi ya wakurugenzi, na
vi. Uhamisho wa wafanyakazi usio na tija
vii. Ufisadi ndani ya Tume
Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Wafanyakazi
Kumekuwa na mahusiano mabaya na uoga kati ya watumishi wa Tume na timu ndogo ya menejimenti (Kaimu Mkurugenzi mkuu, Mkurugenzi wa utawala na fedha na Mwanasheria wa Tume) na wafanyakazi wengine kwamba wafanyakazi wanatakiwa kufanya lile ambalo hawa wanalitaka liwe vinginevyo utakuwa mhanga katika utumishi wako katika tume hii. Hili limepelekea mpaka hata vikao vya mikutano kati ya wafanyakazi na Menejimenti vimekuwa ni vya maagizo tu na hakuna kutoa mawazo wala kuuliza swali ukifanya hivyo unakuwa unatafuta tatizo katika utumishi wako. Aidha imepelekea hata wageni wa wizara wanapotembelea TUME hii kukosa kujua ukweli wa hali ya TUME maana ripoti za uongo zimekuwa zikitolewa kuwa mahusiano kati utawala na wafanyakazi ni mazuri na akitokea mfanyakazi akauliza swali katika ugeni huo basi atengemee mambo mawili kuhamishwa makao makuu au kufukuzwa kazi. Jambo hili limechangiwa kwa sehemu kubwa na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia hususani Naibu Katibu Mkuu (Sayansi) ambaye kwa sasa ni Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila ambaye alitoa maelekezo yasiyo sahihi kwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu. Tunaomba Wizara iliangalie upya suala hili katika Tume ili kufanya tume ifanye kazi kwa mafanikio na kurejesha morali ya wafanyakazi ya kufanya kazi kwa ufanisi na si kwa vitisho ambavyo vinaendelea ambavyo havina tija kwenye Tume na Taifa kwa ujumla. Tunashauri uchunguzi ufanyike ubaini ukweli wa jambo hili.
Uwepo wa chama cha wafanyakazi na uanachama wa wafanyakazi
Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania ni moja ya Taasisi za utafiti na zinazojishughulisha na mambo ya Sayansi na Teknolojia ikiwepo ukaguzi wa vifaa na majengo yanayotumika vifaa vinavyotoa Mionzi ya Nguvu za Atomiki (geji zinazotumika katika utafiti wa madini na gesi, mashine za uchunguzi na matibabu ya kansa kwa mionzi, mashine za X-ray, mashine za CT na mashine zinazotumika viwandani na katika matengenezo ya barabara ambazo zinatoa mionzi, n.k) hivyo kuifanya wafanyakazi wake kuwa chini ya Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu, Sayansi, Teknolojia, Ufundi Stadi, Habari na Utafiti (RAAWU). Tangu Kaimu Mkurugenzi Mkuu aanze kazi Septemba 2016 amekuwa akifanya kazi ya kuwatoa wafanyakazi kwenye chama cha wafanyakazi kwa kigezo cha kuwapa madaraka ya ukuu wa Idara, Vitengo na Ukurugenzi. Jambo ambalo UTUMISHI kupitia nyaraka mbalimbali lilishatolewa maelekezo katika utekelezaji wako. Hili lilifanya viongozi wa chama cha wafanyakazi Tawi, Mkoa, Kanda na Taifa kumshauri Kaimu Mkurugenzi Mkuu kutokuwatoa wafanyakazi katika chama kwa kuwa ni haki yao ya msingi ila tu pale anapowateua kwa nafasi ya uongozi katika taasisi basi waache nafasi za uongozi katika chama na kutumikia nafasi zao za uteuzi lakini waendelee kuwa wanachama wa chama cha wafanyakazi kwa mujibu wa sheria. Pamoja na ushauri huo Kaimu Mkurugenzi Mkuu hakuwa tayari kubadili msimamo wake wa kuwatoa wafanyakazi kwenye chama jambo ambalo lilifanya aingie kwenye mgogoro na viongozi wa Tawi wa chama cha wafanyakazi kwa kuwahusisha na tuhuma ambazo sio za kweli ikafikia wengine kuwahamisha kutoka kwenye Tume na viongozi wengine kuwaondoa makao makuu na kuwapeleka ofisi za kanda na mipakani kama adhabu. Moja ya viongozi walihamishwa katika Tume ni Katibu wa Chama Tawi ambaye alihamishwa mwezi Aprili 2017. Mahusiano mabaya na chama hayakuishia hapo bali yaliendelea mpaka ilipofika mwezi Oktoba 2017 alimfukuza kazi Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi kwa kosa la kutumia simu ya ofisi kwa mawasiliano na wafanyakazi katika kutimiza majukumu yake ya Chama cha wafanyakazi. Kutokana na unyanyasaji huu kwa viongozi wa chama cha wafanyakazi viongozi wengine wa chama katika Halmashauri ya Chama Tawi waliomba kuachia nafasi zao za uongozi na kubaki wanachama wa kawaida ili kuepusha migongano katika Tume. Mpaka tarehe ya ujumbe huu kuanzia Oktoba 2017 hakuna kiongozi hata mmoja wa chama cha wafanyakazi maana mwenyekiti ndio alibaki ambaye amefukuzwa kazi. Kutokana na mgogoro huo hakujafanyika kikao chochote cha Baraza la Wafanyakazi tangu Aprili 2017 mpaka sasa na nyaraka mbalimbali zimelazimishwa kupitishwa bila ushiriki wa baraza la wafanyakazi. Hili pia wanaohusika na usimamizi wa utendaji wa TUME wanaweza kulifuatilia na kujua ukweli wake.
Kutokufanyika kwa vikao vya Baraza la Wafanyakazi
Kaimu Mkurugenzi Mkuu amekuwa akiendesha Tume bila kuwepo kwa vikao vya mabaraza ya wafanyakazi kutoka mwezi Aprili 2017 alipofanya kikao cha mwisho kwa dakika tatu (3) na kuwalipa wajumbe zaidi ya Ishirini na Tano (25) kila mmoja 150,000/= ambayo kwa upande mmoja yalikuwa ni matumizi mabaya ya fedha ya serikali ila kwa kuwa kulipa au kutokulipa ni maamuzi yake na timu yake hili lilifanyika. Vikao hivyo vya Baraza havijafanyika mpaka sasa ni zaidi ya vikao vitatu kutokana na mgogoro wa kutokutaka chama cha wafanyakazi katika Tume. Hali kadhalika jambo hili linaweza kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kujua ukweli wake na wahusika wenye dhamana ya kusimamia utendaji wa Tume. Ijulikane wazi kwamba kuwa kutokufanyika vikao hivi ni kupunguza ushirikishwaji wa wafanyakazi katika utendaji kazi wa Tume na kujua mwenendo wa utendaji kazi na matumizi ya Tume kwa ujumla na kupunguza uwajibikaji kwa viongozi wa Tume.
Mahusiano ya kiutendaji kati ya Menejimenti na Bodi ya wakurugenzi
Kila taasisi ya serikali ikiwa ni pamoja na Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania inasimamiwa na Bodi ya wakurugenzi katika kutimiza majukumu yake. Naomba ijulikane wazi kuwa kumekuwa na mahusiano yasiyo sawia kati ya Menejimenti ya Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania inayoongozwa na Brigedia Jenerali Fulgence Msafiri kwa zaidi ya miezi mitano na Bodi ya wakurugenzi ya Tume ambayo imepelekea kutokufanyika kwa vikao vya Bodi ya wakurugenzi tangu kikao cha mwisho kilichokaliwa mwezi Julai 2017. Kwa kawaida vikao vya bodi za wakurugenzi hutanguliwa na vikao vya Baraza la wafanyakazi lakini kikao hiki kilifanyika bila vikao vya Baraza kutokana na mahusiano mabaya kati ya menejimenti ya Tume na uongozi wa chama cha wafanyakazi ambapo Mkurugenzi mkuu amehamisha viongozi wote na kuwafukuza kazi viongozi wa chama cha wafanyakazi katika Tume. Tunaomba wanaohusika kufanya uchunguzi wa mahusiano kati ya Bodi na Menejimenti ya Tume hii ili kuokoa Tume hii iweze kutimiza majukumu yake ya kisheria kwa kulinda, kusimamia matumizi salama ya nguvu za Atomiki Tanzania kwa wagonjwa, wafanyakazi , wananchi na mazingira kwa ujumla.
Uhamisho wa wafanyakazi usio na tija
Ukirejea maelezo ya awali kwenye utangulizi utakumbuka kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu huyu amehamishiwa Tume kuanzia mwezi Septemba 2016. Kuanzia mwezi Novemba 2016 kumekuwa na uhamisho usio wa kawaida na tija kwenye Tume na Taifa, aidha wafanyakazi na wengine kufukuzwa kazi kwa sababu zisizokuwa na msingi wowote. Naomba nitoe mfano wa mkaguzi mkuu wa ndani kuhamishiwa ofisi ya Zanzibar kuwa mhasibu wa kawaida kwa kuhoji na kuibua maovu ya menejimenti hii ya watu watatu. Wafanyakazi wawili waliofukuzwa kazi katika kipindi hiki, Mfanyakazi Mmoja ni dereva ambaye alifukuzwa kazi kwa kosa la kuendesha gari akiwa na leseni iliyokwisha muda wa matumizi bila onyo lolote. Mfanyakazi wa pili ni mhudumu wa ofisi ambaye pia ni Kaimu Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi ambaye alifukuzwa kazi kwa kosa la kupigia simu wafanyakazi wenzake watatu kupitia kwa mhudumu anayeruhusu kupiga simu za nje ya Tume bila onyo lolote, hii ni mifano tu ya wafanyakazi waliofukuzwa kazi mpaka sasa. Ifahamike kuwa Tume hii imekuwa na upungufu wa wafanyakazi kwa miaka mingi tangu kuanzishwa kwake na pia upungufu wa fedha za kufanyia kazi, aidha kwa kipindi mpaka oktoba 2017 Mkurugenzi huyu amehamisha zaidi ya wafanyakazi kumi na tano ndani ya vituo vya kazi vya Tume na wafanyakazi watatu nje ya Taasisi. Hivi sasa Tume ina mradi mkubwa wa ujenzi wa Maabara baada ya kupata msaada wa vifaa vya kisasa kutoka Umoja wa Ulaya (European Union). Pamoja na vifaa hivyo, umoja huo wa ulaya ulitoa mafunzo kwa baadhi ya wafanyakazi wa Tume ili kuboresha usimamizi wa matumizi salama ya nguvu za atomiki, lakini baadhi ya wafanyakazi hao wamehamishiwa nje ya Tume huku uongozi ukidai kuwepo kwa upungufu wa wataalamu katika kutekeleza majukumu yake. Tunaomba pia wanaohusika na usimamizi wa Tume hii kufanya uchunguzi wa tija wa uhamisho huu wa wafanyakazi kwa Tume na Taifa kwa ujumla.
Mambo haya yote yamefanya wafanyakazi wa Tume kufanya kazi katika mazingira magumu na wasiwasi na hivyo kupunguza ufanisi wa kazi zao za kila siku. Bidii za makusudi zifanyike na wahusika pamoja na wizara husika kuiponya Tume hii. Kwa kufanya ukaguzi na uchunguzi wa mambo hayo yapo mambo mengine yanayoweza kujulikana kwa kuwa maamuzi mengi katika Tume yanafanyika kwa maslahi ya kundi dogo la wenye maslahi na maamuzi hayo kuhusu wafanyakazi.
Ufisadi ndani ya Tume ya Nguvu za Atomiki
Baada ya ziara ya Waziri Joyce Ndalichako mapema 2017, gazeti la Habari Leo la 3 Aprili 2017 liliandika “Ndalichako anusa ufisadi tume ya nguvu ya atomiki”. Ikumbukwe kwamba pamoja na mambo yote yaliyotangulia kusemwa hapo juu timu hii hii ya watu watatu imekua ikichukua fedha za serikali na kuzielekeza kwenye mifuko yao binafsi kwenye manunuzi mbalimbali mfamo magari, hongo kwa wageni ,kujinunulia likizo zao bila ulazima wowote, kumtengenezea kaimu mkurugenzi mkuu safari zisizo na tija ikiongozwa na ofisi ya mwanasheria wa Tume na Mkurugenzi wa Fedha na Utawala ambao ndio maswaiba wa Brigedia Jenerali Fulgency Simon Msafiri. Kitengo cha upimaji wa vyakula ndicho kinaongoza kwa mapato japo ukaribu wa mwanasheria wa Tume na Mkuu wa kitengo cha upimaji wa sampuli za vyakula una ishara ya ufisadi. Vilevile kumuweka mwanadada mchumi ambae hana uwezo kwenye kitengo cha fedha na mipango ili waweze kudhibiti wanapofanya ufujaji. Yapo mambo mengi ambayo tunaamini yakichunguzwa Tume ya Nguvu za Atomiki itakombolewa na kufikia malengo ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda
WAFANYAKAZI TUME YA NGUVU ZA ATOMIKI TANZANIA
Sehemu ya pili: ===>> Nani atakayeokoa tume ya nguvu za atomiki Tanzania
Sehemu ya tatu: ===>> Nani atakayeokoa tume ya nguvu za atomiki Tanzania