Uchaguzi 2020 Nani atagombea urais kwa tiketi ya CHADEMA?

Mkiti

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
1,013
666
Uchaguzi mkuu wa Tanzania unatarajiwa kufanyika mwaka 2020. Hivi karibuni Tundu Lissu amenukuliwa akisema anakusudia kuomba kupeperusha bendera ya CHADEMA. Ama huko nyuma Edward Lowassa nae alinukuliwa akisema atagombea urais kwa tiketi ya CHADEMA. Ni nani kati ya hao wawili unadhani atateuliwa kupeperusha bendera ya CDM kwenye uchaguzi huo muhimu kwa nchi yetu.
 
Ni ujinga kujadili ni nani atapeperusha wakati vikao rasmi vipo na vitakaa kupitisha atakaye watakao chukuwa fomu wakati huo. Hata mimi natangaza kuwa nakusudia kugombea lakini kama Lissu atachukuwa fomu nitaahirisha dhamira yangu
 
Mh.Mbowe ndio mwenye maamuzi most likely might be Lowassa.Sababu Lissu haijulikani atarejea Bongo,au hata akirudi hatujui bifu zake na serikali kama watamruhusu kuendelea na mambo ya kugombea nafisi yoyote.
 
Mwacheni Lisu na habari za kugombea 2020 naona hamumtakii mema Ndomana nnamwiginza kwenye misukosuko bila yeye kujua jambo la kujipatia umaarufu tu limemfikisha hapo alipo iwe la uraisi au uwenyekiti.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa sasa wanaangalia ni nini Nchi inataka, matatizo yanayolikabili Taifa ni yepi kabla ya kuona ni nani ana sifa na uwezo wa kuyakabili na kutatua. Be patient
 
Uchaguzi mkuu wa Tanzania unatarajiwa kufanyika mwaka 2020. Hivi karibuni Tundu Lissu amenukuliwa akisema anakusudia kuomba kupeperusha bendera ya CHADEMA. Ama huko nyuma Edward Lowassa nae alinukuliwa akisema atagombea urais kwa tiketi ya CHADEMA. Ni nani kati ya hao wawili unadhani atateuliwa kupeperusha bendera ya CDM kwenye uchaguzi huo muhimu kwa nchi yetu.
Mgombea wa urais wa UKAWA ni Zitto Kabwe.......hutaki acha!
 
Uchaguzi mkuu wa Tanzania unatarajiwa kufanyika mwaka 2020. Hivi karibuni Tundu Lissu amenukuliwa akisema anakusudia kuomba kupeperusha bendera ya CHADEMA. Ama huko nyuma Edward Lowassa nae alinukuliwa akisema atagombea urais kwa tiketi ya CHADEMA. Ni nani kati ya hao wawili unadhani atateuliwa kupeperusha bendera ya CDM kwenye uchaguzi huo muhimu kwa nchi yetu.
Mgombea wa urais wa UKAWA ni Zitto Kabwe.......hutaki acha!
 
Ni ujinga kujadili ni nani atapeperusha wakati vikao rasmi vipo na vitakaa kupitisha atakaye watakao chukuwa fomu wakati huo. Hata mimi natangaza kuwa nakusudia kugombea lakini kama Lissu atachukuwa fomu nitaahirisha dhamira yangu
Hivyo vikao vilienda wapi wakati wa Edo vs slaa 2015??
 
Back
Top Bottom