Nani anayesimamia elimu nchini?

Rukiko

Senior Member
May 5, 2009
195
57
Nimekuwa nikijiuliza mara nyingi ni nani hasa anayepaswa kusimamia uendeshwaji wa mashule na elimu hapa Tanzania?
Shule nyingi ni za kata ambazo ndio huhudumia wananchi walio wengi.Lakini kumekuwa hakuna walimu wa kutosha na hata vifaa vya kufundisha pengine hata chaki tu. hata sasa wengi wankwenda kufanya mitihani ya kumaliza shule, ytutegemee nini?

Zipo taasisi nyingi tu ambazo zinakusanya michango kutoka sehemu mbalimbali mf.Mfuko wa kuchangia elimu, hata WAMA n.k ambazo lengo lao eti ni kuinua hali ya elimu Tanzania. Lakini sielewi ni elimu gani inayoendelezwa hapa, au elimu za matumbo yao.

Wapo pia matajiri na wafanyabiashara wanaojidai kuchangia maendeleo ya elimu; lakini nao wanaoenda kuchangia sehemu ambapo wanaweza kulamba mkono.Mfano gazeti la the guardian 18 linamwonyesha mengi akiwa katika sherehe ya kuwaaga wanafunzi wazo hill sekondari, watoto wanaahidiwa milioni moja moja na ma-compyuta, katika shule zenye uwezo-wenyewe wanaiita international(au english medium).
Maswali yangu ni:
1. Ni nani hasa anayesimamia shule zetu za walalahoi, kuanzia primary hadi sekondari ambazo zina watoto wa watanzania weeeengi sana.
2. Kwa nini viongozi wakubwa na wafanyabiashara wanapenda kwenda kwenye shule za matajiri ambazo mimi naamini zinawanyonya tu watanzania wenzetu wanaoenda kusomesha watoto wao huko.
3. Kwa nini wasiajiriwe na kufundishwa walimu wengi wenye sifa wakalpiwa vizuri,katika mashule yetu haya ya kata??tukapunguza watoto wetu kusafiri umbali mrefu kwenda kutafuta shule 'nzuri'
4.Hii michango inayokusanywa kila pembe kuhusiana na elimu inainua elimu ipi na vipi?
5.Ni vipi serikali inasimamia unedeshwaji wa mashule haya yanayojiita ya international, kwani kumekuwa na wimbi la kujipangia bei/karo wanavyotaka tu wao.Ugumu upo wapi kwa serikali kubadili mitaala ya elimu iwe inafundishwa kiingreza tupu-kama ndicho wanachoona bora?
6.Nini mpango wa serikali kuboresha elimu kuanzia chini hadi juu?
7. Kiongozi anayesubiri kualikwa kwenye mashule ya wenye hela anatusaidiaje?
8. Tutegemee nini kwa matokeo ya mitihani ya la saba la form4 kwa mashule yetu yalee??? aaaah Tanzania!!!!
 
hapa+wapi+wadau.jpg


ni nani anayewahurumia hawa??? mbona hawachangiwi vifaa vya elimu, madawati n.k. wizara ya elimu kweli ipo???au mwenye nacho ndo huongezewa??
 
ni nani anayewahurumia hawa??? mbona hawachangiwi vifaa vya elimu, madawati n.k. wizara ya elimu kweli ipo???au mwenye nacho ndo huongezewa??
acha kunitoa machozi Mpwa, kweli unambie hatutahukumiwa mbele ya Haki? Unafikiri future ya hawa ni ipi? Laiti tungeuza shangingi V8 moja tungebadilisha kabisa sura ya darasa hili na mengine kama kumi hivi.....laiti tungeacha safari moja tu ya kwenda Marekani kupokea tuzo ya Nutrition na kufungua NGO tungeweza kuwajengea future yao hawa.....nahisi machozi
 
Serikali ya kifisadi, kila aliye kwenye mfumo ni fisadi, hata tukikuweka wewe kuwa waziri wa elimu katika mfumo huu wa kifisadi you will be induced. Tunachotakiwa kufanya kwaza ni kubadilisha huu mfumo kwa kuingiza mwingine ndipo tutaona mabadiliko. Bado tuna nafasi 2015.
 
Kwani watoto wao wanasoma huko mnakopigia kelele? Tatizo la viongoz we2 licha ya wengi wao kuwa wametokea familia duni miaka hyo, wanasahau past na akishakuwa milionea haamini km kuna wa2 mwaka unaisha hawajashika elfu 20 ya pamoja. Mzee mi nadhani tuwatoe tu hawa mafisadi maana tukianza kujadili uozo wa system nzima unaweza kuvaa mabom na kujilipua ktk mkutano wa campaign wa ccm. Pumbavu zao!
 
Kwani watoto wao wanasoma huko mnakopigia kelele? Tatizo la viongoz we2 licha ya wengi wao kuwa wametokea familia duni miaka hyo, wanasahau past na akishakuwa milionea haamini km kuna wa2 mwaka unaisha hawajashika elfu 20 ya pamoja. Mzee mi nadhani tuwatoe tu hawa mafisadi maana tukianza kujadili uozo wa system nzima unaweza kuvaa mabom na kujilipua ktk mkutano wa campaign wa ccm. Pumbavu zao!


Njia zipi zitumike sasa? (hapo kwenye red) , Kwasababu binafsi naona tatizo la shule kama hizi lipo sana vijijini ambapo ndiko wapiga kura wengi wasio na elimu bora wapo, pia kipindi cha uchaguzi hutumia umaskini wao kuwadanganya kirahisi.
 
matokeo haya ya form form 2012 ni nyongeza ya maswali juu ya maswali tuliyojiuliza zamani kuhusu nani msimamizi wa elimu nchini.Ni nani aliyepaswa kuhakikisha watoto wa shule zetu hasa hizi za walalahoi wanasaidiwa katika kuelewa masomo yao na hata kufaulu mitihani yao. Au aliyenacho ndiye atakayeongezewa?

ukiangalia kwa umakini, hakuna hata mmoja anayesimamia au mwenye moyo wa dhati kabisa kuona tunatoka huku tunasonga mbele.Hapa si serikali kwa maana ya rais ambaye pia huwateua mawaziri kusimamia ukuaji wa elimu nchini. Tunamwona Mulugo na Kawambwa ambao pamoja na kukabidhiwa jukumu hili hawajui waanzie wapi na waishie wapi; wamepwaya sana. Na wanapoelezwa ili wasaidiwe wao huwa wakali na kuwatukana watu, watu wanaona tu, na kama mmoja alivyopendekeza ni kuvuliwa dhamana na kuongoza.

Vile vile hata hizi dini pia hazipo hapo kusaidia mwanafunzi iwe ni kiroho ama kimwili, kwa kuwa wao pia -wapo kwa maslahi yao binafsi. pamoja na kuonekana kuwa shule zao zinafanya vizuri lakini ni kuwa wana pesa za kuendeshea shule; mfano waroman na saint schools zao; pesa ipo, na ndio maana wanaweza kupata vitabu vingi, walimu wazuri na chochote wanachotaka. ila ubaya wao, badala ya kwenda kuwasaidia watanzania huwachagua watanzania wenye nazo kwa maana hata karo zao kwa mtoto mmoja tu kwa mwaka unakuta ni mara mbili ya pato la mtanzania wa chini anayelipwa 80,000 kwa mwezi. lakini bado watoto hawa hubaguliwa ndani kwa wale tu 'cream' yaani vichwa ndio pekee watakaoweza kusoma hapo. kingine ni kuendelea kubaguliwa pia unapoonekana kulegalega katika masomo ili usije ukaiabisha shule yao na kuinyima mapato pale utakapofeli.

kwa hiyo ukiangalia kwa undani wake, sio serikali ama hawa wenye mashule binafsi ambao wako tayari kuona kuwa elimu inakua na watoto wetu wanafaulu vizuri na kuweza sasa hata kushindana na nchi nyingine dunaiani kwa kujiletea maendeleo wenyewe. kama kweli watu wa dini wote wangekuwa wakweli, wangejitahidi sana kwa pesa za sadaka na ushawishi wao kuwasaidia watanzania wote na si wale weney nacho-huu ni unafiki

Tanzania pia tunaongoza kwa kuwa na taasisi nyingi zinazojifanya kushughulikia elimu tanzania, mfano Mfuko wa elimu nchini, NGOs kama WAMA na EQUAL RIGHTs ST Marys na nyingine lakini zote hizi inaonekana kama ni usanii kwa kuwa hii mifuko haisaidii mtanzania yeyote bali hutunisha tu matumbo yao. ujanja hapa ni kuanzisha tu na misaada kibao inamwagika kutoka nje.

Watanzania tusipochukua hatua za dhati kuifufua elimu yetu, watoto wa walio wengi wataendelea kuwa mambumbumbu nakuendela kunyonywa na wachache. Teana huu mtindo wa kuegemea private schools ungeondoshwa kabisa, kwa maana sasa ya kurejesha hadhi ya shule zetu zinazomilikiwa na serikali. mfano mzuri walisema wataregulate ada zinazochajiwa na shule binafsi-miaka inakatika tu hakuna lolote; kumbe wale wanaotaka kuregulate ndio wamiliki wa shule hizo...Mambo ni mengi, bado nauliza ni nani anatakiwa kusimamia, ama nini kifanyike aibu hizi zisiendelee kutukumba huku tukipoteza rasmali- watu kubwa namna katika lindi kubwa la umaskni?nawasilisha
 
Back
Top Bottom