Ndahani
Platinum Member
- Jun 3, 2008
- 18,119
- 9,049
Mimi sijaona chuki ya Ole Mushi dhidi ya Polepole...
Mimi sijaona akimhukumu Polepole (he's not judgemental) Mwanga Mkali
Kwa msomaji makini wa hoja ya Ole Mushi, atagundua kuwa andiko lake lote limlenga kumpa changamoto ya kuboresha zaidi shule yake ya uongozi..
Ndiyo maana katumia reference ya China na Prof. Zhang WeiWei namna wanavyopata viongozi wao...
Ole Thadei Mushi, amesema hili akitambua kuwa Humphrey Polepole ni mwana CCM aliyewahi kushika nafasi nyeti chamani na bado anazo zingine na pia ni mbunge na kwa hiyo anaweza kulichukua wazo hili na kulipeleka kwa wenzake...
Mimi sijaona kosa la Mwandishi hata astahili kushambuliwa kwa kiasi hiki...
Kwenye hii jamii yetu ya sasa, nani anayetaka muundo wa kusoma ili wale wenye kustahili ndio wawe viongozi?
Hata kama ukiwekwa watu watavujisha mitihani.