Nani anaweza kuwa CDF mpya wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama?

ESCORT 1

JF-Expert Member
Dec 7, 2015
1,267
2,519
Kufatia habari ya jana ya kustaafu kwa General Mabeyo ndani ya JWTZ, basi kama kawaida yetu sio mbaya tukafanya bashiri ya nani anaweza akawa CDF mpya.

Kwakuwa JF ni uwanja mpana, ina wadau wengi na wengine ni wa huko huko jikoni, sio mbaya tukapendekeza jina la CDF mpya kwa kuzingatia uweledi wake katika kuchapa kazi.

Mimi nampa nafasi kubwa Luteni Jenerali Mathew Mkingule kuwa CDF mpya.

Lakini pia kwenye korido anatajwa Luteni Jenerali Yakubu Mohamed balozi wa Tanzania nchini Uturuki.

Japo pia mzee wa infantry, Meja Jenerali Mwaisaka anapigiwa chapuo.

Vilevile, Meja Jenerali Rajab Mabele naye anaweza akawa CDF mzuri tu kwa utendaji wake mzuri wa kazi huko JKT.

Japo pia kuna minong'ono kuhusu Meja Jenerali Suleimani Mzee kufatia kazi ya kutukuka huko Magereza.

Ila watu wasimua-underrate Meja Jenerali Mbuge lolote linaweza kutokea. Japo kwasasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Brigedia Jenerali J.J. Mwaseba mkuu wa chuo cha TMA naye anatajwa japo atakuwa yupo nyuma sana kwa rank kulinganisha na hao wenzake.

NB:
Uzi huu haumlengi kumpigia mtu yoyote promo!!

Viva JWTZ
Viva Tanzania
 
Anafuatia Brigedia General Marco Elisha Gaguti
1654670150987.png
 
Kwa sisi tuliopitia JKT enzi hizo tunajua nafasi itaenda kwa Lt Gen. Mkingule ambaye ni C of S.... swali sasa ni nani atakua C of S baada ya Mkingule kua CDF jibu ni ngumu kidogo ila kuna Maj Gen. kibao ila wawili likely mmoja kutoka kanda ya ziwa na mwingine kutoka upande wa pili
 
Back
Top Bottom