Nani anawadanganya pesa ndio kila kitu?

Unaweza kuwa na pesa alafu ukawa na kisukari au shinikizo la damu, vyakula vizuri kama burger, keki, pizza utakula kwa macho.

Viatu vikali utashindwa kuvaa ukiogopa kuchubuka na kupata vidonda mguu ukatwe,utashinda na yebo yebo kutwa nzima mpaka ofisini.

Ukiumwa na chochote Malaria, Ukimwi nk mate yanakuwa machungu, hamu ya kula inapotea hata biriani utaliona chungu.

Ukiendekeza kubana na kutafuta hela ukajisahau utaishia kupata vidonda vya tumbo.

Ishu hapa sio kutokula, tatizo ni kula ili mradi umekula siku ipite au kutokula kabisa usave hela utajirike.

Chanzo cha magonjwa mengi kama kisukari na shinikizo la damu ni kuishi maisha yasio na mpangilio katika ulaji, unakula ili mradi umekula unathamini pesa kuliko afya.

Kwa maisha hayo, matokeo yake wengi wetu hujikuta tumeshapata magonjwa hayo wakati pesa ndio zimeingia, unaishia kusikitika huwezi kuzitumia.

Linda afya yako kwenye harakati zako za kutafuta pesa. Afya ndio kila kitu.
Huu uzi unanuka umasikini.
 
Pesa haijawahi kukosa matumizi ndugu kama inashindikana kula vitamu, unashindwaje kuajiri mabaunsa, kumuita King Kiba aimbe, unashindwaje kuwadhamini Yanga, kwenda Dubai kuzurura, kama naumwa basi nitakodi helicopter nikatundikiwe dripu angani
 
Ukipita vijijini kule unaweza kulia; unakuta mtu ana magonjwa, pesa hana na hata nguvu za kulima au kufanya kazi hana. Life zima ni IMPOSSIBLE lakini tajiri hata akiumwa bado anaweza afford hospitali nzuri na huduma yoyote anayoitaka.

Ila maisha bana ni kitendawili. Steve Jobs wa Apple pamoja na hela zote kafa na miaka 50 wakati kuna wazee wako huko vijijini hawajui hata kesho watakula nini, hawana huduma za afya, nk na wanaishi miaka 90+
 
Ila maisha bana ni kitendawili. Steve Jobs wa Apple pamoja na hela zote kafa na miaka 50 wakati kuna wazee wako huko vijijini hawajui hata kesho watakula nini, hawana huduma za afya, nk na wanaishi miaka 90+

Wewe ungepewa choice uishi miaka 50 ya raha au 90+ ya shida ungechagua nini 😆😆😆???..
 
Pesa ndo kila kitu mjomba.
ila kikubwa afya njema.
Usipokuwa na hela una dharaurika sanaa mbele ya ndugu hata jamii.
tafuta hela acha kujifariji
 
Ukipita vijijini kule unaweza kulia; unakuta mtu ana magonjwa, pesa hana na hata nguvu za kulima au kufanya kazi hana. Life zima ni IMPOSSIBLE lakini tajiri hata akiumwa bado anaweza afford hospitali nzuri na huduma yoyote anayoitaka.
Sahihi kabisa.
 
Back
Top Bottom