Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,001
- 112,647
Juzi wakati Rais Samia alipotembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete [siyo ule moyo wa Kikwete 🤣 uliopo ndani ya kidari chake], alisema kuwa alifarijika kusikia kwamba miongoni mwa wagonjwa wanaoenda hapo kutibiwa, wanatoka nchi za jirani na hata Marekani.
Hapo kwenye Marekani alisema kwa mshangao na msisitizo.
Haya hapa kwenye video maneno aliyoyasema. Anzia dakika ya 12:49 hadi 13:10.
Isije wakawa wamemlisha matango pori huyo mama!
Nani atoke Marekani aje Tanzania kutibiwa ugonjwa wa moyo?
Labda ni awe au wawe Wamarekani ambao tayari walikuwepo Tanzania [kwa sababu yoyote ile] halafu wakapatwa na matatizo ya moyo ndo wakapelekwa hapo kupata matibabu.
Ila mtu atoke Marekani na matatizo yake ya moyo aje Tanzania kwa ajili ya kupata matibabu hapo kwenye hiyo taasisi?
Ngumu kuamini….
Hapo kwenye Marekani alisema kwa mshangao na msisitizo.
Haya hapa kwenye video maneno aliyoyasema. Anzia dakika ya 12:49 hadi 13:10.
Isije wakawa wamemlisha matango pori huyo mama!
Nani atoke Marekani aje Tanzania kutibiwa ugonjwa wa moyo?
Labda ni awe au wawe Wamarekani ambao tayari walikuwepo Tanzania [kwa sababu yoyote ile] halafu wakapatwa na matatizo ya moyo ndo wakapelekwa hapo kupata matibabu.
Ila mtu atoke Marekani na matatizo yake ya moyo aje Tanzania kwa ajili ya kupata matibabu hapo kwenye hiyo taasisi?
Ngumu kuamini….