Nani anastahili tuzo ya Nobel katika marais 6 tuliowahi kuwa nao Tanzania?

Tuzo za za Nobel ziko sita, unaongelea tuzo gani ya Nobel?

1.Ya Amani?
2.Ya Fasihi?
3.Ya Biolojia/madawa?
4. Ya Physics ?
5. Ya Kemia?
6. Ya Sayansi ya Uchumi?
Wana JF,
Mimi nafikiri pale tutakapotambua umuhimu wa Sayansi na Teknolojia na kuvitengea bajeti nono ili kuibua na kukuza ubunifu ndipo kama taifa tuanze kuota ndoto ya tuzo hii kutinga Tz, otherwise kama Mtanzania akitokea kuipata basi lazima atakuwa Mwanadiaspora au aliye naturalize nje ya Tz. Hapa Tz siasa inachukuwa rasilimalifedha na rasilimaliwatu wengi kuliko maelezo. Leo hii Wahandisi wabobezi wanahamia kwenye siasa, Madaktari bingwa wanahamia kwenye siasa, Wachumi nguli wanakimbilia siasa, Wakulima mahiri wanaishia kwenye siasa, Maaskari waandamizi wanahamia kwenye siasa (Leo hii Pensheni ya Mwalimu wa Shule ya Msingi aliyestaafu 30.06.1997 kwa hiari katika umri wa miaka 55 inalingana kabisa na Pensheni ya Brigadier General). Tz imewekeza muda, rasilimaliwatu na rasilimalifedha kwa kiwango kikubwa kwenye Siasa kuliko kwenye Sayansi na Teknolojia, tuzo itapatikanaje? Ukiangalia hata kwenye Mifuko ya Pensheni wakati haijaunganishwa kuwa mbili tu, tulikuwa na Mifuko takriban 12 na kila moja ilianzishwa kwa sheria ya Bunge (Act of Parliament) kwamba walikuwa hawataki kuwa wamoja, lakini katika hiyo 12 ni Mfuko wa Pensheni ya Wanasiasa ndiyo ulikuwa unalipa Pensheni nono sana kuliko Mifuko yote, hii ilifanya wataalam ambao wangetuletea Tuzo ya Nobel kutelekeza taaluma na career zao kukimbilia siasa ili wawe wanachama wa Mfuko huo ili wanapostaafu wawe na Pensheni nono.
 
Tuzo za za Nobel ziko sita, unaongelea tuzo gani ya Nobel?

1.Ya Amani?
2.Ya Fasihi?
3.Ya Biolojia/madawa?
4. Ya Physics ?
5. Ya Kemia?
6. Ya Sayansi ya Uchumi?

1: Ya Amani, nyoko nn

Hujui kazuia na kumuadabisha Gaidi kuleta madhara makubwa nchini, isingekuwa hivyo leo Amani ingekuwa mashakani sana, Gaidi hatari sana kwa amani yetu.
 
Kaunda aliposhindwa alikabidhi madaraka kwa Chiluba, Banda aliposhindwa alikabidhi madaraka kwa Michael Satta, unafikiri Lungu alikuwa na ubavu gani wa kukataa kukabidhi madaraka kwa Hichilema??
Na Levy Mwanawasa, ila Zambia nayo ni shule moja nzuri sana ya demokrasia duniani kama siyo Afrika.
 
Recipients’ countries and their number of prizes:

S.N.CountryNumber of Nobel Prizes
1.United States of America380
2.United Kingdom132
3.Germany102
4.France69
5.Sweden32
6.Russia/ Soviet Union31
7.Switzerland28
8.Japan28
9.Canada27
10.Austria22
11.Netherlands21
12.Italy20
13Israel12
Between 1901 and 2019, the Nobel Prizes and the Prize in Economic Sciences were awarded 597 times.

Israel has more Nobel Prizes per capita than the United States, France and Germany.

Source: jagranjosh.com
 
Wana JF,
Mimi nafikiri pale tutakapotambua umuhimu wa Sayansi na Teknolojia na kuvitengea bajeti nono ili kuibua na kukuza ubunifu ndipo kama taifa tuanze kuota ndoto ya tuzo hii kutinga Tz, otherwise kama Mtanzania akitokea kuipata basi lazima atakuwa Mwanadiaspora au aliye naturalize nje ya Tz. Hapa Tz siasa inachukuwa rasilimalifedha na rasilimaliwatu wengi kuliko maelezo. Leo hii Wahandisi wabobezi wanahamia kwenye siasa, Madaktari bingwa wanahamia kwenye siasa, Wachumi nguli wanakimbilia siasa, Wakulima mahiri wanaishia kwenye siasa, Maaskari waandamizi wanahamia kwenye siasa (Leo hii Pensheni ya Mwalimu wa Shule ya Msingi aliyestaafu 30.06.1997 kwa hiari katika umri wa miaka 55 inalingana kabisa na Pensheni ya Brigadier General). Tz imewekeza muda, rasilimaliwatu na rasilimalifedha kwa kiwango kikubwa kwenye Siasa kuliko kwenye Sayansi na Teknolojia, tuzo itapatikanaje? Ukiangalia hata kwenye Mifuko ya Pensheni wakati haijaunganishwa kuwa mbili tu, tulikuwa na Mifuko takriban 12 na kila moja ilianzishwa kwa sheria ya Bunge (Act of Parliament) kwamba walikuwa hawataki kuwa wamoja, lakini katika hiyo 12 ni Mfuko wa Pensheni ya Wanasiasa ndiyo ulikuwa unalipa Pensheni nono sana kuliko Mifuko yote, hii ilifanya wataalam ambao wangetuletea Tuzo ya Nobel kutelekeza taaluma na career zao kukimbilia siasa ili wawe wanachama wa Mfuko huo ili wanapostaafu wawe na Pensheni nono.

Liberation ya kusini Mwa Afrika ni kazi y maana sana aliyoifanya Nyerere

Kuipatia uhuru Tanganyika bila kumwaga damu

Na kusaidia kuondoa umwagaji damu Zanzibar kwa kuiunganisha na Tanganyika
Kisichoona macho ya dunia hii ni kwamba, vitabu vya Mwl Nyerere vya:-
1. Man and Development
2. Ujamaa-Essays on Socialism
3. Nyerere on Socialsim
4. Freedom and Unity
vinatumika kuipaisha China kimaendeleo kuliko vinavyotumika kuipaisha Tz kimaendeleo. Wachina wameamua kuvitafsiri kwa lugha ya kwao na vimekuwa Best Sellers. Ikumbukwe Wachina ni 1.4bl sawa na 18% ya idadi ya watu duniani hivyo ni soko kubwa la vitabu hivyo. Wamegundua mawazo ya Mwl. Nyerere ni lulu iliyolala na karama iliyokosa mchochezi wake. Wachina wanaamini kwamba siyo tu ubepari ndiyo unaoweza kuendeleza jamii, hata Ukomunist na Ujamaa pia. Chama Cha Kikomunisti cha China CPC kimeamua kuwekeza kwenye mawazo ya Mwl. Nyerere. Tz tumelogwa na nani?
 
Labda Kambarage na juhudi zake za ukombozi wa bara la Afrika, wengine waliobaki hamna kitu...
 
Vigezo unavyotumia wewe na jinsi unavyovitafsisri siyo ambavyo MO inavyotumia. Magufuli asingewza kuwemo kwenye Nobel kwa vile hakuwa na impact pana zaidi ya nyumbani ingawa aliongelewa sana kimataifa. Impact ya Nyerere ilisikika Afrika yote; Kikwete yeye alikuwa mla nchi tu, hakuwa na impact yoyote popote pale. Hakuna nchi yoyote duniani utakakokuta watu wanamuongelea Kikwete au kitu chochote cha kumbukumbu ya Kikwete. Nyerere anakumbukuwa sehemu nyingi sana Afrika, hata sehemu usizoaomini kama Mali wana mtaa unaitwa Nyerere, na Magufuli anajulikana dunia nzima.
Uko sahihi, ila kwa Jiwe tulikosea pakubwa, bila Mungu kuingilia kati sijui tungekuwa wapi.
 
Mbona nchi nyingi sana Africa zilipata Uhuru bila kumwaga damu. Wakoloni Waingereza hawakuwa na taabu sana kuachia makoloni yao bila vita kwa watawala wazawa.
Liberation ya kusini Mwa Afrika ni kazi y maana sana aliyoifanya Nyerere

Kuipatia uhuru Tanganyika bila kumwaga damu

Na kusaidia kuondoa umwagaji damu Zanzibar kwa kuiunganisha na Tanganyika
 
Hiyo tuzo wampe Mzee Mwinyi.

Kuna siku nilimuona huyu Mzee akipita mtaani kiwa kwenye gari bila hata kuwa na Mlinzi, Wamachinga wakamshangilia Mzee Ruksaaaaa! Ilinipa faraja sana maana amemaliza muda wake wa uongozi huku akiwaacha watu wakiishi kwa amani, furaha na upendo.
 
Kisichoona macho ya dunia hii ni kwamba, vitabu vya Mwl Nyerere vya:-
1. Man and Development
2. Ujamaa-Essays on Socialism
3. Nyerere on Socialsim
4. Freedom and Unity
vinatumika kuipaisha China kimaendeleo kuliko vinavyotumika kuipaisha Tz kimaendeleo. Wachina wameamua kuvitafsiri kwa lugha ya kwao na vimekuwa Best Sellers. Ikumbukwe Wachina ni 1.4bl sawa na 18% ya idadi ya watu duniani hivyo ni soko kubwa la vitabu hivyo. Wamegundua mawazo ya Mwl. Nyerere ni lulu iliyolala na karama iliyokosa mchochezi wake. Wachina wanaamini kwamba siyo tu ubepari ndiyo unaoweza kuendeleza jamii, hata Ukomunist na Ujamaa pia. Chama Cha Kikomunisti cha China CPC kimeamua kuwekeza kwenye mawazo ya Mwl. Nyerere. Tz tumelogwa na nani?
Kesho tu hapa tutakuja kustuka Korea Kaskazini nayo imefuata nyayo za CPC kwa kuwekeza kwenye mawazo ya Mwl. Nyerere. Kwa kweli Nyerere anaendelea kuishi hata baada ya kufa, natamani hiyo tuzo ya Nobel wangefanya special consideration wakampa hata Mama Maria Nyerere kwa niaba au hata wakaipa JMT, au hata Nyerere Foundation ili hizo fedha ziende zikasaidie jamii.
 
Vigezo unavyotumia wewe na jinsi unavyovitafsisri siyo ambavyo MO inavyotumia. Magufuli asingewza kuwemo kwenye Nobel kwa vile hakuwa na impact pana zaidi ya nyumbani ingawa aliongelewa sana kimataifa. Impact ya Nyerere ilisikika Afrika yote; Kikwete yeye alikuwa mla nchi tu, hakuwa na impact yoyote popote pale. Hakuna nchi yoyote duniani utakakokuta watu wanamuongelea Kikwete au kitu chochote cha kumbukumbu ya Kikwete. Nyerere anakumbukuwa sehemu nyingi sana Afrika, hata sehemu usizoaomini kama Mali wana mtaa unaitwa Nyerere, na Magufuli anajulikana dunia nzima.
Hapa umeonyesha chuki zako kwa Kikwete bila hoja za msingi

1. Kikwete alisaidia kuleta Amani Comoro kwa kumpiga yule Kanali Muasi aitwaye Bacar

2. Alisaidia kuleta amani kongo kwa kuwapiga M23

3. Alisaidia kusuluhisha Kenya, pale walipotaka kuingia kwenye civil war baada ya uchaguzi wa 2008

Soma hii paper:


4. alisaidia kusuluhisha Madagascar

5. Alisaidia kutuliza joto burundi, baada ya Jaribio la Mapinduzi dhidi ya Nkrunzinza, Kikwete alisaidia sana kuzima jaribio lile la mapinduzi na hivyo kusaidia ile nchi isiingie ktk civil war

Kwa hiyo hoja yako eti Kikwete hakufanya chochote si kweli
 
Hiyo tuzo wampe Mzee Mwinyi.

Kuna siku nilimuona huyu Mzee akipita mtaani kiwa kwenye gari bila hata kuwa na Mlinzi, Wamachinga wakamshangilia Mzee Ruksaaaaa! Ilinipa faraja sana maana amemaliza muda wake wa uongozi huku akiwaacha watu wakiishi kwa amani, furaha na upendo.
Mkuu, vipi uchumi ulikaaje? Vile viwanda alivyoacha Mwl kwa mamia viliendelea kuwepo? Pengo kati ya utajiri na umaskini lilikuwaje? Akiba ya fedha za kigeni 1995 ilikaaje? Migogoro ya ardhi (vita vya wakulima na wafugaji) hali ilikuwaje? Makusanyo ya kodi yalikuwaje? GDP ilikuwaje? Nobel inatolewa kwa Sayansi ya Uchumi pia, je, uchumi wa Tz ulikuwa jumuishi? Hali ya chakula ilikuwaje kitaifa? Deni la taifa lilikuwaje? nk nk, tupe maarifa mkuu.
 
Back
Top Bottom