Nani anamuelewa huyu msanii Grand P?

Naimani mko buheri marafiki,

Naomba mwenye kuweza kuweka CV au taarifa za kina zitazofanya sisi wengine wa ukanda wa Afrika mashariki huku tumjue huyu bwana.Jamaa namfahamu kama msanii mwenye pesa ndefu sana na anaekubalika sanaa huko GUINEA sababu huwa naona huko u-tube anavyotrend kwa views nyingi na anavyoshobokewa na masister wa huko pia anaheshimika sana kwa ujumla wake.

Nimejaribu kufuatilia nyimbo zake huko u tube kiukweli sijaona anachovutia kabisa huyu bwana kuanzia sauti yake.Hata kucheza kwake jamaa anaenda vice versa na beat.ila vibe analopata si la Afrika.

Mwenye kumjua zaidi kwa kilicho chini ya uvungu kuhusu mafanikio ya huyu bwana aweke hapa sbb mi sjaona Cha maana.View attachment 1931823View attachment 1931824
Kuna uzi uliletwa na Kasomi umemuelezea vyema Historia yake yote.
 
Gran P (Sio Grand P) ni msanii wa muziki huko Guinea, mwenye mafanikio sana kupitia kipaji chake cha muziki.

Msanii huu alizaliwa kiwa na ulemavu kama anavyoonekana ni ule ulemavu wa mtu kuonekana na umri mkubwa kuliko umbile lake.

Alikuwa msanii tokea kitambo, ila alipata umaarufu zaidi nchi za nje na mitandaoni (Haswa instagram) pale alipoanzisha uhusiano na mwanadada (Euxodie Yao ) mrefu na mwenye umbo kubwa kuliko yeye, mwanadada huyo aliyetokea nchi jirani na Guinea , nchi ya Ivory coast.
Ni Grand P siyo Gran P.

Soma zaidi
Mfahamu Grand P, Msanii mwenye mvuto wa aina yake
 
Mwanaume shujaa Africa magharibi na kati.....

 
Hii dunia ya mwisho yale mambo ya kijinga ndio watu wanapenda mambo ya kishetani ndio hasa wanapenda ,wajinga hawakusoma ,waimbaji ,wacheza mipira ,waigizaji , watu waongo pamoja na wanasiasa uchawara ndio wanaendesha dunia .Wasomi ,watu makini na yote mazuri leo hayana nafasi tena ktk ulimwengu mambo yamekuwa vise varsa ,uongo ndio ukweli na ukweli ndio uongo.Dunia ya mwisho.
 
Nilijua ni alien kumbe ni kamtu fulani kana utajiri, mara ya Kwanza nilikaona kwenye kipindi cha Churchill show cha NTV Kenya nikashangaa sana kanavyo rapu arafu kamevaa bonge la cheni, raba, tisheti karibia inafika magotini!!!
 
Gran P (Sio Grand P) ni msanii wa muziki huko Guinea, mwenye mafanikio sana kupitia kipaji chake cha muziki.

Msanii huu alizaliwa kiwa na ulemavu kama anavyoonekana ni ule ulemavu wa mtu kuonekana na umri mkubwa kuliko umbile lake.

Alikuwa msanii tokea kitambo, ila alipata umaarufu zaidi nchi za nje na mitandaoni (Haswa instagram) pale alipoanzisha uhusiano na mwanadada (Euxodie Yao ) mrefu na mwenye umbo kubwa kuliko yeye, mwanadada huyo aliyetokea nchi jirani na Guinea , nchi ya Ivory coast.
Mimi sidhani kama Grand P (siyo Gran P) ana ugonjwa wa progeria kwakua mwenye progeria kuvuka miaka 18 ni ishu.

Huu ugonjwa unafanya uonekane umezeeka na pia unafanya hata viungo na organs zako ziende kwa rate hiyo hiyo ya kuzeeka. Hivyo by 18 moyo, figo, ini n.k vyote vinakua vya mtu aliyezeeka ndiyo maana inakua ngumu kuishi muda mrefu.

Ila Grand P inaripotiwa is more than twenty something na hapo ndipo naona ama hana progeria au ana progeria ila bado ni mdogo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom