Nani analipia gharama za urushwaji wa Matangazo ya Moja kwa Moja (LIVE) kwa Vyombo Binafsi vya Habari?

WINGER_TEREZA

JF-Expert Member
Jul 31, 2015
242
450
Ndugu wanajukwaa salam, ama baada ya salam, niende moja kwa moja kwenye mada.

Niliwahi kusikia kurusha matangazo ya LIVE kwa nusu ni shilingi 4 million kunako TV (Japo sina uhakika kuhusu hiyo bei - ila point ya msingi ni kurusha matangazo LIVE via TV kwa saa ni gharama).

Sote tunafahamu vyobo vya habari vya serikali TBC na vya chama (Channel 10, Magic FM na Uhuru FM - CCM) vinapewa ruzuku kufanya hizo kazi za "kuiiongelea Serikali".

Lakini, hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa kwa vyombo vya habari visivyo vya serikali kama AZAM MEDIA ( Azam tv na U-fm), WASAFI MEDIA (Wasafi fm na Wasafi Tv), CLOUDS MEDIA (Clouds FM and Clouds TV) na IPP MEDIA (EATV, EA Radio, ITV, Radio One, Capital Radio) na vinginevyo, kujihusishwa na urushaji wa matangazo mubarashara ya shughuli za chama (CCM) na serikali hasa Raisi akiwa katika ziara zake huko mikoani.

Pia, sasa hivi katika maombolezo ya Msiba wa Hayati Benjamin Mkapa pia naona nao wako mstari wa mbele katika kutoa matangazo ya huu msiba tena LIVE kwa siku kama ya nne mfululizo sasa.

Swali langu ni je, ni nani anagharamia hizo gharama kubwa na kufanya coverage za hizo LIVE? Na vipi mboona hakuna chombo hata kimoja cha habari kinarusha LIVE shughuli za wapinzani huko kwenye mikutano yao mikuu ya vyama vyao ya kupitisha wagombea wao hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi?
 
Ndugu wanajukwaa salam, ama baada ya salam, niende moja kwa moja kwenye mada.

Niliwahi kusikia kurusha matangazo ya LIVE kwa nusu ni shilingi 4 million kunako TV (Japo sina uhakika kuhusu hiyo bei - ila point ya msingi ni kurusha matangazo LIVE via TV kwa saa ni gharama).

Sote tunafahamu vyobo vya habari vya serikali TBC na vya chama (Channel 10, Magic FM na Uhuru FM - CCM) vinapewa ruzuku kufanya hizo kazi za "kuiiongelea Serikali".

Lakini, hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa kwa vyombo vya habari visivyo vya serikali kama AZAM MEDIA ( Azam tv na U-fm), WASAFI MEDIA (Wasafi fm na Wasafi Tv), CLOUDS MEDIA (Clouds FM and Clouds TV) na IPP MEDIA (EATV, EA Radio, ITV, Radio One, Capital Radio) na vinginevyo, kujihusishwa na urushaji wa matangazo mubarashara ya shughuli za chama (CCM) na serikali hasa Raisi akiwa katika ziara zake huko mikoani.

Pia, sasa hivi katika maombolezo ya Msiba wa Hayati Benjamin Mkapa pia naona nao wako mstari wa mbele katika kutoa matangazo ya huu msiba tena LIVE kwa siku kama ya nne mfululizo sasa.

Swali langu ni je, ni nani anagharamia hizo gharama kubwa na kufanya coverage za hizo LIVE? Na vipi mboona hakuna chombo hata kimoja cha habari kinarusha LIVE shughuli za wapinzani huko kwenye mikutano yao mikuu ya vyama vyao ya kupitisha wagombea wao hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi?

Jibu zuri kwa swali lako nina uhakika analo Pascal Mayalla
 
Unalinganisha msiba wa rais mstaafu na vijimkutano vya vyama vya siasa tena vya upinzani???
Think twice!
Tunaongelea mkutano wa CCM ambao nadhani ulikuwa siku tatu au kuapishwa kwa kila siku DED, DC, RC na makatibu tawala
 
Mkuu naomba nieleweshe hizo gharama huwa zinatoka wapi ikiwa vifaa vyote ni vyao na studio ni yao ,wafanyakazi wao
 
Inaweza kuwa bure bwerere kabisa. Hii inaitwa "giving back to the community..":D
 
Mbona hawajitolei kwa shughuli za upinzani kwa mfano ujio wa Lissu juzi mbona hata chombo kimoja hakikuonesha, au mkutano wa mkuu wa CUF na ATA-TADEA
Tukio lisilo na mashiko hawapotezi muda wao.

Pia naona mmejazana mitandaoni mkilazimisha hiyari za vyombo vya habari viwatangazie utopolo wenu.

Mbeleko imekatika
 
Back
Top Bottom