trachomatis
JF-Expert Member
- Jun 7, 2011
- 3,758
- 736
Tandahimba ni jimbo la uchaguzi na pia ni wilaya katika mkoa wa Mtwara. Population ni 240,000 hivi.Kielimu iko nyuma kama maeneo mengine ya kusini yalivyo.Si ajabu mtu wa miaka 30 hadi 40 asiyejua kusoma. Misimu ni miwili tu mvua na jua.
Umeme ukikatika maji ya bomba hayapatikani. Ila umeme hukatika kwa nadra sana kwa kuwa unatumika wa gesi ya Mnazi Bay. Korosho ndiyo tegemeo kubwa kwa uchumi wa wilaya hii.
Halmashauri ya Tandahimba inashindana na Mji /Manispaa kama Ilala kwa mapato! Mfano mwaka wa fedha uliopita takribani bilioni 55 zilipatikana..! Ili kufika Tandahimba inakubidi ufike Mtwara na kufuata barabara ya changarawe kwa urefu km 96.Kipindi cha mvua na baada ya kipindi hicho kunakuwa na mahandaki ya kutisha sana barabarani.
Tangu kufariki Mh Nandonde (mbunge maarufu sana enzi hizo wa Tandahimba) hili jimbo mbunge hufikisha kipindi kimoja tu cha miaka mitano! 2010 ndiyo imevunja rekodi,Mh Juma Njwayo alishinda kwa tabu sana mchujo wa chama chake hadi kupelekea wengi kwenye chama chake kutompenda. ''Alimshinda'' mgombea kijana wa CUF Ahmad Katani.
Tuache mengine yote,lakini kinachonifanya niweke hii thread ni sera moja ya CDM. Kwamba maeneo yenye uwezo kiuchumi yaboreshwe kwanza yenyewe na kwa utaratibu maalum maeneo yasiyozalisha ndipo yaje kupewa mgawo.
Karibuni wana JF kuchangia lolote katika maelez yoyote hapo juu.
Umeme ukikatika maji ya bomba hayapatikani. Ila umeme hukatika kwa nadra sana kwa kuwa unatumika wa gesi ya Mnazi Bay. Korosho ndiyo tegemeo kubwa kwa uchumi wa wilaya hii.
Halmashauri ya Tandahimba inashindana na Mji /Manispaa kama Ilala kwa mapato! Mfano mwaka wa fedha uliopita takribani bilioni 55 zilipatikana..! Ili kufika Tandahimba inakubidi ufike Mtwara na kufuata barabara ya changarawe kwa urefu km 96.Kipindi cha mvua na baada ya kipindi hicho kunakuwa na mahandaki ya kutisha sana barabarani.
Tangu kufariki Mh Nandonde (mbunge maarufu sana enzi hizo wa Tandahimba) hili jimbo mbunge hufikisha kipindi kimoja tu cha miaka mitano! 2010 ndiyo imevunja rekodi,Mh Juma Njwayo alishinda kwa tabu sana mchujo wa chama chake hadi kupelekea wengi kwenye chama chake kutompenda. ''Alimshinda'' mgombea kijana wa CUF Ahmad Katani.
Tuache mengine yote,lakini kinachonifanya niweke hii thread ni sera moja ya CDM. Kwamba maeneo yenye uwezo kiuchumi yaboreshwe kwanza yenyewe na kwa utaratibu maalum maeneo yasiyozalisha ndipo yaje kupewa mgawo.
Karibuni wana JF kuchangia lolote katika maelez yoyote hapo juu.