Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,113
- 33,623
Vyama vikubwa vya siasa hapa nchini CHADEMA na CCM kwa nyakati tofauti huwa vinaonesha kwamba vinachukia sana ufisadi. Lakini kila wakati vyama hivi vimekuwa vikitupiana mpira kuhusu kutamalaki kwa ufisadi kwenye nchi yetu.
CCM huwa inawashutumu CHADEMA kuwa kuwapokea "mafisadi" wanaotoka kwenye chama hicho na CHADEMA nayo inawashutumu CCM kwa kuzalisha "mafisadi" wanaoliangamiza taifa.
Lakini inavoonekana ni kwamba CHADEMA na CCM inawajua hao "mafisadi" kwa undani sana ama kinagaubaga. Sisi kama taifa tusiishie kusema fulani na fulani ni "mafisadi" bali ni lazima tulazimishe hao "mafisadi" wachukuliwe hatua.
Lakini inavoonekana kati ya wazalisha "mafisadi" (CCM) na wapokea "mafisadi" (CHADEMA) lazima kati yao wapo ambao wanaulea na kuulinda ufisadi. Ili kumalizana na ufisadi kwenye nchi yetu ni lazima kwanza tupambane na walinda "mafisadi".
Lazima tujiulize ni kwa nini mafisadi hawashitakiwi badala yake tunaishia kusikia CHADEMA na CCM wakiishia kurushiana vijembe majukwaani? Mwenyekiti wa CCM Taifa anasema kwamba "majizi" na "mafisadi" wanakimbilia CHADEMA. Lakini yeye si Rais wa nchi ni kwa nini hawachukulii hatua huko huko CHADEMA walikokimbilia hao "majizi" na "Mafisadi"?
Ni lazima tujue ni nani anawalinda mafisadi kati ya vyama hivi viwili !!
CCM huwa inawashutumu CHADEMA kuwa kuwapokea "mafisadi" wanaotoka kwenye chama hicho na CHADEMA nayo inawashutumu CCM kwa kuzalisha "mafisadi" wanaoliangamiza taifa.
Lakini inavoonekana ni kwamba CHADEMA na CCM inawajua hao "mafisadi" kwa undani sana ama kinagaubaga. Sisi kama taifa tusiishie kusema fulani na fulani ni "mafisadi" bali ni lazima tulazimishe hao "mafisadi" wachukuliwe hatua.
Lakini inavoonekana kati ya wazalisha "mafisadi" (CCM) na wapokea "mafisadi" (CHADEMA) lazima kati yao wapo ambao wanaulea na kuulinda ufisadi. Ili kumalizana na ufisadi kwenye nchi yetu ni lazima kwanza tupambane na walinda "mafisadi".
Lazima tujiulize ni kwa nini mafisadi hawashitakiwi badala yake tunaishia kusikia CHADEMA na CCM wakiishia kurushiana vijembe majukwaani? Mwenyekiti wa CCM Taifa anasema kwamba "majizi" na "mafisadi" wanakimbilia CHADEMA. Lakini yeye si Rais wa nchi ni kwa nini hawachukulii hatua huko huko CHADEMA walikokimbilia hao "majizi" na "Mafisadi"?
Ni lazima tujue ni nani anawalinda mafisadi kati ya vyama hivi viwili !!