Nani ana Mamlaka na Jukumu la Kutayalisha Wazalendo Na Wana Wa Nchi Ya Tanzania?

DSN

JF-Expert Member
Feb 2, 2011
2,837
1,674
Natamani kuwa mzalendo lakini sijui, kwa zama na nyakati hizi za sasa tulipofika ili uwe mzalendo ni sifa zipi zinakufanya kuwa mzalendo?

Napata shida sana naomba mnijuze wanajf hivi ni kweli katika Watanzania Miliioni Alobaini na Usheehee hatuna akina Nyerere wala Edward Moringe Sokoine ambao jamii inaona wanafaha kukuzwa na kupewa dhamana ya kuongoza kwa maslahi na faida ya Watanzania?

Naomba mnijuze nani ana jukumu na mamlaka ya kutayarisha na kuunda Wazalendo na Wana wa Nchi ya Tanzani?.

Na hao Wazalendo au Wana wa Nchi kama Wapo ni kina nani kwa sasa tuwasupport watusaidie kutukwamua kutoka kwenye hofu na mashaka pasipokujali wanatoka chama gani?

Hayati Baba Wa Taifa Mwalimu Julias Kambarage Nyerere na Hayati Edward Moringe Sokoine ni tunu ya viongozi wachache wna wa Nchi ambao walisimamia haki na mali asili ya Watanzania kwa faida yetu na kwa vizazi vyetu.Walisimamia na kuwa na dhamana ya maliasili zote za Taifa, ambazo wangependa unyonyaji wangekuwa matajili wakubwa sana wao na familia zao lakini walikufa maskini, Nijuzeni maswali yangu hayo juu.

Nawasilisha
 
Wenye mamlaka na nyadhifa za kuwakuza na kuwaanda watu kama hao wako upande mwingine kabisa, ufisadi. Kwa hiyo hawawezi kuaanda watu wakuja kuwashitaki na kuwafunga kwa ufisadi walio fanya. Kwa sasa tunahitaji mzalendo mmoja awe mkulu ambaye ataweza kukuza vijana wengi kuwa wazalendo.
 
Wenye mamlaka na nyadhifa za kuwakuza na kuwaanda watu kama hao wako upande mwingine kabisa, ufisadi. Kwa hiyo hawawezi kuaanda watu wakuja kuwashitaki na kuwafunga kwa ufisadi walio fanya. Kwa sasa tunahitaji mzalendo mmoja awe mkulu ambaye ataweza kukuza vijana wengi kuwa wazalendo.

Mkuu LincolinTZA tutampataje huyo Mkulu ambae atatufikisha huko,manake tuliofikilia vijana damu inachemka nao wanaonyesha dalili za kuegemea kaa lenye joto ya la UFISADI.Tufanye kumjua Musa wetu huyo na wafuasi wake?
 
Dr.slaa/lissu na makamanda wote wa chadema watatufikisha huko kwenye uzalendo wa wa mara ya pili
 
Mkuu LincolinTZA tutampataje huyo Mkulu ambae atatufikisha huko,manake tuliofikilia vijana damu inachemka nao wanaonyesha dalili za kuegemea kaa lenye joto ya la UFISADI.Tufanye kumjua Musa wetu huyo na wafuasi wake?

Tunahitaji mtendaji wa kazi na siyo mwanasiasa. Mtu ambaye atanyanyuliwa na wananchi na wala siyo matajiri.
 
Back
Top Bottom