Nani amsimulie Rais Samia namna madini yanavyotoroshwa nchini?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Nadhani simulizi ya wizi inaweza kusimuliwa vyema kwa Mkuu wa nchi ikadhibitiwa kwani yeye anamiliki vyombo vyombo vya udhibiti. Naomba nichokonoe wizi huu wa madini ili wanaohusika wazibe palipotoboka.

Wizi unaweza kufanywa Kwa sababu mwizi amedhamiria kuiba lakini pia wizi unaweza kusababishwa na urasimu wa watoa huduma. Naomba niwaambie kwamba urasimu wa watoa huduma umezalisha nipe nikupe na hapa ndipo milioni moja ya Rushwa inapopofusha macho na kuruhusu madini ya mabilioni kuvuka mpaka.

Nchi jirani wanauza madini yanayozalishwa nchini, wanayatoa wapi? Watu wamehifadhi madini nyumbani je wanavuka nayo vipi maeneo ya uchimbaji?

Mbinu zinazotumika kuiba na kusafirisha madini kinyemela nje ni hizi zifuatazo;

1. Kwenye machimbo ya mirerani watu wanaboresha mahusiano na walinzi, yasemekena hakuna motisha kwa walinzi so kumotishana Kati ya walinzi na wenye madini kunasaidia kuvusha mzigo.

2. Katika mgodi huohuo limezaliwa kundi ambalo linafahamika kama " unajua Mimi ni Nani". Kundi hili limeingia ubia na viongozi na watu wenye nguvu na sasa wanoko wote waliokuwa wanadhibiti madini wanaondolewa waingie makabaila wanaoendana na mfumo wa dili. Ni kawaida Sasa hivi mtu kupiga simu juu akilalamika kusisumbuliwa na viongozi wakubwa kutoa maelekezo bila kujua dhamira ya malalamiko nikusafisha njia.

3. Mipakani hakuna ukaguzi, na penye ukaguzi watu wanaficha mzigo kwenye buti na kuandaa kiasi cha kusafisha njia. Wenye fedha waliojificha kwenye chama hakuna kukaa nikuchekeana tu. Ukitoa fedha kidogo wenye dhamana wanakuita mkarimu na wanakusafishia njia pamoja na kukupigia simu kukuuliza unapita lini Tena?

4. Wapo wenzetu wenye rangi wanaojihita wawekezaji wao wanaondoka nayo kwenye private jet, kumbuka nao wakikaguliwa sana wanalalamika usumbufu na wanasiasa wanawaabudu hivyo vijana wazalendo wanawajibishwa kwa uzalendo wao. Baadhi kurunzi linaeleza wanapita VIP no usumbufu.

5. Wanasiasa na wafanyabiashara wanafidia uporaji waliofanyiw awamu ya tano.

Nini, kifanyike? Mhe. Asomapo umbea huu aufanyie kazi may be atabaini si umber au stori za vijiweni kama nilivyozisikia vijiweni bali ndio ukweli. Vinginevyo kauli ya tumechezewa sana inarudi kwa Kasi tena ikidhaminiwa na watu walewale aliowateua.

Hawa watu sijui kwanini wanapenda kumkwamisha aliyewateua na sijui kwanini anayeteua anawaonea huruma aliowateua wanaomsaliti kwa kuvunja moyo wazalendo wachache waliopo mtaani. Hudumu umbeya wenye ukweli.
 
AdorableHandmadeIrishdraughthorse-size_restricted.gif
 
Kwa hiyo Mkuu hiyo ni Tanzanite au hata dhahabu na almasi? Nasikia Mererani kuna ukuta mkubwa na kamera zaidi ya 10,000 na wenzetu wenye nguo za madoa doa wanalinda pale masaa 24 siku 7 za wiki, nani anathubutu kutorosha madini mbele ya hawa jamaa
 
4. Wapo wenzetu wenye rangi wanaojihita wawekezaji wao wanaondoka nayo kwenye private jet, kumbuka nao wakikaguliwa sana wanalalamika usumbufu na wanasiasa wanawaabudu hivyo vijana wazalendo wanawajibishwa kwa uzalendo wao. Baadhi kurunzi linaeleza wanapita VIP no usumbufu.
Na usijifanye kusahau mkuu; philosophia ya wakati huu ni hii:

"Tanzania inahitaji wawekezaji zaidi, kuliko wawekezaji wanavyoihitaji Tanzania" Hii ni kwa mjibu wa mkuu.

Umeandika mengi, na bado tutayashuhudia mengi sana wakati huu, kwa sababu utawala ndiko wanakotaka kulielekeza taifa. Hivi vikelele vya akina Kamugisha haviwezi kuzuia lolote.
 
Kuna msanii aliimba ukifungua mlango wa mbele hakikisha wa nyuma umefungwa, la sivyo utaikuta Igunga huko.

Sasa sisi inaonekana tumeachia milango yote, ngoma iko Igunga sasa....
 
Kwa mujibu wa mkulu wetu, ufisadi na wizi haujawahi kuwepo awamu hii

Nyinyi acheni kisingizia bhana!

Mnaona Watu wamebeba mawe ya kuogea nanyi mwasema Ni madini?
 
mkuu unajisumbua bure, huyu bibi mbinua macho kama anatoka roho ndo mtoa baraka kwa huo upuuzi unaoendelea, viongozi wetu wana laana yaani badala ya kuzisimamia raslimali zilinufaishe taifa wao wanawasaidia wezi kuliibia taifa madam yao yanawanyookea, wakitoka hapo wanaleta tozo za uzalendo kuwanyonya wasonakitu.
 
mkuu unajisumbua bure, huyu bibi mbinua macho kama anatoka roho ndo mtoa baraka kwa huo upuuzi unaoendelea, viongozi wetu wana laana yaani badala ya kuzisimamia raslimali zilinufaishe taifa wao wanawasaidia wezi kuliibia taifa madam yao yanawanyookea, wakitoka hapo wanaleta tozo za uzalendo kuwanyonya wasonakitu.
Dah. Hilo neno Tozo ya Uzalendo silipendi hata kulisikia limekaa kinafiki sana.
Hii nchi ilivyo na rasilimali mali nyingi hatustahili kufikia hapo.
Yani kiongozi wajipime sana maana viti walivyopewa ni vikibwa na hawaviwezi maana tatizo ni hii mifumo ya elimu ya kukariri wana Doctorate na PhD zisizo na tija wala kunufaisha nchi.
 
Dah. Hilo neno Tozo ya Uzalendo silipendi hata kulisikia limekaa kinafiki sana.
Hii nchi ilivyo na rasilimali mali nyingi hatustahili kufikia hapo.
Yani kiongozi wajipime sana maana viti walivyopewa ni vikibwa na hawaviwezi maana tatizo ni hii mifumo ya elimu ya kukariri wana Doctorate na PhD zisizo na tija wala kunufaisha nchi.
mi hujiuliza hua hawajifunzi kwa wenzao wa mataifa yaloendelea, wenzetu huyaweka mbele zaidi maslahi ya nchi kuliko chochote bt huku kwetu maslahi binafsi ndo kila kitu.
 
Nadhani simulizi ya wizi inaweza kusimuliwa vyema kwa Mkuu wa nchi ikadhibitiwa kwani yeye anamiliki vyombo vyombo vya udhibiti. Naomba nichokonoe wizi huu wa madini ili wanaohusika wazibe palipotoboka.

Wizi unaweza kufanywa Kwa sababu mwizi amedhamiria kuiba lakini pia wizi unaweza kusababishwa na urasimu wa watoa huduma. Naomba niwaambie kwamba urasimu wa watoa huduma umezalisha nipe nikupe na hapa ndipo milioni moja ya Rushwa inapopofusha macho na kuruhusu madini ya mabilioni kuvuka mpaka.

Nchi jirani wanauza madini yanayozalishwa nchini, wanayatoa wapi? Watu wamehifadhi madini nyumbani je wanavuka nayo vipi maeneo ya uchimbaji?

Mbinu zinazotumika kuiba na kusafirisha madini kinyemela nje ni hizi zifuatazo;
1. Kwenye machimbo ya mirerani watu wanaboresha mahusiano na walinzi, yasemekena hakuna motisha kwa walinzi so kumotishana Kati ya walinzi na wenye madini kunasaidia kuvusha mzigo.

2. Katika mgodi huohuo limezaliwa kundi ambalo linafahamika kama " unajua Mimi ni Nani". Kundi hili limeingia ubia na viongozi na watu wenye nguvu na sasa wanoko wote waliokuwa wanadhibiti madini wanaondolewa waingie makabaila wanaoendana na mfumo wa dili. Ni kawaida Sasa hivi mtu kupiga simu juu akilalamika kusisumbuliwa na viongozi wakubwa kutoa maelekezo bila kujua dhamira ya malalamiko nikusafisha njia.

3. Mipakani hakuna ukaguzi, na penye ukaguzi watu wanaficha mzigo kwenye buti na kuandaa kiasi cha kusafisha njia. Wenye fedha waliojificha kwenye chama hakuna kukaa nikuchekeana tu. Ukitoa fedha kidogo wenye dhamana wanakuita mkarimu na wanakusafishia njia pamoja na kukupigia simu kukuuliza unapita lini Tena?

4. Wapo wenzetu wenye rangi wanaojihita wawekezaji wao wanaondoka nayo kwenye private jet, kumbuka nao wakikaguliwa sana wanalalamika usumbufu na wanasiasa wanawaabudu hivyo vijana wazalendo wanawajibishwa kwa uzalendo wao. Baadhi kurunzi linaeleza wanapita VIP no usumbufu.

5. Wanasiasa na wafanyabiashara wanafidia uporaji waliofanyiw awamu ya tano.

Nini, kifanyike? Mhe. Asomapo umbea huu aufanyie kazi may be atabaini si umber au stori za vijiweni kama nilivyozisikia vijiweni bali ndio ukweli. Vinginevyo kauli ya tumechezewa sana inarudi kwa Kasi tena ikidhaminiwa na watu walewale aliowateua. Hawa watu sijui kwanini wanapenda kumkwamisha aliyewateua na sijui kwanini anayeteua anawaonea huruma aliowateua wanaomsaliti kwa kuvunja moyo wazalendo wachache waliopo mtaani. Hudumu umbeya wenye ukweli.
Nilichokigundua hapa wewe hujui lolote kuhusu biashara ya madini. Mbali ya kuwa hujui lakini pia amekubali kufanywa MJINGA WA KILAIKI.
Haya ni matokeo ya nchi kuwa na viongozi waongo na wanafiki waliovaa majoho ya UZALENDO
Embu fanya kwanza utafiti
Biashara ya madini haifanyiki mama kuuza mbuzi kule Pugu mnadani
 
Kwanini mwenye mgodi anakubali kuibiwa?
Au akiibiwa anapata nini?
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 👍
Hivi mleta mada alivyozungumza ,utadhani kuwa Madini yanaibiwa kutoka mashimoni na kuvuushwa nje ya nchi.
Lakini Ukweli ni kwamba ,Watanzania wengi tuu wananufaika kwa kufanikisha mfumo mzima kufanikiwa hadi madini yanatoroshwa nje yanchi.
Mchimbaji anampa dalali, dalali anavuusha hadi nje ya Mgodi na kuwapa chao walinzi wa mlangoni.
Mnunuzi ananunua kw bei anayoitaka Mwenye mali, yaani mchimbaji au dalali wake,
Mlanguzi anavuusha mzigo nakusepa nao ughaibuni ili na yeye ajipatie faida.
Mipakani nako wanakatiwa chochote ili kuwezesha mchakato huu ukamilike.
Sasa mimi SIJAONA TATIZO HAPO WALA HAKUNA ALIYE DHULUMIWA, bali naona kuna wanufaika wengi tuu ambao pato lao linakua na linachangia kuondoa umasikini nchini baada ya serikali kushindwa kufanya hivyo kwa Miaka 60 iliyopita.
Ikiwa Hali itaendelea kama hivi ilivyo, wananchi watainuka sana kimaisha na Matajiri wataongezeka na Mzunguko wa Fedha utakuwa.
 
Back
Top Bottom