Nani amfunge paka kengere?

Byendangwero

JF-Expert Member
Oct 24, 2010
871
56
Watu wote makini, wanakubaliana ya kuwa rais Kikwete hastahili hata kidogo kutuchagulia jopo la wataalamu wa kuratibu mchakato wa uandikaji wa katiba mpya. Hii inatokana na sababu zifuatazo; kwanza, yeye siye aliyeanzisha hoja hiyo, na hivyo itakuwaje basi, akaingilia hoja ya watu bila ya kujadiliana nao kwanza. Pili, kuna ushahidi ya kuwa yeye pamoja na serikali yake hawapendi kuwepo kwa katiba mpya. jambo hilo linazua hofu kwamba kujiingiza kwake kuna lengo la kuizima hoja hiyo. Na mwisho, zoezi hili linahitajika liwe shirikishi katika hatua zote, jambo ambalo halitawezekani ikiwa tume itakayo ratibu mchakato huo itateuliwa na rais. Hii ni kutokana na ukweli kwamba, tume hiyo baada ya kukamilisha kazi yake, inatakiwa itayarishe ripoti ya mapendekezo yake na kuipeleka kwa rais; na rais kwa upande wake ataichambua ripoti hiyo na kuchukua yale tu atakayeona yanamfaa. Katika hali hiyo, hakuna uhakika ya kuwa katiba itakayotokana na mchakato wa aina hiyo, itakuwa inawakilisha matakwa ya watu. Ili kuepukana na kasoro hizo kuna haja kwa wadau wote kukaa pamoja na kukubaliana mfumo utakaotumika katika kufanikisha suala hili. Najua kuna wale wanao amini ya kuwa kazi hiyo itafanywa na bunge, lakini upende husipende, bunge letu lilivyo sasa, haliwezi kufanikisha jambo hilo bila ya kuwepo shinikizo kutoka kwa wadau; hasa kwa wakati huu ambapo rais amekwishatoa msimamo wake, na kwa wakati huo huo wadau mbalimbali wanaonekana kutoa kauli zinazokinzana. Labda tujiulize ni nani achukue jukumu la kuwakutanisha hao wadau. Naona chadema ifanye kazi hiyo. Hii inatokana na ukweli kuwa Katibu wake mkuu anakubalika miongoni mwa wengi wa wadau hao na hivyo anaweza kuwa kiungo muimu.
 
Mwacheni Kikwete ajaze maji kwenye pakacha ,inaonyesha amesahau kama amebakiza miaka mitatu !
 
amebakiza mwaka mmoja as president without CCM remote control....., kwani 2012 uchaguzi mkuu wa CCM chairman mpya ndiye atakua president to be na lazima akabidhiwe remote control....., ok mkuu mwiba
 
Kwa uamuzi wa kujiandikia katiba kivyake bila ya wananchi kumiliki mchakato mzima kwa hatua zote kwangu mimi naona kama Kikwete anajitoa mhanga vile!
 
Kikwete ni mtu makini sana jamani basi tu nyie hamumpendi atawashughulikia mafisadi mpaka mtaona aibu na hii ishu ya katiba haikuwepo kny ilani ya uchaguzi wa ccm ila ya kaahidi kuifuatilia hamuoni kama ni kiongozi mzuri?
 
Kikwete ni mtu makini sana jamani basi tu nyie hamumpendi atawashughulikia mafisadi mpaka mtaona aibu na hii ishu ya katiba haikuwepo kny ilani ya uchaguzi wa ccm ila ya kaahidi kuifuatilia hamuoni kama ni kiongozi mzuri?

No comment.
 
Kikwete ni mtu makini sana jamani basi tu nyie hamumpendi atawashughulikia mafisadi mpaka mtaona aibu na hii ishu ya katiba haikuwepo kny ilani ya uchaguzi wa ccm ila ya kaahidi kuifuatilia hamuoni kama ni kiongozi mzuri?

kuna umakini gani kufuatilia kitu ambacho hakikuwapo kwenye mipango yako?! Acheni unafiki enyi wana kwa kumsingizia kikwete ni mtu makini wakati madudu kibao yametokea chini ya uongozi wake:car:
 
Back
Top Bottom