Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,516
Hadi sasa, saa mbili na dakika 25 usiku wa Alhamisi ya tarehe 7/11/2019 sijasikia hata mgombea mmoja wa Mtaa, Kijiji au Kitongoji wa CCM aliyeenguliwa au kutoteuliwa kugombea nafasi aliyoiomba kwenye uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa.
'Vilio' na malalamiko dhidi ya kuenguliwa na kutoteuliwa kugombea yanatoka tu kwenye vyama vya upinzani. Hata rufaa za wagombea wa upinzani nyingi zimeshatupwa.
Yanatajwa makosa mbalimbali, hasa katika ujazaji wa fomu za kugombea, yaliyopelekea kuenguliwa au kutoteuliwa kwa wagombea wa vyama vya upinzani. Inavyoonekana, wagombea kupitia CCM wamejaza kwa usahihi na kitaalamu fomu zao.
Katika ufanano huo wa wagombea wa CCM wa kutokosea hata kidogo kujaza fomu zao nchini kote(kitu ambacho ni kigumu kwakuwa utofauti wa kibinaadamu haukosekani), nani amewajazia wagombea wa CCM fomu zao kwa utaalamu na usahihi? Kama yupo, inaruhusiwa kujaziwa fomu hizo?
'Vilio' na malalamiko dhidi ya kuenguliwa na kutoteuliwa kugombea yanatoka tu kwenye vyama vya upinzani. Hata rufaa za wagombea wa upinzani nyingi zimeshatupwa.
Yanatajwa makosa mbalimbali, hasa katika ujazaji wa fomu za kugombea, yaliyopelekea kuenguliwa au kutoteuliwa kwa wagombea wa vyama vya upinzani. Inavyoonekana, wagombea kupitia CCM wamejaza kwa usahihi na kitaalamu fomu zao.
Katika ufanano huo wa wagombea wa CCM wa kutokosea hata kidogo kujaza fomu zao nchini kote(kitu ambacho ni kigumu kwakuwa utofauti wa kibinaadamu haukosekani), nani amewajazia wagombea wa CCM fomu zao kwa utaalamu na usahihi? Kama yupo, inaruhusiwa kujaziwa fomu hizo?