BABA TUPAC
JF-Expert Member
- Sep 30, 2015
- 1,527
- 3,801
Wakuu,
Nimekuwa nikisikia sana swaala la kwamba mtu akitukana/ kupiga au akikataa kusaidia wazazi anaweza pata laana kama kufukuzwa kazi, kuwa kichaa au kufariki kabisa.
Binafsi namfaham kijana mmoja alikuwa anasoma UDOM, pindi tu alipofika chuo alianza dharau kwa baba yake mzazi (hakuwa na tatizo na mama yake).
Kijana huyo mzee wake alistaafu kazi Tazara hivyo alikuwepo tu, katika ugomvi na mzee wake siku moja alimtukana mzee wake na kumwambia yupo yupo tu anashinda ndani kuanzia asubuhi mpaka jioni na hana msaada kwa familia (ilitamka maneno haya nje ya nyumba, akiropoka na watu walisikia huku kila mtu akishika kichwa).
Kijana aliendelea na masomo yake lakini ilipofika June/ July, 2011 ikiwa ni kama miezi sita baada ya kumkashifu mzazi wake hadharani kijana huyu alishiriki kwenye mgomo. Baadae chuo cha UDOM kilitoa orodha ya watu waliokuwa chanzo cha mgomo na hivyo kufukuzwa chuo, kijana huyo alifukuzwa chuo na kurudi nyumbani.
Watu wengi mtaani walisema hiyo ni laana toka kwa mzazi wake. Lengo la uzi huu ni kutaka kukusanya shahidi mbali mbali zinahusianisha baadhi ya matukio katika maisha ya watu na kutukana au kutosaidia wazazi wao, je umeshawahi kushuhudia kitu cha namna hii?? lete mambo
Nimekuwa nikisikia sana swaala la kwamba mtu akitukana/ kupiga au akikataa kusaidia wazazi anaweza pata laana kama kufukuzwa kazi, kuwa kichaa au kufariki kabisa.
Binafsi namfaham kijana mmoja alikuwa anasoma UDOM, pindi tu alipofika chuo alianza dharau kwa baba yake mzazi (hakuwa na tatizo na mama yake).
Kijana huyo mzee wake alistaafu kazi Tazara hivyo alikuwepo tu, katika ugomvi na mzee wake siku moja alimtukana mzee wake na kumwambia yupo yupo tu anashinda ndani kuanzia asubuhi mpaka jioni na hana msaada kwa familia (ilitamka maneno haya nje ya nyumba, akiropoka na watu walisikia huku kila mtu akishika kichwa).
Kijana aliendelea na masomo yake lakini ilipofika June/ July, 2011 ikiwa ni kama miezi sita baada ya kumkashifu mzazi wake hadharani kijana huyu alishiriki kwenye mgomo. Baadae chuo cha UDOM kilitoa orodha ya watu waliokuwa chanzo cha mgomo na hivyo kufukuzwa chuo, kijana huyo alifukuzwa chuo na kurudi nyumbani.
Watu wengi mtaani walisema hiyo ni laana toka kwa mzazi wake. Lengo la uzi huu ni kutaka kukusanya shahidi mbali mbali zinahusianisha baadhi ya matukio katika maisha ya watu na kutukana au kutosaidia wazazi wao, je umeshawahi kushuhudia kitu cha namna hii?? lete mambo