Mzukulu
JF-Expert Member
- Feb 14, 2020
- 1,401
- 2,631
Uko zako ndani ya Basi la Mikoani na kwa bahati nzuri unaweza kukuta ama umebahatika Kukaa na Mrembo Kiti Kimoja na unaanza zako Kumuingizia Voko zako au labda Kondakta wa Basi husika ameweka Sinema Moja Kali na Matata yenye iliyo na Mvuto halafu unakuta katikati ya Safari kuna ama Abiria Mwenzenu au Mtu anapanda ndani na Kuanza Kuhubiri tena kwa Makelele makubwa tu.
Hivi nyie Wahubiri mmeambiwa kuwa Sisi Abiria akina Mzukulu hatumjui Mungu? Mbona katika Ndege / Meli / Treni hampandi Kuhubiri hivyo?
Mnakera sana Wanafiki wakubwa nyie. Na Siku zingine muwe na Adabu mjue kuwa siyo Abiria wote huwa ni Wakristo tu bali kuna Waislamu pia.
Hivi nyie Wahubiri mmeambiwa kuwa Sisi Abiria akina Mzukulu hatumjui Mungu? Mbona katika Ndege / Meli / Treni hampandi Kuhubiri hivyo?
Mnakera sana Wanafiki wakubwa nyie. Na Siku zingine muwe na Adabu mjue kuwa siyo Abiria wote huwa ni Wakristo tu bali kuna Waislamu pia.