SONGOKA
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 1,843
- 1,841
Tume ya katiba imenichanganya, imenishangaza na imeniacha hoi..Nani alitoa maoni ya serikali TATU?? je ni asilimia ngapi?? Wananchi wangapi wa kawaida wanaujua muundo huo.?? Kama katika muundo huu tulionao shule hazina madawati, hospitali hazina vifaa, balabala hazina lami, wafanyakazi wanadai malimbikizo, wastaafu hawajalipwa mafao yao, polisi hawana magari, wanachuo hawapati mikopo..n.k... Je tutatoa wapi pesa ya kuunda na kughalimia hiyo serikali ya tatu? kuwajengea majengo, kewanunulia mashangingi, kuwalipa mishahara minono,na nyingine watazoiba??? Kwanini iyo pesa isitumike kupunguza matatizo yetu..au kwa busara ileile waliyotumia wana tume kupendekeza muundo huo, kwa nini wasingependekeza serikali moja ili tuserve pesa kwa ajili ya matatizo lukuki yanayotuandama?? Hii ni nchi ya ajabu sana tena sana, HAINA PRIORITY.. nini cha muhimu, kero za muungano au matatizo ya wananchi ambao hata food, cloth and shelter ni tatizo ?? kwa budgeti yetu tegemezi sikutegemea busara mbovu kama hii.....na kwa msingi huu wa "ingawa wananchi wengi walisema hivi ila tume ikatumia busara" kazi ipo.