Nani Aliyepanga Mishahara Hadi Sh. Mil 40 Kwa Mwezi?

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,319
33,125
Nani Aliyepanga Mishahara Hadi Sh. Mil 40 Kwa Mwezi?




MIONGONI mwa mambo ambayo Rais Magufuli anastahili kupongezwa na Watanzania waadilifu – bila kujali ‘kambi’ zao – ni ujasiri wake wa ‘kuifyekelea mbali’ na kuipunguza mishahara ya baadhi ya waajiriwa serikalini na taasisi za umma iliyokuwa inafikia hadi Shilingi milioni 40 na zaidi kwa mwezi!

Wiki iliyopita kulikuwa na habari kwamba mishahara ya aina hiyo imefyekwa na serikali ya Rais Magufuli na kwamba hakuna Mtanzania anayefanya kazi serikalini na taasisi za umma atakayepokea mshahara zaidi ya Shilingi milioni 15.

Pamoja na hatua hiyo kupongezwa na mamilioni ya maskini wa nchi hii ambao hutembea bila viatu, wakanywa uji usiokuwa na sukari na wakachangia maji ya kunywa na punda katika mabwawa, swali kubwa hapa ni: Nani huyo aliyewapangia watumishi wa umma mishahara hiyo ya mamilioni na wengine akawapangia Shilingi laki mbili (200,000) kwa mwezi?

Ni ajabu kwamba serikali ambayo ndiyo ilibidi ionyeshe mfano mwema kwa waajiri wengine katika sekta binafsi kuhusu mgawanyo wa haki wa mapato na raslimali za taifa kwa wananchi wake, kwa miaka nenda-rudi imekuwa msitari wa mbele kuidharau kanuni hiyo tukufu.



Hii ni ishara ya wazi kwamba nchi ilikuwa imetopea katika dhuluma na ukatili. Ni ufunuo wa wazi kwamba nchi ilikosa wasimamizi waadilifu. Ni dhahiri uongozi wa kiadilifu ulikoma wakati wa Mwalimu Julius Nyerere ukaibuka tena wakati wa Dk. John Magufuli aliyetufumbua macho kuhusu uozo na dhuluma kibao ambazo wasomi na wajanja wa nchi hii wamekuwa wakiwafanyia Watanzania wenzao.

Tumefikia hatua ya ‘mamishahara’ ya aina hiyo kwa vile hapakuwa na kiongozi aliyekuwa anauonea aibu au uchungu umaskini wa Watanzania. Walioingia madarakani waliona wamepata bahati ya kujinufaisha, wakaisahau amri kuu ya Mungu ya: Mpende jirani yako!

Wakawasomesha watoto wao shule za ‘bei mbaya’ wakati watoto wa malofa wakisoma shule duni katika misitu ya Geita na Handeni, wakafurahi kusafiri kwa ndege wakati wengine wakisafiri kwa miguu, wakafanya harusi za mamilioni ya fedha kwao, watoto na wajukuu zao wakati Watanzania wenzao hata kuku mmoja wa Krismas hushindwa kununua!

Yote hayo yanawakumbusha waadilifu wote kwamba Afrika si maskini bali ina umaskini wa viongozi waadilifu na makini! Afrika ina kila aina ya utajiri ambao ungeifanya kuwa Bustani ya Eden iwapo ingekuwa na viongozi waadilifu.

Kiongozi ‘siriazi’ hatakubali uongozi wake utoe mshahara wa Sh. 45,000,000 kwa watumishi fulani na Sh. 200,000/= kwa watumishi wengine serikalini na taasisi zake – hata kama kuna tofauti za aina gani katika viwango vya elimu na utaalam, kwani masuala ya tiba, malazi, chakula na kadhalika wote wanakutana nayo mitaani.

Tofauti ya Sh. 45,000,000 na Sh. 200,000 katika mishahara ni kubwa mno hata malaika wa mbinguni hawawezi kuikubali. Kukubali tofauti ya aina hii kwa watu wanaoamka wote pamoja asubuhi kwenda kuwahudumia wananchi wenzao hospitalini, jeshini, shuleni, benki, na kadhalika, hakika ni kufanya dhambi! Ni kwa vile wote hao wana thamani sawa katika kuitumikia jamii.

Lakini, yote hayo yamefanyika mbele ya Watanzania wote, wakiwemo viongozi wa dini, wazee na vijana ambao wameiona dhuluma hii na wakaendelea kukaa kimya wasijue kwamba ndiyo huzaa ‘Panya Road’ na matatizo mengine. Ni kwa sababu kile alichotupa Mungu katika nchi yetu, tangu mbuga za wanyama, madini ya Tanzanite, dhahabu na kadhalika, vinafaidiwa na wachache kwa kisingizio kwamba walipoteza muda mwingi wakiwa darasani!

Wasomi wanasahau kwamba wananchi wenzao nao hupoteza muda wote wa maisha yao wakilima mpunga na mahindi ambayo kila mtu anavitumia kila siku.

Pamoja na kumtakia kila la heri Rais Magufuli katika kutufumbua macho na kuibomoa msingi yote ya dhuluma iliyodumu miaka kibao, safu hii inamwambia wazi kwamba uongozi uliomtangulia ndiyo uliotufikisha katika Tanzania aliyoikuta wakati anaingia Ikulu!

Mungu anawaona!

Mwandishi: Walusanga Ndaki
GBP.
 

Attachments

  • simu banking..jpg
    simu banking..jpg
    77.1 KB · Views: 596
  • PESA.jpg
    PESA.jpg
    34 KB · Views: 94
Vision ya taifa ilikuwa ni kuongeza idadi ya watu wenye kipato cha kati(middle class).
Nchi yenye idadi kubwa ya wananchi wenye kipato cha kati,uchumi hukua na kuongeza shughuli mbalimbali zenye kuongeza mzunguko wa fedha.
'Ni bora kuongezea aliyochini ili amfikie aliye juu',
Mtazamo huu wa kuwarudisha nyuma walio juu,inatudisha nyuma ukuaji wa kiuchumi,kwani tatizo lilokuwa linapigiwa kelele ilikuwa,ni Serikali kushindwa kuwanyanyua wale wenye vipato vidogo.
Ukiangalia,bado hata hao waliochini bado mishahara haiongezwi.
Kwa hiyo,inawezekana kuna tatizo lingine zaidi ya hatua hizi zinachukuliwa za kupunguza kipato cha waliofikia viwango vya juu katika kipato.
 
Serikali ya ccm na tamaa zao ndio waliotufikisha huko.



swissme
 
Salary slip yake ya mshahara wa 9.5 million aliyoahidi kuiweka hadharani tangu April, 2016 imepotelea wapi? Mbona yeye anapata U$192,000 kwa mwaka sawa na 403 million na gharama zake zote na familia yake kwa mwaka mzima zinalipwa na walipa kodi hivyo mshahara wake hauna kazi yoyote? Je, kishaufyeka mshahara wake kwa kiasi gani?
 
Nani Aliyepanga Mishahara Hadi Sh. Mil 40 Kwa Mwezi?




MIONGONI mwa mambo ambayo Rais Magufuli anastahili kupongezwa na Watanzania waadilifu – bila kujali ‘kambi’ zao – ni ujasiri wake wa ‘kuifyekelea mbali’ na kuipunguza mishahara ya baadhi ya waajiriwa serikalini na taasisi za umma iliyokuwa inafikia hadi Shilingi milioni 40 na zaidi kwa mwezi!

Wiki iliyopita kulikuwa na habari kwamba mishahara ya aina hiyo imefyekwa na serikali ya Rais Magufuli na kwamba hakuna Mtanzania anayefanya kazi serikalini na taasisi za umma atakayepokea mshahara zaidi ya Shilingi milioni 15.

Pamoja na hatua hiyo kupongezwa na mamilioni ya maskini wa nchi hii ambao hutembea bila viatu, wakanywa uji usiokuwa na sukari na wakachangia maji ya kunywa na punda katika mabwawa, swali kubwa hapa ni: Nani huyo aliyewapangia watumishi wa umma mishahara hiyo ya mamilioni na wengine akawapangia Shilingi laki mbili (200,000) kwa mwezi?

Ni ajabu kwamba serikali ambayo ndiyo ilibidi ionyeshe mfano mwema kwa waajiri wengine katika sekta binafsi kuhusu mgawanyo wa haki wa mapato na raslimali za taifa kwa wananchi wake, kwa miaka nenda-rudi imekuwa msitari wa mbele kuidharau kanuni hiyo tukufu.



Hii ni ishara ya wazi kwamba nchi ilikuwa imetopea katika dhuluma na ukatili. Ni ufunuo wa wazi kwamba nchi ilikosa wasimamizi waadilifu. Ni dhahiri uongozi wa kiadilifu ulikoma wakati wa Mwalimu Julius Nyerere ukaibuka tena wakati wa Dk. John Magufuli aliyetufumbua macho kuhusu uozo na dhuluma kibao ambazo wasomi na wajanja wa nchi hii wamekuwa wakiwafanyia Watanzania wenzao.

Tumefikia hatua ya ‘mamishahara’ ya aina hiyo kwa vile hapakuwa na kiongozi aliyekuwa anauonea aibu au uchungu umaskini wa Watanzania. Walioingia madarakani waliona wamepata bahati ya kujinufaisha, wakaisahau amri kuu ya Mungu ya: Mpende jirani yako!

Wakawasomesha watoto wao shule za ‘bei mbaya’ wakati watoto wa malofa wakisoma shule duni katika misitu ya Geita na Handeni, wakafurahi kusafiri kwa ndege wakati wengine wakisafiri kwa miguu, wakafanya harusi za mamilioni ya fedha kwao, watoto na wajukuu zao wakati Watanzania wenzao hata kuku mmoja wa Krismas hushindwa kununua!

Yote hayo yanawakumbusha waadilifu wote kwamba Afrika si maskini bali ina umaskini wa viongozi waadilifu na makini! Afrika ina kila aina ya utajiri ambao ungeifanya kuwa Bustani ya Eden iwapo ingekuwa na viongozi waadilifu.

Kiongozi ‘siriazi’ hatakubali uongozi wake utoe mshahara wa Sh. 45,000,000 kwa watumishi fulani na Sh. 200,000/= kwa watumishi wengine serikalini na taasisi zake – hata kama kuna tofauti za aina gani katika viwango vya elimu na utaalam, kwani masuala ya tiba, malazi, chakula na kadhalika wote wanakutana nayo mitaani.

Tofauti ya Sh. 45,000,000 na Sh. 200,000 katika mishahara ni kubwa mno hata malaika wa mbinguni hawawezi kuikubali. Kukubali tofauti ya aina hii kwa watu wanaoamka wote pamoja asubuhi kwenda kuwahudumia wananchi wenzao hospitalini, jeshini, shuleni, benki, na kadhalika, hakika ni kufanya dhambi! Ni kwa vile wote hao wana thamani sawa katika kuitumikia jamii.

Lakini, yote hayo yamefanyika mbele ya Watanzania wote, wakiwemo viongozi wa dini, wazee na vijana ambao wameiona dhuluma hii na wakaendelea kukaa kimya wasijue kwamba ndiyo huzaa ‘Panya Road’ na matatizo mengine. Ni kwa sababu kile alichotupa Mungu katika nchi yetu, tangu mbuga za wanyama, madini ya Tanzanite, dhahabu na kadhalika, vinafaidiwa na wachache kwa kisingizio kwamba walipoteza muda mwingi wakiwa darasani!

Wasomi wanasahau kwamba wananchi wenzao nao hupoteza muda wote wa maisha yao wakilima mpunga na mahindi ambayo kila mtu anavitumia kila siku.

Pamoja na kumtakia kila la heri Rais Magufuli katika kutufumbua macho na kuibomoa msingi yote ya dhuluma iliyodumu miaka kibao, safu hii inamwambia wazi kwamba uongozi uliomtangulia ndiyo uliotufikisha katika Tanzania aliyoikuta wakati anaingia Ikulu!

Mungu anawaona!

Mwandishi: Walusanga Ndaki
GBP.

Mbaya zaidi wananchi wote hao Wananunua mchele, sukari, hata nguo na kupangisha nyumba ktk soko moja.

Haikuwa fair
 
Kichokuwa kinatakiwa sio kupunguza salary kwa wenye kipato cha juu,hapo katikat kuna kundi linatakiwa kuongezewa salary ili nao wajiongezee shughuli za kiuchumi,hii itaongeza mzunguko wa pesa,hilo kundi limesahaulika na hali ya uchumi inayumba nchin
 
Kichokuwa kinatakiwa sio kupunguza salary kwa wenye kipato cha juu,hapo katikat kuna kundi linatakiwa kuongezewa salary ili nao wajiongezee shughuli za kiuchumi,hii itaongeza mzunguko wa pesa,hilo kundi limesahaulika na hali ya uchumi inayumba nchin

Unamaanisha kima.cha chini.kiwe ten million.
Kwa kodi gani.inayopatkana? You can't be serious
 
Mishara kama hiyo wanatakiwa kulipwa raisi makamu raisi na waziri mkuu tu wengine mishahara isizidi sh mil 8 hiyo milioni 15 bado nyingi sana
 
Nani Aliyepanga Mishahara Hadi Sh. Mil 40 Kwa Mwezi?




MIONGONI mwa mambo ambayo Rais Magufuli anastahili kupongezwa na Watanzania waadilifu – bila kujali ‘kambi’ zao – ni ujasiri wake wa ‘kuifyekelea mbali’ na kuipunguza mishahara ya baadhi ya waajiriwa serikalini na taasisi za umma iliyokuwa inafikia hadi Shilingi milioni 40 na zaidi kwa mwezi!

Wiki iliyopita kulikuwa na habari kwamba mishahara ya aina hiyo imefyekwa na serikali ya Rais Magufuli na kwamba hakuna Mtanzania anayefanya kazi serikalini na taasisi za umma atakayepokea mshahara zaidi ya Shilingi milioni 15.

Pamoja na hatua hiyo kupongezwa na mamilioni ya maskini wa nchi hii ambao hutembea bila viatu, wakanywa uji usiokuwa na sukari na wakachangia maji ya kunywa na punda katika mabwawa, swali kubwa hapa ni: Nani huyo aliyewapangia watumishi wa umma mishahara hiyo ya mamilioni na wengine akawapangia Shilingi laki mbili (200,000) kwa mwezi?

Ni ajabu kwamba serikali ambayo ndiyo ilibidi ionyeshe mfano mwema kwa waajiri wengine katika sekta binafsi kuhusu mgawanyo wa haki wa mapato na raslimali za taifa kwa wananchi wake, kwa miaka nenda-rudi imekuwa msitari wa mbele kuidharau kanuni hiyo tukufu.



Hii ni ishara ya wazi kwamba nchi ilikuwa imetopea katika dhuluma na ukatili. Ni ufunuo wa wazi kwamba nchi ilikosa wasimamizi waadilifu. Ni dhahiri uongozi wa kiadilifu ulikoma wakati wa Mwalimu Julius Nyerere ukaibuka tena wakati wa Dk. John Magufuli aliyetufumbua macho kuhusu uozo na dhuluma kibao ambazo wasomi na wajanja wa nchi hii wamekuwa wakiwafanyia Watanzania wenzao.

Tumefikia hatua ya ‘mamishahara’ ya aina hiyo kwa vile hapakuwa na kiongozi aliyekuwa anauonea aibu au uchungu umaskini wa Watanzania. Walioingia madarakani waliona wamepata bahati ya kujinufaisha, wakaisahau amri kuu ya Mungu ya: Mpende jirani yako!

Wakawasomesha watoto wao shule za ‘bei mbaya’ wakati watoto wa malofa wakisoma shule duni katika misitu ya Geita na Handeni, wakafurahi kusafiri kwa ndege wakati wengine wakisafiri kwa miguu, wakafanya harusi za mamilioni ya fedha kwao, watoto na wajukuu zao wakati Watanzania wenzao hata kuku mmoja wa Krismas hushindwa kununua!

Yote hayo yanawakumbusha waadilifu wote kwamba Afrika si maskini bali ina umaskini wa viongozi waadilifu na makini! Afrika ina kila aina ya utajiri ambao ungeifanya kuwa Bustani ya Eden iwapo ingekuwa na viongozi waadilifu.

Kiongozi ‘siriazi’ hatakubali uongozi wake utoe mshahara wa Sh. 45,000,000 kwa watumishi fulani na Sh. 200,000/= kwa watumishi wengine serikalini na taasisi zake – hata kama kuna tofauti za aina gani katika viwango vya elimu na utaalam, kwani masuala ya tiba, malazi, chakula na kadhalika wote wanakutana nayo mitaani.

Tofauti ya Sh. 45,000,000 na Sh. 200,000 katika mishahara ni kubwa mno hata malaika wa mbinguni hawawezi kuikubali. Kukubali tofauti ya aina hii kwa watu wanaoamka wote pamoja asubuhi kwenda kuwahudumia wananchi wenzao hospitalini, jeshini, shuleni, benki, na kadhalika, hakika ni kufanya dhambi! Ni kwa vile wote hao wana thamani sawa katika kuitumikia jamii.

Lakini, yote hayo yamefanyika mbele ya Watanzania wote, wakiwemo viongozi wa dini, wazee na vijana ambao wameiona dhuluma hii na wakaendelea kukaa kimya wasijue kwamba ndiyo huzaa ‘Panya Road’ na matatizo mengine. Ni kwa sababu kile alichotupa Mungu katika nchi yetu, tangu mbuga za wanyama, madini ya Tanzanite, dhahabu na kadhalika, vinafaidiwa na wachache kwa kisingizio kwamba walipoteza muda mwingi wakiwa darasani!

Wasomi wanasahau kwamba wananchi wenzao nao hupoteza muda wote wa maisha yao wakilima mpunga na mahindi ambayo kila mtu anavitumia kila siku.

Pamoja na kumtakia kila la heri Rais Magufuli katika kutufumbua macho na kuibomoa msingi yote ya dhuluma iliyodumu miaka kibao, safu hii inamwambia wazi kwamba uongozi uliomtangulia ndiyo uliotufikisha katika Tanzania aliyoikuta wakati anaingia Ikulu!

Mungu anawaona!

Mwandishi: Walusanga Ndaki
GBP.
Pia kuna Viongozi hapo hapo wanakubali Mtumishi aliyejiendeleza kimasomo Ashushwe mshahara kwa kusoma fani nyingine. "Rec categorization". Eti umesoma fani za watu! Hapo hapo walikuwa wanapitisha safari, semina, warsha kwa kikundi cha watu hao hao kila siku. Huwezi amini kuna baadhi ya watumishi hawajawahi kutoka nje ya mkoa wanaofanyia kazi kikazi. Rais wetu Mungu akulinde hakika unajitahidi kuvunja System za ulaji wa wachache Utumishi wa Umma. Geuza mawe yote ikiwezekana tupatie fursa ya mtandao ya kumwaga uozo wote Utumishi wa Umma.
 
Salary slip yake ya mshahara wa 9.5 million aliyoahidi kuiweka hadharani tangu April, 2016 imepotelea wapi? Mbona yeye anapata U$192,000 kwa mwaka sawa na 403 million na gharama zake zote na familia yake kwa mwaka mzima zinalipwa na walipa kodi hivyo mshahara wake hauna kazi yoyote? Je, kishaufyeka mshahara wake kwa kiasi gani?
Mimi nilikua ninasubiri kuskia mswaada wa Sheria ya kukatwa kodi kwenye mshahara wa Raisi ili alipe kodi kama watanzania wengine. Kimyaaaaa!
 
Nampongeza pia kwafuta service charges ambazo zilikuwa hazieleweki tunalipa za nini?
 
Salary slip yake ya mshahara wa 9.5 million aliyoahidi kuiweka hadharani tangu April, 2016 imepotelea wapi? Mbona yeye anapata U$192,000 kwa mwaka sawa na 403 million na gharama zake zote na familia yake kwa mwaka mzima zinalipwa na walipa kodi hivyo mshahara wake hauna kazi yoyote? Je, kishaufyeka mshahara wake kwa kiasi gani?
Habari hiyo kamwe hutamsikia yeye wala vijana wa lumumba wakizungumzia.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom