Nani aliyemwapisha Spika na kwanini?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Nilikuwa nazungumza na mzalendo mmoja mwishoni mwa juma na akaniuliza maswali fulani yakitu ambacho labda hatukukiangalia kilipotokea.

a. Rais akitangazwa kuwa Rais anaapishwa na Jaji Mkuu - Mkuu wa Mhimili
b. Jaji Mkuu akiteuliwa anaapishwa na Rais - Mkuu wa Mhimili
c. Spika akitangazwa kuwa Spika anaapishwa na Katibu wa Bunge - mtumishi wa Umma (Civil servant).

Katika mazungumzo yangu na mkulu huyo mmoja jingine likajitokeza:

a) Wabunge wanakuwa Wabunge wakati gani? - Wanapotangazwa na RO kuwa wameshinda na hasa inaposemwa "Namtangaza X,Y kuwa ni Mbunge halali wa Jimbo la M" au
b) Anapokuja Bungeni na kula kiapo cha Ubunge?

Kama jawabu ni (a) kwanini Mbunge huyo asiapishwa hapo hapo kuwa Mbunge na anasubiri kuja Bungeni kuapishwa wakati tayari ametangazwa kuwa ni Mbunge?

Kama jawabu ni (b) kwanini RO anamtangaza mtu kuwa Mbunge badala ya kumtangaza tu kuwa ameshinda kura za Ubunge na anakuwa "Mbunge Mteule" hadi pale atakapoapishwa?

Tulipoliangalia hilo tukajikuta tunaingia kwenye tatizo jingine:

Wabunge "wateule" wanapopiga kura kumchagua Spika wanapata wapi hizo nguvu hizo wakati hawajaapa kuilinda na kuitetea Katiba? Aidha ni wabunge au siyo kama ni wabunge kwanini wakishamchagua Spika huyo Spika ndio anawaapisha wao kuwa wabunge?

Well.. I'm confused enough.. and talk about "no need for a new constitution"...
 
Yote uliyoongea ni sehemu ya mapungufu ya Katiba yetu. Hata hivyo kuhusu mbunge, ninadhani kuwa anakuwa mbunge mara tu baada ya kuchaguliwa na watu wake na kutangazwa na returning officer. Kuapishwa bungeni hufanyika ili kumruhusu kushiriki mijadala ya bunge; asipoapishwa na bunge hawezi kukosa ubunge wake lakini nadhani hataruhusiwa kushiriki mijadala ya bungeni.

katiba na sheria zetu zina mapungufu mengi sana ikiwa na pale waapaji wanapoamua kwa makusudi kutokutumia misahafu ya dini zao.
 
Mwakei,

Mbona wewe unaleta vurugu na kuchokonoa ilhali bado hatujajua kura za Urais tunazitatua vipi? Nawe umezidi ubundi!
 
Yote uliyoongea ni sehemu ya mapungufu ya Katiba yetu. Hata hivyo kuhusu mbunge, ninadhani kuwa anakuwa mbunge mara tu baada ya kuchaguliwa na watu wake na kutangazwa na returning officer. Kuapishwa bungeni hufanyika ili kumruhusu kushiriki mijadala ya bunge; asipoapishwa na bunge hawezi kukosa ubunge wake lakini nadhani hataruhusiwa kushiriki mijadala ya bungeni.

katiba na sheria zetu zina mapungufu mengi sana ikiwa na pale waapaji wanapoamua kwa makusudi kutokutumia misahafu ya dini zao.

Hivi kwa nini tunataka kumshirikisha mungu katika sehemu ambayo tunalazimika kufuata sheria za kibinaadamu?

What if katiba anayoapa kuitekeleza inapingana na sheria za mungu wake anaemuamini?

Ukiapa kwa msahafu mathalan, kipi kinakuwa na nguvu ya maamuzi yako, katiba au msahafu? Ulichoapa au ulichoapia?

Na kwa wale wasioamini mungu jee?
 
Mwanakijiji, if you were a teacher... (or if you are a teacher as i write) you students must be very lucky, though lazy ones would complain, umepembua hadi ukakuta mchele una ngano kidogo

big up! najifunza everyday namna ya kuangalia issues zinazohusu haki za raia na wajibu wao
 
Mkjj umeanza uchochezi eti??? hahah ahaha ahaha! muda si mrefu Wazee wa DSM wataandamana kushutumu uchochezi wako! Hahaha ahaha.

Anyways, Good one bro! najiuliza kwa nini miaka yoote hii hili jambo halikuwahi kuongelewa. Au ndiyo ule utaratibu kwamba serikali ikisema, ikipanga, ikifikiri haikosei.
 
kwa kweli hili hata mimi sikulifikiria hadi nilipozungumza na huyu ndugu Ijumaa ambaye ni mtumishi kigogo tu wa serikali hii; kuna maswali mengine ambayo aliniuliza na naona hata woga kuyauliza maana wasije kunifanyia press conference bure.. I mean kina Chiligati au Waziri ajaye wa Habari na Utamaduni..
 
Nilikuwa nazungumza na mzalendo mmoja mwishoni mwa juma na akaniuliza maswali fulani yakitu ambacho labda hatukukiangalia kilipotokea.

a. Rais akitangazwa kuwa Rais anaapishwa na Jaji Mkuu - Mkuu wa Mhimili
b. Jaji Mkuu akiteuliwa anaapishwa na Rais - Mkuu wa Mhimili
c. Spika akitangazwa kuwa Spika anaapishwa na Katibu wa Bunge - mtumishi wa Umma (Civil servant).

Katika mazungumzo yangu na mkulu huyo mmoja jingine likajitokeza:

a. Wabunge wanakuwa Wabunge wakati gani? - Wanapotangazwa na RO kuwa wameshinda na hasa inaposemwa "Namtangaza X,Y kuwa ni Mbunge halali wa Jimbo la M" au
b. Anapokuja Bungeni na kula kiapo cha Ubunge?

Kama jawabu ni (a) kwanini Mbunge huyo asiapishwa hapo hapo kuwa Mbunge na anasubiri kuja Bungeni kuapishwa wakati tayari ametangazwa kuwa ni Mbunge?

b. Kama jawabu ni (B) kwanini RO anamtangaza mtu kuwa Mbunge badala ya kumtangaza tu kuwa ameshinda kura za Ubunge na anakuwa "Mbunge Mteule" hadi pale atakapoapishwa?

Tulipoliangalia hilo tukajikuta tunaingia kwenye tatizo jingine:

Wabunge "wateule" wanapopiga kura kumchagua Spika wanapata wapi hizo nguvu hizo wakati hawajaapa kuilinda na kuitetea Katiba? Aidha ni wabunge au siyo kama ni wabunge kwanini wakishamchagua Spika huyo Spika ndio anawaapisha wao kuwa wabunge?

Well.. I'm confused enough.. and talk about "no need for a new constitution"...

Kwanza nakushukuru sana mkuu kwa kuitendea haki JF - kweli ni "home of great thinkers", kwa hoja kama hizi. sasa nilipitisha macho haraka kwenye katiba yetu, angalau nakala niliyonayo inaeleza yafuatayo
1. Mbunge aliyechaguliwa na wananchi katika uchaguzi atakuwa mbunge baada ya kutangazwa na Tume ya uchaguzi, kwa kuwa ndiyo yenye mamlaka kwa mujibu wa Ibara ya 74 ya katiba, ibara ndogo 6(b). RO anafanya kazi kwa maagizo ya Tume ya uchaguzi, lakini ni Tume yenyewe yenye mamlaka ya kutangaza. aidha katika ibara hiyohiyo, ibara ndogo ya 12 inasema:

"Hakuna mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka ya
kuchunguza jambo lolote lililotendwa na Tume ya Uchaguzi katika​
kutekeleza madaraka yake kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii."

kwa hiyo hata kama Tume imechakachua, haiwezekani kuihoji uchakachuaji wake.

2. Ibara ya 68 ya katiba inasema:
"Kila Mbunge atatakiwa kuapishwa katika Bunge kiapo cha
uaminifu kabla hajaanza kushiriki katika shughuli za Bunge; lakini
Mbunge aweza kushiriki katika uchaguzi wa Spika hata kabla​
hajaapishwa."

Maana yake huyu ni mbunge tayari, ila ili aweze kushiriki shughuli za Bunge, imempasa kula kiapo cha uaminifu. naona watunga katiba waliliona hili unalolisema na ndio maana wakaweka hiyo "provision" ya kumchagua Spika kabla ya wao wenyewe kuapishwa.

Kimsingi nakubaliana kwamba katiba hii haitufai kwa sasa na tunahitaji katiba mpya. naona ndio msingi wa hoja yako
 
Mindi asante sana.. lakini hujajaribu kugusia nani anamwapisha Spika na kwa nini? Najua sheria na Katiba inasema nini.. ninaulizia something deeper kidogo.. kwanini SPIKA haapishwi na Jaji MKUu kama Rais anavyoapishwa?
 
Hili la kuaapa kuna jambo! inamaana bunge lina hadhi ndogo kiasi hiki? kwamba Mkuu wake anaapisha hovyo hovyo tu?sikuwahi fikiria
 
mwanakijiji,tunashukuru kwa hoja nzuri,ni kweli bado kunatatizo ktk katiba ya hii nchi,haiwezekani katibu wa bunge kumwapisha spika wa bunge ambe anaongoza mhimili wa 3 wa serikali,lakini pia tutambuwe kuwa mwakilishi aliyechaguliwa na wapigakura ni mbunge tosha na anaitwa mteule kwa kuwa bado hajapata baraka za spika,ila hilo halimzuii yeye kuwa mbunge,haya mengine ya wabunge kumchaguwa spika then huyo spika kuwaapisha wabunge ni utaratibu tu ambao hauna msingi wowote ule

mapinduziiiii daimaaaaaa
 
Labda tuanzie hapa: KATIBU wa BUNGE anateuliwaje? Sifa zake ni zipi? Ana hadhi sawa na JAJI wa Mahakama kuu? ROs ambao karibu wote ni WAKURUGENZI wa Halmashauri/Manispaa/miji wanao uwezo KIKATIBA kumtangaza mtu kuwa ni DIWANI/MBUNGE? Viapo hivi vya kushika vitabu vitakatifu badala ya KATIBA ya NCHI sio UDINI kweli wakati tunasema kila mara NCHI yetu haina DINI?
 
Halafu tunakosea jambo moja. Rais haapishwi na Jaji Mkuu. Anaapa mbele ya Jaji Mkuu (42.5 ya Katiba ya JMT)
 
kwa kweli hili hata mimi sikulifikiria hadi nilipozungumza na huyu ndugu Ijumaa ambaye ni mtumishi kigogo tu wa serikali hii; kuna maswali mengine ambayo aliniuliza na naona hata woga kuyauliza maana wasije kunifanyia press conference bure.. I mean kina Chiligati au Waziri ajaye wa Habari na Utamaduni..

MMK,
Usihofu kuyauliza,kwani ndo twajifunza kupia kwayo.
 
Halafu tunakosea jambo moja. Rais haapishwi na Jaji Mkuu. Anaapa mbele ya Jaji Mkuu (42.5 ya Katiba ya JMT)

kuna tofauti gani hapo mkuu?
basi kama ni hivyo hata Jaji mkuu haapishwi na rais bali anaapa mbele ya rais.
Mi naona ni lugha tu hapo ndugu yangu.
 
Thats why i like JF, unapata upembuzi yakinifu! ila wakija wanasihasa wataharibu sasa hivi badala ya kujenga hoja. Ahsanteni sana
 
Mwanakijiji kwa mujibu wa Mwanasheria wa Katiba aliyebobea nchini, katika muundo wa Tanzania, Spika sio Kiongozi wa Mhimili wowote wa Uongozi. Inabidi ufikiri sana uelewe hoja hii - walinganishe Rais, Jaji Mkuu na Spika wa Bunge utaona kuwa hao wawili wa kwanza ndio wana madaraka katika mihimili yao, yaani Serikali na Mahakama. Kwa maana nyingine, Spika sio Kiongozi wa Bunge - ni muendeshaji/mratibu (modereta) tu!
 
Hii nimeipenda kwani umeutendea vema mtandao " The Home of Great Thinkers" Big up MKJJ. Kama msemo wa Entrepreneurs unaosema " When others see darkness good entrepreneurs see light".

Nilikuwa nazungumza na mzalendo mmoja mwishoni mwa juma na akaniuliza maswali fulani yakitu ambacho labda hatukukiangalia kilipotokea.

a. Rais akitangazwa kuwa Rais anaapishwa na Jaji Mkuu - Mkuu wa Mhimili
b. Jaji Mkuu akiteuliwa anaapishwa na Rais - Mkuu wa Mhimili
c. Spika akitangazwa kuwa Spika anaapishwa na Katibu wa Bunge - mtumishi wa Umma (Civil servant).

Katika mazungumzo yangu na mkulu huyo mmoja jingine likajitokeza:

a. Wabunge wanakuwa Wabunge wakati gani? - Wanapotangazwa na RO kuwa wameshinda na hasa inaposemwa "Namtangaza X,Y kuwa ni Mbunge halali wa Jimbo la M" au
b. Anapokuja Bungeni na kula kiapo cha Ubunge?

Kama jawabu ni (a) kwanini Mbunge huyo asiapishwa hapo hapo kuwa Mbunge na anasubiri kuja Bungeni kuapishwa wakati tayari ametangazwa kuwa ni Mbunge?

b. Kama jawabu ni (B) kwanini RO anamtangaza mtu kuwa Mbunge badala ya kumtangaza tu kuwa ameshinda kura za Ubunge na anakuwa "Mbunge Mteule" hadi pale atakapoapishwa?

Tulipoliangalia hilo tukajikuta tunaingia kwenye tatizo jingine:

Wabunge "wateule" wanapopiga kura kumchagua Spika wanapata wapi hizo nguvu hizo wakati hawajaapa kuilinda na kuitetea Katiba? Aidha ni wabunge au siyo kama ni wabunge kwanini wakishamchagua Spika huyo Spika ndio anawaapisha wao kuwa wabunge?

Well.. I'm confused enough.. and talk about "no need for a new constitution"...
 
Back
Top Bottom