Nani alikudanganya kuwa CCM na Polisi Tanzania hawana Vinasaba vya Undugu, Mshikamano na Ushirikiano?

Mzukulu

JF-Expert Member
Feb 14, 2020
1,401
2,631
ULINZI WAIMARISHWA DODOMA:

Dodoma: 07 Julai, 2020

Wakati vikao vya uamuzi vya Chama Cha Mapinduzi vikitarajiwa kufanyika Jijini Dodoma, ukiwemo Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chama hicho, Jeshi la Polisi limesema limeimarisha zaidi hali ya ulinzi na usalama.

Mkutano mkuu utafanyika Jumamosi na Jumapili na utakuwa na kazi ya kuchagua jina moja la mgombea wa CCM wa uraisi kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Zanzibar.

Leo katika mkutano na waandishi wa habari, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, ametoa onyo kali kwa yeyote atakayejaribu kuleta fujo au utapeli wakati wa vikao na mkutano mkuu wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi.

Aidha, Kamanda Muroto, amewatoa hofu wageni wote watakaohudhuria mkutano huo kuwa hali ya ulinzi na usalama wa mali zao, umeimarishwa zaidi.

uhurudigital

Najaribu Kukumbuka ni lini nimewahi kukutana na Statement kama hii ikielekezwa kwa Vyama mahiri vya Upinzani kama CHADEMA, CUF na ACT.
 
Gentamycine!
The Greatest Popoma on the Planet

Ukibadili ID badili na mwandiko basi! Mbona ni simple psychology haiitaji hata rocket science au PhD?!
 
Tamko hilo lingetamkwa mkutano wa chadema humu kusingetosha polisi wangetukanwa na Bavicha Hadi basi kuwa lengo Ni kuwadhibiti chadema ili wasiwe na Uhuru
 
CCM Tunayoijuwa sisi ilikuwa Kila kitu tunajitolea kujenga ofisi na Mengine kwa nguvu zetu

Ccm mpya ni Chama dola .. hakuna watu wa kujitolea hata bendera wanapandishiwa na askari au wafungwa
Bendera za wenzao wanatuma Polisi washushe


IMG_2637.jpg
 
ULINZI WAIMARISHWA DODOMA:

Dodoma: 07 Julai, 2020

Wakati vikao vya uamuzi vya Chama Cha Mapinduzi vikitarajiwa kufanyika Jijini Dodoma, ukiwemo Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chama hicho, Jeshi la Polisi limesema limeimarisha zaidi hali ya ulinzi na usalama.

Mkutano mkuu utafanyika Jumamosi na Jumapili na utakuwa na kazi ya kuchagua jina moja la mgombea wa CCM wa uraisi kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Zanzibar.

Leo katika mkutano na waandishi wa habari, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, ametoa onyo kali kwa yeyote atakayejaribu kuleta fujo au utapeli wakati wa vikao na mkutano mkuu wa taifa wa Chama Cha Mapinduzi.

Aidha, Kamanda Muroto, amewatoa hofu wageni wote watakaohudhuria mkutano huo kuwa hali ya ulinzi na usalama wa mali zao, umeimarishwa zaidi.

uhurudigital

Najaribu Kukumbuka ni lini nimewahi kukutana na Statement kama hii ikielekezwa kwa Vyama mahiri vya Upinzani kama CHADEMA, CUF na ACT.
Ukishangaa ya polis utayaona ya magereza kusimika bendera za sisiem dodoma nzima tena saa7 mchana kweupeee!

Nasubiri siku watanzania wenye mapenzi mema na nchi yao watakaposimika za CHADEMA halafu usiku watumwe vibaraka wa watawala kwenda kuzishusha, KUTAKUWA NA PARAPANDA NYINGI SANA ASUBUHI
 
Back
Top Bottom