The Phylosopher
JF-Expert Member
- Mar 11, 2015
- 1,494
- 2,040
Kwa mtazamo wangu naona kuna tatizo kubwa kati ya waalimu cwt na serikali.
Ninachoelewa mimi ni kwamba cwt ni chama cha waalimu Tanzania, yaani chama cha kutetea maslahi waalimu.
Cwt haifanyi hiyo kazi kabisa. Wapowapo tu. Waalimu wa nchi hii wanaonewa na kunyonywa na kudharauliwa na kila awamu ya utawala.
Kulikuwa na jitihada za wadau za kuanzisha chama kingine cha waalimu likini kimepigwa vita Hadi kimeuliwa. Waalimu waliojifanya kujiunga kwenye chama kipya wamepigwa bit hadi wamenywe.
Ukiachilia mbali kuacha kuwatetea waalimu chama hiki kinawakata waalimu hela nyingi sana ambazo hata haijulikani zinafanya kazi gani. Ingekuwa hakuna mkono wa serikali walahi cag angeenda kukagua pale angekuta mauzauza mengi sana.
Kila mwanachama anakatwa 2% ukichukua idadi ya waalimu ambayo inakaribia laki 7 ukakata hizo asilimia unapata hela ndefu sana.
Ukiwasikiliza waalimu wana malalamiko na manung'uniko ambayo hakuna mtu sahihi wa kuubana serikali kwa niaba yao.
Waalimu ndio kundi kubwa sana la waajiriwa katika serikali ambalo linanufaika kidogo sana na keki ya nchi hii.
Yaani kazi ngumu mshahara mdogo hakuna posho kero kibao wakati wao ni wawezeshaji wa taaluma zote hii sio sawa hata kidogo.
Naomba waalimu tujitambue tuanzishe chama cha kutetea sio chama cha kutulainisha na kutuibia hela.
Ninachoelewa mimi ni kwamba cwt ni chama cha waalimu Tanzania, yaani chama cha kutetea maslahi waalimu.
Cwt haifanyi hiyo kazi kabisa. Wapowapo tu. Waalimu wa nchi hii wanaonewa na kunyonywa na kudharauliwa na kila awamu ya utawala.
Kulikuwa na jitihada za wadau za kuanzisha chama kingine cha waalimu likini kimepigwa vita Hadi kimeuliwa. Waalimu waliojifanya kujiunga kwenye chama kipya wamepigwa bit hadi wamenywe.
Ukiachilia mbali kuacha kuwatetea waalimu chama hiki kinawakata waalimu hela nyingi sana ambazo hata haijulikani zinafanya kazi gani. Ingekuwa hakuna mkono wa serikali walahi cag angeenda kukagua pale angekuta mauzauza mengi sana.
Kila mwanachama anakatwa 2% ukichukua idadi ya waalimu ambayo inakaribia laki 7 ukakata hizo asilimia unapata hela ndefu sana.
Ukiwasikiliza waalimu wana malalamiko na manung'uniko ambayo hakuna mtu sahihi wa kuubana serikali kwa niaba yao.
Waalimu ndio kundi kubwa sana la waajiriwa katika serikali ambalo linanufaika kidogo sana na keki ya nchi hii.
Yaani kazi ngumu mshahara mdogo hakuna posho kero kibao wakati wao ni wawezeshaji wa taaluma zote hii sio sawa hata kidogo.
Naomba waalimu tujitambue tuanzishe chama cha kutetea sio chama cha kutulainisha na kutuibia hela.