Nani abadilike mie au mume wangu? Reply

IP

New Member
Oct 7, 2009
2
0
Mimi ndimi mke anayelalamikiwa katika thread iliyotolewa mapema leo.
Nimelazimika kutoa maoni yangu kwa PI, baada ya mume wngu kuniambia kusoma comments za watu kuhusu maisha yetu.
Kwanza kuna mengi ambayo hakusema hapa lakini ametoa kipande tu cha maongezi ya juzi siku mbili na si tano kama anavyosema.
Ni kweli tulikutana wakati nikiwa na miaka 22 wakati huo aliniona niko katika wakati akanioa kwa kunipa sifa kem kem jinsi nilivyo wa kisasa na mrembo. Tumeishi miaka 11 na sijui hizo 13 anahesabu za uchumba pia au vipi. Nimezaa watoto wazuri na kila mmoja ana sifa yake nzuri. Tatizo hili la kubadilika nadhani Mme wangu haelewi mabadiliko. Kwa nini mabadiliko yaonekane kuwa kuvaa suruali (ambayo huwa navaa anyway) ionekane kuwa ni mabadiliko ya maendeleo? Nani kawadanganya? kama amewaona wanaovaa suruali huko anawataka aseme na asidanganye umma kuwa ni mambo ya kisasa. Mbona hata huyo Michelle ambaye anamsema anavaa sketi? sijawahi kuona ubaya huo. Kama swala ni la elimu. Alinioa nikiwa na elimu ya kidato cha sita kipindi kile tena PCB! Yeye alikuwa na degree moja. tatizo, alipoondoka kwenda US alikaa huko miaka 3 aliporudi ndo akaanza 1) mimi mnene nipungue 2) Nitembee kama so and so. 3) Nipende show fulani fulani TV, zote nimejaribu kwa kuendana na anayotaka lakini hayo hasemi. Tatizo ni hili la kubadili mwendo, nasema hapo no way.
Elimu nimejiendeleza nina diploma nzuri tu na kazi ninayo ya kuweza kubadili mwelekeo wowote. Lugha ipo kisawasawa anachotaka aseme ni mabadiliko gani siyo kula pweza hapa.
Yeye sasa ni mtu mzima asitake namimi niwe na PhD ndo aone nimebadilika. Yeye ni mhadhiri na PhD ni lazima kwake mie kazi yangu haiitaji PhD. Mabadiliko hayo yana malengo mengine na siyo kama anavyo sema. Yeye analazimika kuandaa publications ili kazi isimame anataka na mie niandike papers! NO WAY.
Mume wangu nakupenda tu hivyo ulivyo. Nitakusaidia ubadilike.
Note: I was not an idler that's why I am not a begger!
Nilitegemea mawazo yaliyo ya kujenga zaidi kutoka kwa huyu msomi kuliko haya. labda mawazo ya kupembua na hao anaoshauriwa yatamsaidia, lakini think before you take an action.
IP
progress.gif
 
We kweli kiboko. Umejiunga leo leo na umeshajua mmeo kakuua jamvini. Tumekustukia kamchezo kako. Wewe ndio yule yule unatuchezea shere. (Kwa kukufurahisha tu) Wewe ndio mshamba, tumemshauri mmeo akamate kifaa kingine ajirushe nacho. Japokuwa aliyeandika ile kutuomba ushauri ndio wewe mwenyewe uliyoandika thread hii. Hahahahaha! Kalaghabaho.
 
Kwanini usingejibu kulekule? kuanzisha thread mpya ni kuharibu mtiririko wa michango ...Hukatazwi kumjibu kule au unaogopa mkong'oto nyumbani kuwa umemjibu mume kwenye kadamnasi.Wewe mjibu kule akikukong'ota lete malalamiko hapa utapewa mbinu za kujibu mapigo.
Mods pls do the needful.
 
We kweli kiboko. Umejiunga leo leo na umeshajua mmeo kakuua jamvini. Tumekustukia kamchezo kako. Wewe ndio yule yule unatuchezea shere. (Kwa kukufurahisha tu) Wewe ndio mshamba, tumemshauri mmeo akamate kifaa kingine ajirushe nacho. Japokuwa aliyeandika ile kutuomba ushauri ndio wewe mwenyewe uliyoandika thread hii. Hahahahaha! Kalaghabaho.

Kaka unaua vibaya ha ha ha ha!!
 
Kwanini usingejibu kulekule? kuanzisha thread mpya ni kuharibu mtiririko wa michango ...Hukatazwi kumjibu kule au unaogopa mkong'oto nyumbani kuwa umemjibu mume kwenye kadamnasi.Wewe mjibu kule akikukong'ota lete malalamiko hapa utapewa mbinu za kujibu mapigo.
Mods pls do the needful.
Kweli bana sijui kwa nn kaanzisha hii? maana mara ya kwanza mi nimsoma kwenye ile thread ya kwanza then sijui nn kimemkuta kaaweka tena as individual thread....watu tunataka mtiririko bana!
 
Kwanini usingejibu kulekule? kuanzisha thread mpya ni kuharibu mtiririko wa michango ...Hukatazwi kumjibu kule au unaogopa mkong'oto nyumbani kuwa umemjibu mume kwenye kadamnasi.Wewe mjibu kule akikukong'ota lete malalamiko hapa utapewa mbinu za kujibu mapigo.
Mods pls do the needful.


Huyu ni msanii mmoja anaekumbwa na mafrustrations ya maisha, huenda yuko divorced, sasa anatafuta jinsi ya kumrudia huyo aliemtoroka, na inakuwa shida kidogo.

Jana tulikushauri tukijua una shida ya kikweli, kumbe unaleta saundi za mwaka 47 hapa!

Sort out your life man, kama ni ulevi uache, usitupime sie hapa...hatudanganyiki!
 
halafu uandishi wako mzee do! sijui kama ulisoma lugha primary/sec.
 
Huyu ni msanii mmoja anaekumbwa na mafrustrations ya maisha, huenda yuko divorced, sasa anatafuta jinsi ya kumrudia huyo aliemtoroka, na inakuwa shida kidogo.

Jana tulikushauri tukijua una shida ya kikweli, kumbe unaleta saundi za mwaka 47 hapa!

Sort out your life man, kama ni ulevi uache, usitupime sie hapa...hatudanganyiki!

Please bring back my shoes PakaJimmy, umevivaa unakumbuka. Hujanirudishia.
Umevaa viatu vyangu. Kule nimekugongea thanks na nyingine nakupea kwa hapa; thanks
 
Please bring back my shoes PakaJimmy, umevivaa unakumbuka. Hujanirudishia.
Umevaa viatu vyangu. Kule nimekugongea thanks na nyingine nakupea kwa hapa; thanks


Nakupa hizi viatu pamoja na soksi kabisa! Kiatu yenyewe mzee huku Arusha tunaita MASENDEU! Unajua ile kiatu ya tairi ya gari? ndo hiyo! ..Lol!
 
Nakupa hizi viatu pamoja na soksi kabisa! Kiatu yenyewe mzee huku Arusha tunaita MASENDEU! Unajua ile kiatu ya tairi ya gari? ndo hiyo! ..Lol!

Nayafahamu mkuu. Nimekaa Ar miaka mitatu, nilikuwa nashughulikia trupa kama sina akili nzuri. Vipi, bado zipo? Manake na kabaridi ka hapo, afu ukashindilia na kakonyagi inakuwa balaa.
 
Nayafahamu mkuu. Nimekaa Ar miaka mitatu, nilikuwa nashughulikia trupa kama sina akili nzuri. Vipi, bado zipo? Manake na kabaridi ka hapo, afu ukashindilia na kakonyagi inakuwa balaa.


Haha..haaaa!

We kweli umekaa huku...Kwa sasa huku ndo balaa hasa kama unapenda mambo ya `chomaz` na `maudirinki! Kuna visehemu vipya viingi kibao!

Watu wa huku mzee wanaingia bar, na gari yake nje anaiacha iko silence muda wote, eti nayo inakunywa, na inam`keep company!

Sijui ni mahela ya ufisadi...!!!
 
Haha..haaaa!

We kweli umekaa huku...Kwa sasa huku ndo balaa hasa kama unapenda mambo ya `chomaz` na `maudirinki! Kuna visehemu vipya viingi kibao!

Watu wa huku mzee wanaingia bar, na gari yake nje anaiacha iko silence muda wote, eti nayo inakunywa, na inam`keep company!

Sijui ni mahela ya ufisadi...!!!

Hahahaha! Mkuu umenikumbusha ya wana Apollo wa Mererani. Nakumbuka tulishafungiwa pale Mrina Bar,(sijui bado ipo?) tukaambiwa tunywe mpaka bia zote ziishe. Nilizigida nikachemka nikatoroka.
 
If this is true, i am off. hapa bado uyu Chrispin siku mkewe atakapokuja hapa na akajua ni yeye.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom