Mimi ndimi mke anayelalamikiwa katika thread iliyotolewa mapema leo.
Nimelazimika kutoa maoni yangu kwa PI, baada ya mume wngu kuniambia kusoma comments za watu kuhusu maisha yetu.
Kwanza kuna mengi ambayo hakusema hapa lakini ametoa kipande tu cha maongezi ya juzi siku mbili na si tano kama anavyosema.
Ni kweli tulikutana wakati nikiwa na miaka 22 wakati huo aliniona niko katika wakati akanioa kwa kunipa sifa kem kem jinsi nilivyo wa kisasa na mrembo. Tumeishi miaka 11 na sijui hizo 13 anahesabu za uchumba pia au vipi. Nimezaa watoto wazuri na kila mmoja ana sifa yake nzuri. Tatizo hili la kubadilika nadhani Mme wangu haelewi mabadiliko. Kwa nini mabadiliko yaonekane kuwa kuvaa suruali (ambayo huwa navaa anyway) ionekane kuwa ni mabadiliko ya maendeleo? Nani kawadanganya? kama amewaona wanaovaa suruali huko anawataka aseme na asidanganye umma kuwa ni mambo ya kisasa. Mbona hata huyo Michelle ambaye anamsema anavaa sketi? sijawahi kuona ubaya huo. Kama swala ni la elimu. Alinioa nikiwa na elimu ya kidato cha sita kipindi kile tena PCB! Yeye alikuwa na degree moja. tatizo, alipoondoka kwenda US alikaa huko miaka 3 aliporudi ndo akaanza 1) mimi mnene nipungue 2) Nitembee kama so and so. 3) Nipende show fulani fulani TV, zote nimejaribu kwa kuendana na anayotaka lakini hayo hasemi. Tatizo ni hili la kubadili mwendo, nasema hapo no way.
Elimu nimejiendeleza nina diploma nzuri tu na kazi ninayo ya kuweza kubadili mwelekeo wowote. Lugha ipo kisawasawa anachotaka aseme ni mabadiliko gani siyo kula pweza hapa.
Yeye sasa ni mtu mzima asitake namimi niwe na PhD ndo aone nimebadilika. Yeye ni mhadhiri na PhD ni lazima kwake mie kazi yangu haiitaji PhD. Mabadiliko hayo yana malengo mengine na siyo kama anavyo sema. Yeye analazimika kuandaa publications ili kazi isimame anataka na mie niandike papers! NO WAY.
Mume wangu nakupenda tu hivyo ulivyo. Nitakusaidia ubadilike.
Note: I was not an idler that's why I am not a begger!
Nilitegemea mawazo yaliyo ya kujenga zaidi kutoka kwa huyu msomi kuliko haya. labda mawazo ya kupembua na hao anaoshauriwa yatamsaidia, lakini think before you take an action.
IP
Nimelazimika kutoa maoni yangu kwa PI, baada ya mume wngu kuniambia kusoma comments za watu kuhusu maisha yetu.
Kwanza kuna mengi ambayo hakusema hapa lakini ametoa kipande tu cha maongezi ya juzi siku mbili na si tano kama anavyosema.
Ni kweli tulikutana wakati nikiwa na miaka 22 wakati huo aliniona niko katika wakati akanioa kwa kunipa sifa kem kem jinsi nilivyo wa kisasa na mrembo. Tumeishi miaka 11 na sijui hizo 13 anahesabu za uchumba pia au vipi. Nimezaa watoto wazuri na kila mmoja ana sifa yake nzuri. Tatizo hili la kubadilika nadhani Mme wangu haelewi mabadiliko. Kwa nini mabadiliko yaonekane kuwa kuvaa suruali (ambayo huwa navaa anyway) ionekane kuwa ni mabadiliko ya maendeleo? Nani kawadanganya? kama amewaona wanaovaa suruali huko anawataka aseme na asidanganye umma kuwa ni mambo ya kisasa. Mbona hata huyo Michelle ambaye anamsema anavaa sketi? sijawahi kuona ubaya huo. Kama swala ni la elimu. Alinioa nikiwa na elimu ya kidato cha sita kipindi kile tena PCB! Yeye alikuwa na degree moja. tatizo, alipoondoka kwenda US alikaa huko miaka 3 aliporudi ndo akaanza 1) mimi mnene nipungue 2) Nitembee kama so and so. 3) Nipende show fulani fulani TV, zote nimejaribu kwa kuendana na anayotaka lakini hayo hasemi. Tatizo ni hili la kubadili mwendo, nasema hapo no way.
Elimu nimejiendeleza nina diploma nzuri tu na kazi ninayo ya kuweza kubadili mwelekeo wowote. Lugha ipo kisawasawa anachotaka aseme ni mabadiliko gani siyo kula pweza hapa.
Yeye sasa ni mtu mzima asitake namimi niwe na PhD ndo aone nimebadilika. Yeye ni mhadhiri na PhD ni lazima kwake mie kazi yangu haiitaji PhD. Mabadiliko hayo yana malengo mengine na siyo kama anavyo sema. Yeye analazimika kuandaa publications ili kazi isimame anataka na mie niandike papers! NO WAY.
Mume wangu nakupenda tu hivyo ulivyo. Nitakusaidia ubadilike.
Note: I was not an idler that's why I am not a begger!
Nilitegemea mawazo yaliyo ya kujenga zaidi kutoka kwa huyu msomi kuliko haya. labda mawazo ya kupembua na hao anaoshauriwa yatamsaidia, lakini think before you take an action.
IP