Namtafuta dada yangu toka nchini Uganda

KIBURUDISHO

JF-Expert Member
Mar 28, 2011
1,002
274
Tafadhali sana naombeni msaada wenu wa jinsi gani au nifanyeje namtafuta dada yangu anaitwa
Ghati Josephati Magoiga,sijawahi onana nae tuliambiwa na baba kuwa tuna dada yetu anaishi Nchini Uganda alizaliwa mnamo mwaka 1982 nyumbani kwao alipozaliwa panaitwa Bujiku.Sikuweza kusikia

Mimi ila niliambiwa mwaka 2007 aliwahi kutoa taarifa redio free africa kuwa anamtafuta baba yake ambaye ambaye anaitwa Josephat Magoiga alikuwa mwanajeshi toka Tanzania alishiriki vita ya kumng'oa Iddi Amini ambaye hajawahi kumuona maana aliondoka Uganda tokea kipindi cha vita vya Kagera

Mama yake aliachwa akiwa na ujauzito wake na alipozaliwa tu mwaka 1982 mama yake alimtumia baba barua ya kumtaka ampatie jina la kumuita mtoto huyo aliyezaliwa na baba aliijibu barua kwa kumtumia jina kuwa aitwe Ghati Josephati tokea hapo walipotezana mawasiliano hadi hivi sasa, tokea alipotoa taarifa ile mwaka 2007 kupitia RFA kuwa anamtafuta baba yake.

Alijitambulisha kuwa anafanya kazi kwenye ubalozi wa Sweden nchini Uganda.Kwa bahati mbaya mimi binafsi sikuipata taarifa hiyo redioni ila niliambiwa na baba ambaye nae aliambiwa kuwa anatafutwa. Sasa sijui hata
nianzie wapi naombeni mwongozo wenu.
 
Tafadhali sana naombeni msaada wenu wa
jinsi gani au nifanyeje
namtafuta dada yangu anaitwa
Ghati Josephati Magoiga,sijawahi onana nae
tuliambiwa na baba kuwa tuna
dada yetu anaishi Nchini Uganda alizaliwa
mnamo mwaka 1982 nyumbani kwao
alipozaliwa panaitwa Bujiku.Sikuweza kusikia
mimi ila niliambiwa mwaka 2007
aliwahi kutoa taarifa redio free africa kuwa
anamtafuta baba yake ambaye ambaye
anaitwa Josephat Magoiga alikuwa
mwanajeshi toka Tanzania alishiriki vita ya
kumng'oa Iddi Amini ambaye
hajawahi kumuona maana aliondoka
Uganda tokea kipindi cha vita vya Kagera
mama mama
yake aliachwa akiwa na
ujauzito wake na alipozaliwa tu mwaka 1982
mama yake alimtumia baba barua
ya kumtaka ampatie jina la kumuita mtoto
huyo
aliyezaliwa na baba aliijibu
barua kwa kumtumia jina kuwa aitwe Ghati
Josephati tokea hapo walipotezana
mawasiliano hadi hivi sasa,tokea alipotoa
taarifa ile mwaka 2007 kupitia RFA kuwa
anamtafuta baba yake.
alijitambulisha kuwa anafanya kazi kwenye
ubalozi wa Sweden nchini Uganda.Kwa bahati
mbaya mimi binafsi sikuipata taarifa hiyo
redioni ila niliambiwa na baba ambaye nae
aliambiwa kuwa anatafutwa.Sasa sijui hata
nianzie wapi naombeni mwongozo wenu.

Mbona majawabu unayo! safiri nenda uganda ,ubalozi wa sweden uganda. google jina lake umaweza kumpata ktk mitandao ya kijamii, nenda katika mji aliozaliwa, ulizia at random primary sekondary,college,varsity,church au nenda katoe tangazo EATV.
 
Halo ni rahisi sana now a days kumpata mutu hasa kwenye hii developed world,Anza hivi tafuta pesa kidogo halafu safiri mpaka uganda chukua detail ulizonazo anzia pale ambapo baba yako anasema walikuwepo ukifika hapo bandika picha na vipeperushi,

Mbili nenda Radio free Africa kwenye Library yao anaweza kuwa aliacha details

Tatu hapa pia kuna ubalozi wa Sweden pale Umoja House ukiendpalewatakusadia kwa sababu hizi balozi ni lazima kuna database ya wafanyakazi kwenye wizara yao ya mambo ya nje.
 
Halo ni rahisi sana now a days kumpata mutu hasa kwenye hii developed world,Anza hivi tafuta pesa kidogo halafu safiri mpaka uganda chukua detail ulizonazo anzia pale ambapo baba yako anasema walikuwepo ukifika hapo bandika picha na vipeperushi,

Mbili nenda Radio free Africa kwenye Library yao anaweza kuwa aliacha details

Tatu hapa pia kuna ubalozi wa Sweden pale Umoja House ukiendpalewatakusadia kwa sababu hizi balozi ni lazima kuna database ya wafanyakazi kwenye wizara yao ya mambo ya nje.

Mkuu asante kwa ushauri wako,hasa kuhusu kwenda Rfa kuulizia kama aliacha detail zake nashukuru.
 
Mbona majawabu unayo! safiri nenda uganda ,ubalozi wa sweden uganda. google jina lake umaweza kumpata ktk mitandao ya kijamii, nenda katika mji aliozaliwa, ulizia at random primary sekondary,college,varsity,church au nenda katoe tangazo EATV.

Hofu yangu mkuu ni jina hasa analotumia yawezakuwa hili alilolitoa baba halitumii sana.
 
Hofu yangu mkuu ni jina hasa analotumia yawezakuwa hili alilolitoa baba halitumii sana.
Fine ,wewe unchotakiwa kufanya ni kuweka mazingira yeye to find you! toa details zote za baba yako kwenye possible places anazoweza kupatikana huyo bint na kama mzee yuko hai basi amtaje huyo mama yenu wa kambo then omba mungu! all the best ,hope you guys be reunited with your loooong lost sister-damu nzito.......!
 
TAHADHARI Uganda sasa hivi wako juu sana hasa kwa Utekaji nyara na Utapeli wa hali ya juu,kuna jamaa yangu yeye alikuwa anamtafuta Rafiki yake kwa njia ya Magazeti ya huko Uganda (Newvision)katokea jamaa kasema yeye anamfahamu hivyo akapewa taarifa za huyo jamaa yake ikiwa pamoja na namba ya simu,Jamaa yangu akaamua kumpigia simu wakaongea lakini jamaa kamwambia afanye jitihada aende Kampala wiki hiyo maana alikuwa na safari ya kwenda Ulaya jamaa kasafiri kafika Kampala na kukutana na jamaa aliyemwambia ampeleke kwa jamaa yake hapo Nakasero.

Baada ya kumfikisha sehemu ambayo yeye mwenyewe haijui aliingizwa kwenye chumba ambacho ndani yake kuna chumba tena hakuna Dirisha umeme upo na Mlango ukafungwa walitokea Mabounsa wawili wakamwambia atoe kila kitu chake walikuwa wanatafuta pesa tu naye alikuwa na shs Million moja ya TZ Walichukua hiyo pesa baada ya siku mbili walimpakia kwenye usiku wakampeleka nje ya mjii hali akiwa amefungwa kitambaa machoni wakamtelekeza huko wao wakaondoka.

Alihangaika sana kupata nauli ya kurudi nyumbani alitembea kwa mguu siku tatu akifuata barabara ya kutoka Kampala kwenda Mtukula mwisho alienda Kanisani kuomba msaada ndipo walimsaidia.hivyo CHukua tahadhali sana sana maana Dunia ya leo si salama sana,BE AWARE ALL THE TIME.
 
iliwai mtokea rafik yangu alitangaza hivo hivo kuna mtu akajitokeza harafu akasema yeye ata anafanya biashara ya kwenda china kuleta laptop.camera.yule rafik akafurah kampata kaka yake tena ni mfanyabiashara mkubwa. mara jamaa akamuaid kumletea kontena la laptops. sasa akajifanya kumuagizia dereva apeleke bukoba. na wakawa wanawasiliana na dereva kila mahali anapofikia. yule dereva kufika kahama akasema ameshikwa na trafic wanataka laki saba. na akapewa aongee na hao trafic. na trafic wakakomaa hio ela. uyo rafik yangu ikabid akope ela kwa waalimu wenzake akamtumia. ile amemtumia namba ikawa mteja aipatikan. jamaa kumpigia na uyo ndugu yake aliyempata alipotangaza kwa radio naye akawa apatikan. so jamaa akawa katapeliwa hio ni baada ya kutangaza kwa radio kumtafuta kaka ake na tapel likajitokeza na kumpigia simu.
 
Back
Top Bottom