Namsikiliza Katibu Mkuu wa chama kipya WAPO RADIO

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
anasema watu wa cuf wanaoshiriki kwenye umoja wa kitaifa zanzibar ni watu 8 tu. anasema ni mawaziri 7 na seif. Rakini ngazi za chini , masheha, wakuu wa wilaya ,mikoa hamna mtu wa cuf hata mmoja.
 
Anasema; watu cuf wanaiita ccm b lakini hakuna kiongozi alnayepinga hilo. hiyo iliniudhi sana. lakini baada ya kutafakari na kuona tabia zinaanza kufanana na ccm b nikaamua kutoka peke yangu kama mimi, nikaenda kwenye vyombo vya habari na Miraji said abdallah ambaye aliniunga mkono. kwa kuwa sisi ndo tulio baini udhaifu wa cuf. naamini hata wengine waking'amua watatoka.
 
anasema: mimi sijashawishiwa na mtu. ukizingatia mimi sikua na cheo chochote cuf japo nilikuwa na uwezo wa kukabidhiwa majukumu.
 
anasema: chama chetu hakitakua kama ccj. ccj hakikia na msingi, hakikua na watu wanao waunga mkono. sisi hatutakuwa na wadhamini 250 bali zaidi ya 2000 kwa kila mkoa. msajili aandae fomu.
 
anasema: sisi hatufungamani na hamadi rashid. hamad rashid bado yupo cuf ambacho sisi tunaona ni kichafu kwa hiyo na yeye ni mchafu kwa kuwa bado yupo cuf mbunge wa wawi. lakini kama atataka kujiunga na sisi tunamkaribisha na wananchi wote kwa ujumla.
 
mheshimiwa Rimbo anaendelea kusema;
wakati tunaanza mfomo wa vyama vya siasa tulitaka tuchukue dola ya zanzibar na bara. baadae tukaona kama cuf tuanze kwanza kuichukua zanzibar halafu ndo tuje kuichukua cuf. so huu ndo ulikuwa wakati wa katibu mkuu wa cuf kuanza kuimalisha cuf baada ya uchaguzi lakini hata igunga hakukanyaga.
 
anasema watu wa cuf wanaoshiriki kwenye umoja wa kitaifa zanzibar ni watu 8 tu. anasema ni mawaziri 7 na seif. Rakini ngazi za chini , masheha, wakuu wa wilaya ,mikoa hamna mtu wa cuf hata mmoja.
alaa...hii serikali wazanzibari wanayotamba nayo kuwa ya umoja wa kitaifa kumbe ina watu nane tu kutoka CUF?
 
anasema sisi tulitaka tuitwae zanzibar halafu tuje bara. lakini seif hakufanya hivyo. lakini hamad alipo anza kupiga kelele ndo seif akaanza kufanya ziara bara.
 
anasema; chama cha ADC kinaenda kuiondoa ccm madarakani kama watanzania watatuunga mkono sababu vyama vilivyopo vyote wameshapoteza mwelekeo. tuache kung'ang'ania vitu vyetu ambavyo hata havifai.
 
mwenyekiti wa mda wa chama ni Miraj said.
 
anasema sisi tulitaka tuitwae zanzibar halafu tuje bara. lakini seif hakufanya hivyo. lakini hamad alipo anza kupiga kelele ndo seif akaanza kufanya ziara bara.

Inapendeza kuona Tanzania kuna watu wenye uthubutu mkubwa hivi, hawa cuf wamejiua wenyewe kwa ubinafsi wao. Big up Mhe. Said Miraji (mwenyekiti - ADC) na Lucas Limbu (katibu mkuu - ADC) kwa ushupavu na ukomavu wenu wa kisiasa mliotuonyesha.
 
anasema; miraj ndiye aliyekuwa meneja kampeni wa ripumba kwa tanzania, yeye ndo alikuwa anasemea cuf, alikuwa mkurugenzi wa blue guard tanzania. Miraj aliamua kupumzika mwenyewe nafasi ya ulinzi cuf baada ya kuona amepuuzwa cuf bila kujari cuf inapokea ruzuku zaidi ya mil250 akaenda kukaanga chips pale buguruni na hii tunaiongea hadharani. na aliwaandikia barua viongozi kwamba huu utaratibu tunao enda nao sio. akaamua kujishusha. fikiri kutoka ukurugenzi wa taifa hadi kuwa mkaanga chips ni uungwana.
 
....hamad rashid bado yupo cuf ambacho sisi tunaona ni kichafu kwa hiyo na yeye ni mchafu kwa kuwa bado yupo cuf mbunge wa wawi.
hahahahaha... for all we know, yeye bado ni Mbunge wa Wawi, na huwi Mbunge bila chama, and the last time we checked your party was CUF! I agree.
 
wakuu anaye ongea ni katibu mkuu rimbu sio mwenyekiti miraj.samahani kwa hilo. mod naomba ubadilishe heading iwe katibu mkuu sio mwenyekiti.
 
katibu anaendelea kusema: nia ya miraj ilikuwa kumtetea mtanzania sio kujitajilisha ndo maana kaacha mshahara kaenda kutengeneza chips. sasa baada ya kuona chama kinaporomoka ikabidi tutafute mbadala wa chama kama kimbilio.
Prof.ripumba kama anakosa ni kosa la udhaifu wa kuto wakemea hawa watendaji lakini ripumba hana matatizo.
 
huoni cuf wanatafunwa na damu ya ubaguzi ya kuwabagua wakristo? mpigaji simu kasema.
anajibu: Tumeanzisha chama hiki kwa nia njema ya kuwatetea watanzania na kuwaunganisha kwa nia ya dhati.
 
katibu anaendelea kusema: nia ya miraj ilikuwa kumtetea mtanzania sio kujitajilisha ndo maana kaacha mshahara kaenda kutengeneza chips. sasa baada ya kuona chama kinaporomoka ikabidi tutafute mbadala wa chama kama kimbilio.
Prof.ripumba kama anakosa ni kosa la udhaifu wa kuto wakemea hawa watendaji lakini ripumba hana matatizo.
Siyo kwamba chips zilikuwa hazilipi?
 
rimbu nilikuambia cuf inakufa kipindi cha nyuma ukaniambia nimetumwa na chadema. kitakacho iondoa ccm kwenye madaraka sio kuanzisha chama kipya bali kujenga ustahimilifu na uvumilivu kwenye chama. watanzania wameshachoka vyama vya siasa. je unasemaje kwa hilo? mpiga simu kauliza na simu ikakatika(ni salvatory kapiga simu).
; katibu kakubali kweli salvatory alimtabilia cuf imekufa. tatizo la cuf hawataki kukosolewa. 2007 ndo mala ya mwisho cuf kufanya uchaguzi ndani ya chama lakini wamesogeza hadi 2014.
 
anasema haya ndo hamad rashid wakamfukuza.
 
wamemuuliza kwanini wasijiunge na dp kwa mtikila kumuunga mkono katika kupigania haki zetu?
anajibu: ni utumwa kujiunga na chama cha mtu. je tanzania ni chama gani kisicho chama cha mtu? vyama vyote ni vya watu sisi tunataka tuanzishe chama cha watanzania.
 
Back
Top Bottom