Namshukuru mungu sikusoma UDSM

Nancy Tweed

Senior Member
Nov 22, 2010
123
3
kwa kuangalia haraka haraka tuu, kama watu wengi wa humu ndiyo wamesoma udsm, kweli kazi ipo huko nyumbani.
 
kwa kuangalia haraka haraka tuu, kama watu wengi wa humu ndiyo wamesoma udsm, kweli kazi ipo huko nyumbani.

Unaweza kuwa specific Dada Nancy ?

UDSM pamechoka, tulishawahi kuchambua maandishi kutoka tovuti yao hata mtoto anayeenda hizi English Medium schools na kurudi nyumbani kufuatilia CNN kwa makini hawezi kuandika vile.

Lakini still, madai yako umeyatoa kirejareja mno kupita bila kuulizwa ujieleze zaidi.
 
Huu Uzi Unahusiana Vipi na kuwa kwenye Jukwaa la siasa.
Wewe ulisoma wapi unayetaka ku politicise kilakitu ?
 
kwa kuangalia haraka haraka tuu, kama watu wengi wa humu ndiyo wamesoma udsm, kweli kazi ipo huko nyumbani.

Unataka wawe kama hawa?

Tamko La Wasomi Wa Vyuo Vikuu Dodoma Kuhusu Kitendo Cha Wabunge Wa Chadema Kutoka Nje Ya Ukumbi Wa Bunge Wakati Wa Hotuba Ya JK.

Sisi vijana wasomi wa vyuo vikuu mbalimbali vilivyoko mkoa wa Dodoma kwa pamoja tunapenda kuweka wazi maoni yetu juu ya kitendo kilichofanywa na Wabunge wa CHADEMA wakati Mhe. Rais alihutubia Bunge.

Kwanza tumeshtushwa na kitendo hicho na kuweka wazi masikitiko yetu kwa kuwa kilichofanyika ni kinyume na matarajio ya wapiga kura waliowachagua waheshimiwa wabunge hao kuwawakilisha ndani ya chombo hicho kikubwa na chenye heshima kubwa ndani na nje ya nchi.

Bunge ni sehemu ya kuwakilisha wananchi kwa hoja chini ya kanuni zilizopo bila kujali itikadi ya chama chochote cha siasa na kazi kubwa ya mbunge ni kuishauri na kuisimamia Serikali kwa niaba ya wananchi waliomchagua au kuwachagua.

Kwa mantiki hiyo basi kama Wabunge hawamtambui Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maana yake hawana kazi ya kufanya ndani ya Bunge kwani kazi yao kubwa ni kuishauri na kuisimania Serikali sasa kama hawaitambui Serikali hiyo hawana sababu ya kuendelea kuwepo Bungeni.

Pili Baada ya uchaguzi wa Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda, wabunge hao pia walinukuliwa na vyombo vya habari na ushaidi tunao wakiweka wazi kumkubali kiongozi huyo, na kauli mbiu yake ya ‘Bunge moja' je, kitendo walichofanya inaashiria utekelezaji wa kauli mbiu ya Bunge moja?

Tatu msimamo wa kutomtambua Rais ni wa CHADEMA kama chama na waliotoka nje ya Bunge ni wabunge sasa ni vema wabune hao watambue na kutafakari upya kama kweli wanawawakilisha Bungeni wananchi au cha na kutekeleza misimamo yao bila kujali maslahi ya waliowachagua na kumpa kura nyingi Rais Kikwete?.

Nne Kwa badhi ya wabunge wa CHADEMA kutomtambua Rais wakati akilihutubia bunge ni wazi kuwa hata sheria zitakzopitishwa na Bunge hawatahusika kwa kuwa mwenye mamlaka ya mwisho kukubali sheria iliyotungwa na Bunge itumike ni Rais ambaye wanadai hawamtutambui.



Ni dhahiri kuwa watashindwa kufanya kazi yao ya uwakilishi na usimamizi wa Serikali Bungeni .

Je wanawaonesha watanzania dalili gani kama si kutaka kuleta machafuko nchini na mgawanyiko ndani ya Bunge na kwa Jamii kwa ujumla?.

Wananchi waliowachagua wabunge hao wanapaswa kutafakari upya wawakilishi waliowachagua kama wana uelewa wa kutosha kuhusu bunge, sisi vijana wa vyuo vikuu tunajua na tunatambua kuwa Rais ni Sehemu ya Bunge na Bunge haliwezi kukamilika bila Rais na hii ndio maana kila sheria inayopitishwa na Bunge ni lazima yeye Rais aweke sahihi yake.

Katika mazungumo yake na waandishi wa habari wiki hii Mweneykiti wa CHADEMA MHE. Freeman Mbowe, alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wabunge wake na madiwani wanaweza kuendelea kuwakilisha wananchi licha ya kutomtambua Rais.

Sisi tunasema hili si sahihi bali ni upotoshaji mkubwa, kamwe mtoto hawezi kudai kuwa hamtabui Baba yake kisha anaendelea kumwita Baba na kutumia kila kitu kinachotolewa na Baba huyo huyo. Huo ni utovu wa nidhamu au kukosa maadili.

Sisi vijana wa vyuo vikuu Mkoa wa Dodoma tunawaomba Watanzania wote wenye nia njema na Taifa letu kuwapuuza wabunge wa CHADEMA na kutambua kuwa lengo lao ni kutaka kutuhamisha kutoka kwenye ajenda ya msingi ya Maendeleo na kubaki kwenye malumbano ya kisiasa kama tulivyoshuhudia katika nchi jirani.

Kamwe tusikubali kudanganywa na watu wachache.

Mwisho tungependa kuwaomba Wabunge wa CHADEMA wawaombe radhi watanzania kwa kuvuruga tashwira safi ya Bunge letu lisilo na ubaguzi na itikadi za kisiasa vinginevyo wanawadharau watanzania waliowachagua wakidhani kwamba niwaadilifu wa Taifa na si cha chama chao.

Tutambue kuwa kazi kubwa ya CHADEMA na Wabunge wake kwa sasa ni kuwachanganya watanzania ili badala ya kuendelea na shughuli za ujenzi wa taifa wabaki na malumbano ya hapa na pale kwa manufaa yao binafsi.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Bunge letu na kutuepusha na ubaguzi kama huu uliofanywa na baadhi ya Wabunge wa CHADEMA.

Aksanteni sana.

IMESOMWA NA THOBIAS MWESIGA RICHARD
KWA NIABA YA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU MKOA WA DODOM
 
Unaweza kuwa specific Dada Nancy ?

UDSM pamechoka, tulishawahi kuchambua maandishi kutoka tovuti yao hata mtoto anayeenda hizi English Medium schools na kurudi nyumbani kufuatilia CNN kwa makini hawezi kuandika vile.

Lakini still, madai yako umeyatoa kirejareja mno kupita bila kuulizwa ujieleze zaidi.

Mkuu Kiranga mi nafikiri kama ni suala taaluma, Professionalism siyo suala la UDSM tu ni suala la kitaifa. Kushuka kwa ubora wa elimu, kukosa mipango endelevu katika nyanja mbalimbali za elimu na mambo kama hayo. Isitoshe muundo mzima wa elimu hapa nchini ni tatizo toka shule za awali mpaka vyuo vikuu hili mi nafikiri ndio tatizo kubwa.
 
kwa kuangalia haraka haraka tuu, kama watu wengi wa humu ndiyo wamesoma udsm, kweli kazi ipo huko nyumbani.


Nancy ,

Tofauti yako wewe na yule aliyesoma UDSM ni nini? Kwanza sentensi yako uliyoandika hapo juu inaonyesha dhahiri ya kuwa hujui unachoongea. Umeanza kuandika bila ya kufuata sheria zozote za uandishi sanifu; unaandika Mungu bila ya kuanza na herufi kubwa, UDSM unaandika kwa herufi ndogo yaani ni vichekesho tuu. Mikato unaiweka tuu ovyo ovyo bila ya kufuata mtitiriko. Mimi nakushauri ndungu yangu kama huko nje ya nchi basi rudi shule kwani sentensi yako hapo juu speaks volume about your level of understanding.
 
kwa kuangalia haraka haraka tuu, kama watu wengi wa humu ndiyo wamesoma udsm, kweli kazi ipo huko nyumbani.

namshukuru sana mungu nimesoma udsm....dada huwezi kuijua udsm na impact yake kwa wahitimu wake kama hukusoma pale hata ujadili hapa mpaka mtondogoo..kalagha bhao!
 
Nancy, first post unaanza na UDSM, ok tell us where have you studied..? baba yako ana chuo? halafu nidhamu yako is too low, in general unawadhalilisha wote waliopo na waliomaliza UD, unatoka DOM no dought, this shows u have babish, kiddish, childish mind, kama umefika chuo nitashangaa, don't expose ur ignorance here, best way kuficha ujinga wako keep quite, nikwambie hivi, ungesoma UD usingekuwa na ubongo unaotamka haya madudu, u join JF kusema haya?
 
namshukuru sana mungu nimesoma udsm....dada huwezi kuijua udsm na impact yake kwa wahitimu wake kama hukusoma pale hata ujadili hapa mpaka mtondogoo..kalagha bhao!

ur... Rite mupe meno yake huyoo..... Asijeshindwa kutafuna! Mupe maneno yake asijeshindwa kububunya..... UDSM= Hekima ni Uhuru.
 
Mkuu Kiranga mi nafikiri kama ni suala taaluma, Professionalism siyo suala la UDSM tu ni suala la kitaifa. Kushuka kwa ubora wa elimu, kukosa mipango endelevu katika nyanja mbalimbali za elimu na mambo kama hayo. Isitoshe muundo mzima wa elimu hapa nchini ni tatizo toka shule za awali mpaka vyuo vikuu hili mi nafikiri ndio tatizo kubwa.

Right,

But that doesn't change the fact that UDSM is lagging horribly.

UDSM used to be the pinnacle of education in Tanzania and even the region, now it is a ghost of it's former self. So the decline in educational standards is amply demonstrated by the declining standards at and products of UDSM.

The folly of free - or near free- education is that it can work as long as that "tragedy of the commons" effect doesn't kick in, once the novelty of university education expired, we found ourselves overtaxing the same resources mindlessly and expecting a quality education, hardly realistic.

I am watching the advent of private universities with a keen eye, perhaps they will rise to the occassion and rescue our sinking ship.

I can already envision some lamenting that the private universities could be even worse and I am in a stupor of wishful thinking.
 
Hivi umefika hata hapo UDSM penyewe hivi karibuni? Yaani pamechoka utadhani pametelekezwa.....

Nyani Ngabu...UDSM pamechoka kwa majengo? Kama hoja yako ni majengo sidhani kama ni tija kama wanachuo wanapata taaluma iliyowapeleka chuoni.
"Miafrika Ndivyo Tulivyo-by Nyani Ngabu"
 
Nyani Ngabu...UDSM pamechoka kwa majengo? Kama hoja yako ni majengo sidhani kama ni tija kama wanachuo wanapata taaluma iliyowapeleka chuoni.
"Miafrika Ndivyo Tulivyo-by Nyani Ngabu"

Ndugu, UDSM pamechoka kiujumla! Yaani kuanzia mazingira, majengo, vifaa na nyenzo za kufundishia hadi ubora wa elimu itolewayo hapo. Majengo hawayafanyii ukarabati. Vyumba vya madarasa, ofisi za walimu, mabweni ya wanafunzi, na majengo mengine ya chuo hicho yamechakaa vibaya sana. Kwa hadhi yake chuo hicho kilitakiwa kiwe na mazingira mazuri kwa ujumla. Sasa kama mazingira ni mabovu hivyo kweli unategemea hata elimu itolewayo hapo itakuwa bora kweli?

Haya tuje kwenye vifaa na nyenzo za kufundishia. Hivi kuna computer labs ngapi hapo UDSM? Maktaba yenyewe ipo ipo tu. Na mtu ukitaka kufanya inter-library loan kwa vitabu ambavyo hawana sijui unaenda wapi? Tumaini? Chuo hakina hata 'lounges' za kusomea. Unakuta wanafunzi wamekaa pale chini ya ule mti wanaouita 'mdigrii' wakisoma. Hapo chini ya mti mtu inabidi uwe na concentration ya hali ya juu la sivyo utaishia kuwa distracted tu.

Angalia hata tovuti yao. Yaani ovyo ovyo tu. Makosa kibao ya kisarufi na tahajia. Kwa kweli uhodari wa wahitimu wengi wa UDSM siku hizi umeshuka sana. Binafsi sivutiwi kabisa na mazao ya hapo. Kama wewe unaona elimu itolewayo hapo ni bora na mazao yake ni bora basi mimi na wewe tuna viwango tofauti!!!
 
Chuo kikuu cha Dsm kuna viongozi wapo pale kwa matumbo yao na sio kwa maendeleo ya chuo au taifa.kila head wa Idara anapambana jinsi ya kuiba,mfano huyu mkuu wa Computer centre ni mwizi na nyangau aliegeuza kitengo muhimu ktk maendeleo ya njii hii kuwa kama banda lake la mama ntilie,amejaza ndugu zake na watoto wake,
Kuna Mradi wa Smart Card.mradi huu kutokana na njaa za watu wachache,mradi huu pia upo kapuni,mivutano kila kona.
Ukija Muhimbili-mfukuto wa MOI kujitenga na Muhimbili wawe Independent kila kukicha ndio unaongezeka.hii ndio Tanzania
 
Nancy ,

Tofauti yako wewe na yule aliyesoma UDSM ni nini? Kwanza sentensi yako uliyoandika hapo juu inaonyesha dhahiri ya kuwa hujui unachoongea. Umeanza kuandika bila ya kufuata sheria zozote za uandishi sanifu; unaandika Mungu bila ya kuanza na herufi kubwa, UDSM unaandika kwa herufi ndogo yaani ni vichekesho tuu. Mikato unaiweka tuu ovyo ovyo bila ya kufuata mtitiriko. Mimi nakushauri ndungu yangu kama huko nje ya nchi basi rudi shule kwani sentensi yako hapo juu speaks volume about your level of understanding.

Wala herufi kubwa hazijui
 
Back
Top Bottom