Napenda haki,ila haki bila wajibu sio sahihi!! aidha ukitaka uheshimiwe lazima ujiheshimu. kwa muda sasa nimeanza kumuelewa Rais Jakaya Kikwete kuwa ni mtu Mstahimilivu na muungwana ambaye nimeshuhudia mara nyingi akichelea kutoa maamuzi ili kudhihirisha Umakini wake! Kwa tabia ya waafrika hasa viongozi wa kiafrika sio wengi wenye staha, wengi huamua maamuzi ya kidikteta na kufedhehesha.
Kauli ya Rais aliyoitoa jana kupitia vyombo vya habari ninaiunga mkono kwa asilimia mia, sitaki kuamini kuwa serikali hii inauwezo huo wa kulipa Daktari waliyemsomesha bure milioni tatu na nusu, haiwezekani!!
Kauli ya Rais niya uwazi na ukweli!! Anayeona mshahara wa lakitisa ni mdogo aende popote akaajiriwe, huo sio ushauri mbaya.! Tatizo lililopo ni kuwa madaktari wengi ni watoto wa vigogo maana inaeleweka wazi kuwa shule zinazofundisha masomo ya sayasi na zenye ufaulu mzuri ni zile za kulipia ambazo watoto wa shule za kata hawawezi kuwa madaktari. Kwa mantiki hii, hakuna haja ya kusumbuana, Hospitali za Binafsi zipo nyingi, kilichopo hao wanaodhani mshahara ni mdogo waende tu kwa amani, kuliko kuwachochea madaktari wenye moyo na kazi kugoma na kuumiza wagonjwa.
Kama madaktari wanadhani taaluma yao ni bora sana, basi waende wakajitafutie sehemu stahiki. Stop migomo, vivyo hivyo kwa walimu, kama wanadhani kazi ya ualimuhailipi hakuna haja ya kusumbua serikali shule za binafsi zipo nyingi japo usalama wa kazi ni mdogo dawa si kugoma dawa ni kuondoka!!!!
Kauli ya Rais aliyoitoa jana kupitia vyombo vya habari ninaiunga mkono kwa asilimia mia, sitaki kuamini kuwa serikali hii inauwezo huo wa kulipa Daktari waliyemsomesha bure milioni tatu na nusu, haiwezekani!!
Kauli ya Rais niya uwazi na ukweli!! Anayeona mshahara wa lakitisa ni mdogo aende popote akaajiriwe, huo sio ushauri mbaya.! Tatizo lililopo ni kuwa madaktari wengi ni watoto wa vigogo maana inaeleweka wazi kuwa shule zinazofundisha masomo ya sayasi na zenye ufaulu mzuri ni zile za kulipia ambazo watoto wa shule za kata hawawezi kuwa madaktari. Kwa mantiki hii, hakuna haja ya kusumbuana, Hospitali za Binafsi zipo nyingi, kilichopo hao wanaodhani mshahara ni mdogo waende tu kwa amani, kuliko kuwachochea madaktari wenye moyo na kazi kugoma na kuumiza wagonjwa.
Kama madaktari wanadhani taaluma yao ni bora sana, basi waende wakajitafutie sehemu stahiki. Stop migomo, vivyo hivyo kwa walimu, kama wanadhani kazi ya ualimuhailipi hakuna haja ya kusumbua serikali shule za binafsi zipo nyingi japo usalama wa kazi ni mdogo dawa si kugoma dawa ni kuondoka!!!!