Shehullohi
JF-Expert Member
- Jul 21, 2020
- 3,754
- 3,675
Hayo ni mambo ceremonial tu. Marais wote wamepewa uchifu huo ceremonial, lakini Tanzania haitambui uchifu wala cheo kama hicho cha kurithi. Kwa sababu Tanzania kimsingi bado ni Jamhuri inayoamini katika usawa wa watu, na ukikubali uchifu umekubali kwamba kuna koo fulani zimefaa kutawala nyingine.
Kwa hiyo ule utaratibu uliotumika kumtawaza/simika haukuhusisha ibada za matambiko na makafara ya mizimu? Unaposema ceremonial unamaanisha nini? Huyu chifu kwa utaratibu ule hakufanyiwa ibada ya mizimu, kuvishwa kaniki na ngosi ya chui? Kwenye ulimwengu wa kiroho upande wa kiza limefanyika jambo kubwa sana. Uislamu na Ukristo sijui unatuambia mambo yapi juu ya utaratibu huu.