Nampenda lakini sina namna

punditt

Senior Member
Feb 19, 2019
112
49
habari za mda huu wadau wa jf# namini mko poa . bilia ya kupoteza wakati acha niende ky mada moja kwa moja.

Hakika katika hii dunia ya sayari ya tatu hakuna kitu kizuri kama kuwa na furaha maana unaweza ukawa na pesa,cheo, umarufu . n.k lakini ukakosa kitu kinachoitwa furaha. Hutakuwa na amani katika maisha yako .na furaha huja pale unapopata mtu ,rafiki ,mchumba sahihi wa kuwa nae.

Nimeanza mahusiano na mchumba wangu takribani miaka mitatu (3) mpka sasa bado naendlea nae, ingawa kunachangamoto za hapa na pale cz sisi ni binadamu kukosea huwa hakukwepeki.

Nampenda sn mpenzi wangu kwani anaonesha kunijali,kunifariji pale napokuwa na tatzo, pia ni mwanamke ambae ana sifa za kipekee sn tofaut na wengine cz ,ni mkweli, hana makundi ya watu ,ni mwepesi wa kusamehe ,mvumilivu na pia yapo mengi ambayo ananitendea mpka moyo wangu umejidhihilishia kuwa awe ndo mkewngu wa kufunga nae pingu za maisha .

Lakini Kitu ambacho kimekuwa changamoto ky mahusiano yetu ni utofauti wa dini, yeye ni muslam na mm ni mkristu, .mpka ss nashindwa nifanyaje maana nimejitahidi kumshawishi aje kwenye upande wa dini yangu bado hayuko tayari " na mm pia siko tyr kubadili dini . Asa shida inakuja nampenda sna sitaki nimkose katika maisha yangu,.

*Naombeni ushauri wenu wadau bila kuweka itikadi za kidini ,
asanteni namini maoni yenu ni msaada mkubwa sn kwangu#


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njia rahisi ni ile watayosema uende huko huko kwa mwenye huo mzigo. Full stop mwisho wa malumbano!
 
habari za mda huu wadau wa jf# namini mko poa . bilia ya kupoteza wakati acha niende ky mada moja kwa moja.

Hakika katika hii dunia ya sayari ya tatu hakuna kitu kizuri kama kuwa na furaha maana unaweza ukawa na pesa,cheo, umarufu . n.k lakini ukakosa kitu kinachoitwa furaha. Hutakuwa na amani katika maisha yako .na furaha huja pale unapopata mtu ,rafiki ,mchumba sahihi wa kuwa nae.

Nimeanza mahusiano na mchumba wangu takribani miaka mitatu (3) mpka sasa bado naendlea nae, ingawa kunachangamoto za hapa na pale cz sisi ni binadamu kukosea huwa hakukwepeki.

Nampenda sn mpenzi wangu kwani anaonesha kunijali,kunifariji pale napokuwa na tatzo, pia ni mwanamke ambae ana sifa za kipekee sn tofaut na wengine cz ,ni mkweli, hana makundi ya watu ,ni mwepesi wa kusamehe ,mvumilivu na pia yapo mengi ambayo ananitendea mpka moyo wangu umejidhihilishia kuwa awe ndo mkewngu wa kufunga nae pingu za maisha .

Lakini Kitu ambacho kimekuwa changamoto ky mahusiano yetu ni utofauti wa dini, yeye ni muslam na mm ni mkristu, .mpka ss nashindwa nifanyaje maana nimejitahidi kumshawishi aje kwenye upande wa dini yangu bado hayuko tayari " na mm pia siko tyr kubadili dini . Asa shida inakuja nampenda sna sitaki nimkose katika maisha yangu,.

*Naombeni ushauri wenu wadau bila kuweka itikadi za kidini ,
asanteni namini maoni yenu ni msaada mkubwa sn kwangu#


Sent using Jamii Forums mobile app
Mpe mimba mengine mtahadili baadae akishazaliwa mtoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwanza kabisa huyo ni girlfriend na sio mchumba, nazani maana ya uchumba huijui, uchumba ni pale mnapotambulishana kwa wazazi na mahari kutolewa ndo unakuwa uchumba. Pili, kuna ndoa ya serikalini kila mtu anabaki na dini yake, au hiyo hamuijui? na mwisho, kama kila mmoja wenu hayuko tayari kufata dini ya mwenzie, na kufunga ndoa serikalini hamtaki, basi kuliko kuendelea kupotezeana muda ni heri kila mmoja aendelee na maisha yake aangalie kwingine, tena especially kwa huyo binti, time is ticking asije kumbuka shuka kumekucha, if u real love her then let her go or fata dini yake umuoe. Last but not least, hiyo ky veeepe?
 
Ayayayayayayayaaa....wacha tu nikae kimya make udini si mzuri..



Cc Smart911

Sent using Jamii Forums mobile app
Udini ni mzuri sana ukitumika vizuri.
Kuwahimiza watu waache zinaa kwa kufuata mafundisho ya dini huu ni udini mzuri.

Kuwahimiza watu waache kuuwana kwa sababu djni inakataza huu ni udini.

Kuhimiza watu waowane kwa sababu sheria ya dini imeruhusu huu ni udini.

Basi hata kukataza muislamu kuolewa na asiyekuwa muislamu pia udini huo uheshimiwe.

Wanawake wasiokuwa waislamu wako wengi sana,kipi hasa mtu anahangaika nacho kumtaka huyo muislamu mmoja ambaye nyuma yake wapo wasiokuwa waislamu wengi sana mkuu.

Tatizo linakuja kwa wazazi na ndugu na hata mwenyewe binti hawako tayari,atasema walazimishe waowane wakati wazazi hawajaridhia na hapo hakuna raha ya ndoa.

Kama anayekataa kubadili ili aolewe ni mdini basi hata anayekataa kubadili dini ili aowe naye ni mdini pia,wala isigandamizwe kwa upande mmoja tu.

Kama ambavyo mtu anajiuliza kwamba kwani uislamu una nini hasa mpaka mtu akatae kubadili dini ili aolewe basi ndivyo hivyo nayeye anajiuliza kwamba ukristo una nini hasa mpaka mtu akatae kubadili dini ili aowe?

Kama ambavyo yeye anampenda huyo binti lakini hataki kubadili dini yake kumfata mke basi inawezekana na huyo mwanamke anampenda huyo mwanaume lakini hataki kubadili dini yake.wote wako sawa.

Ukiona mtu anakataa kufanya jambo fulani kwa kigezo cha dini basi jua hilo jambo anataka kulitekeleza kwa sababu ya dini.

Ukiona mtu anakataa kuolewa kwa sababu muoaji sio dini yake basi jua fika huyo muolewaji anataka kuolewa kwa sababu ya dini yake.

Ukiona mtu anakataa kula nguruwe kwa sababu ya ya dini yake basi jua huyo mtu anakula kwakufuata dini yake inamuamrisha ale nini.

Ukioana mtu anakataa kuvaa kimini kwa sababu ya dini yake basi jua mtu huyo anavaa kwa kufuata dini yake imesemaje.

Muhimu tuangalie kwa nini kila mmoja hataki kubadili dini

Je ukristo umekataza mtu kubadili dini?

Je uislamu umekataza mtu kubadili dini?
 
mkuu pole sana ila unapaswa kukaa chini wewe ka wewe uone kupoteza na kupata kupi kuliko kwepesi, pili ukiona mnaweza funga ndoa ya serikali inafaa waweza fanya hivyo. pia na kinyume chake naamini umenielewa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom