Kama wingi wa wabunge ndio kitu cha maana CDM wangeacha yale makapi yaendelee kukaa bungeni. Fikiri kwanini CDM imewafyeka fyeka,nguvu ya CDM sio wabunge ni UMMA.Habari wakuu
Hapo jana nilipoyaona majina ya wabunge wa CHADEMA waliokuwa wamegomea vikao vya bunge kutolewa na spika akiwataka wakapimwe covid19 ndio waruhusiwe kurudi tena bungeni nilishtuka na kustaajabu kidogo kwa namba ya wabunge wa chama hiki kuwa kwa uchache kipindi hiki
itakumbukwa baada ya uchaguzi wa 2015 chadema kilikuwa na zaidi ya wabunge 60 ndani ya bunge la jamhuri lenye viti zaidi ya 390
hii namba kwa muda wa miaka minne tu imeporoka sio kushuka kwa kasi kasi kubwa
kwa chama kilicho na nia ya kushika dola ilitakiwa kiwe kinajiimarisha sasa kuelekea uchaguzi mkuu hapo October na sio kupukutishwa kwa kupungzwa namba ya wabunge wake
kwa muono wangu hili ni anguko kubwa lazima tukubali chadema kuna sehemu kinafeli na hii ni ishara kwamba chama hiki kinakufa taratibu kama si haraka