Namna ya kuokoa CHADEMA isife...

Habari wakuu

Hapo jana nilipoyaona majina ya wabunge wa CHADEMA waliokuwa wamegomea vikao vya bunge kutolewa na spika akiwataka wakapimwe covid19 ndio waruhusiwe kurudi tena bungeni nilishtuka na kustaajabu kidogo kwa namba ya wabunge wa chama hiki kuwa kwa uchache kipindi hiki

itakumbukwa baada ya uchaguzi wa 2015 chadema kilikuwa na zaidi ya wabunge 60 ndani ya bunge la jamhuri lenye viti zaidi ya 390

hii namba kwa muda wa miaka minne tu imeporoka sio kushuka kwa kasi kasi kubwa
kwa chama kilicho na nia ya kushika dola ilitakiwa kiwe kinajiimarisha sasa kuelekea uchaguzi mkuu hapo October na sio kupukutishwa kwa kupungzwa namba ya wabunge wake

kwa muono wangu hili ni anguko kubwa lazima tukubali chadema kuna sehemu kinafeli na hii ni ishara kwamba chama hiki kinakufa taratibu kama si haraka
Kama wingi wa wabunge ndio kitu cha maana CDM wangeacha yale makapi yaendelee kukaa bungeni. Fikiri kwanini CDM imewafyeka fyeka,nguvu ya CDM sio wabunge ni UMMA.
 
Ni wazi kunahitajika 'maamuzi magumu' ndani ya CDM ili kuiokoa CDM isife katika mapito inayopitia kipindi hiki...!! Kadiri muda unavyotaradadi ndivyo inaonekana dhahiri pumzi zinazidi kukata..! Nini kifanyike ? Toa ushauri wa dhati hapa..!
 
Njia ni moja tu,mbowe na genge lake waachie ngazi chama kishikwe na watu wasafi.Siyo watu walewale tu miaka nenda rudi wapiga pesa tu.
 
NAMNA YA KUOKOA CHADEMA ISIFE
Hakika chama kikuu cha upinzani kinaugua na kiko ICU. Kime ”paralaizi”.
Sio jambo la kufurahisha hata kidogo. Ni msiba wa taifa. Taifa linahitaji upinzani imara na ulio makini ili liweze kusonga mbele. Bahati mbaya sana uongozi wa CHADEMA haswa mwenyekiti wake anaonekana kukata tamaa na kuishiwa mikakati.

Ukisikiliza kauli zake sasa ni za mtu aliyeamua kumwachia mungu! Mkiti wa chama kikuu cha upinzani hapaswi kutoa kauli anazotoa Mbowe hivi sasa. Kauli za “anayetaka kuondoka na aondoke” ni za mtu aliyeshindwa!

Kwa kuwa tupo wengine tunaotaka kuona upinzani ukiimarika ni wajibu wetu kumsaidia Mbowe. Japo kachelewa sana Mbowe kama kiongozi mkuu anapaswa kufanya yafuatayo:

1. Kuitisha mkutano mkuu wa dharura ili kujadili hatma ya chama.
2. Kusitisha mara moja utaratibu wa wabunge kuchangia chama kila mwezi
3. Kutayarisha taarifa yakinifu ya mapato na matumizi ya chama na kuisambaza kwa wanachama na viongozi.
4. Kuvunja mara moja kamati isiyo rasmi. Kamati inayotuhumiwa kuendesha chama kinyemela.
5. Kuacha mara moja tabia ya kutoa maamuzi binafsi kwenye masuala mazito.
6. Kutayarisha mara moja sera za chama kuhusu kilimo, maji, elimu, etc
7. Kutangaza kuwa hatagombea tena kiti kwenye uchaguzi ujao wa chama
8. Kuhakikisha kila mgombea wa chama anahudumiwa bila ubaguzi
9. Kuweka wazi kuwa 2020 nafasi ya mgombea uraisi kwa tiketi ya CDM iko wazi yeyote anaweza kugombea na hatamuunga yeyote mkono.
10. Kutumia ruzuku kujenga ofisi za chama
11. Awaagize viongozi wake waache mara moja kupinga na kukosoa juhudi za serikali ambazo zinawanufaisha wapiga kura.

Haya ndio haswa matatizo yanayofanya viongozi waikimbie CHADEMA na wananchi waidharau CHADEMA.
Ikiwa hatazingatia basi ategemee muda si mrefu kukimbiwa hadi na wajumbe wa Baraza Kuu na Kamati Kuu.
Nawasilisha
CCM ndio inakiua CHADEMA kwa msaada wa Serikali
 
I
NAMNA YA KUOKOA CHADEMA ISIFE
Hakika chama kikuu cha upinzani kinaugua na kiko ICU. Kime ”paralaizi”.
Sio jambo la kufurahisha hata kidogo. Ni msiba wa taifa. Taifa linahitaji upinzani imara na ulio makini ili liweze kusonga mbele. Bahati mbaya sana uongozi wa CHADEMA haswa mwenyekiti wake anaonekana kukata tamaa na kuishiwa mikakati.

Ukisikiliza kauli zake sasa ni za mtu aliyeamua kumwachia mungu! Mkiti wa chama kikuu cha upinzani hapaswi kutoa kauli anazotoa Mbowe hivi sasa. Kauli za “anayetaka kuondoka na aondoke” ni za mtu aliyeshindwa!

Kwa kuwa tupo wengine tunaotaka kuona upinzani ukiimarika ni wajibu wetu kumsaidia Mbowe. Japo kachelewa sana Mbowe kama kiongozi mkuu anapaswa kufanya yafuatayo:

1. Kuitisha mkutano mkuu wa dharura ili kujadili hatma ya chama.
2. Kusitisha mara moja utaratibu wa wabunge kuchangia chama kila mwezi
3. Kutayarisha taarifa yakinifu ya mapato na matumizi ya chama na kuisambaza kwa wanachama na viongozi.
4. Kuvunja mara moja kamati isiyo rasmi. Kamati inayotuhumiwa kuendesha chama kinyemela.
5. Kuacha mara moja tabia ya kutoa maamuzi binafsi kwenye masuala mazito.
6. Kutayarisha mara moja sera za chama kuhusu kilimo, maji, elimu, etc
7. Kutangaza kuwa hatagombea tena kiti kwenye uchaguzi ujao wa chama
8. Kuhakikisha kila mgombea wa chama anahudumiwa bila ubaguzi
9. Kuweka wazi kuwa 2020 nafasi ya mgombea uraisi kwa tiketi ya CDM iko wazi yeyote anaweza kugombea na hatamuunga yeyote mkono.
10. Kutumia ruzuku kujenga ofisi za chama
11. Awaagize viongozi wake waache mara moja kupinga na kukosoa juhudi za serikali ambazo zinawanufaisha wapiga kura.

Haya ndio haswa matatizo yanayofanya viongozi waikimbie CHADEMA na wananchi waidharau CHADEMA.
Ikiwa hatazingatia basi ategemee muda si mrefu kukimbiwa hadi na wajumbe wa Baraza Kuu na Kamati Kuu.
Nawasilisha
Ili CHADEMA isife SERIKALI iache kuipendelea CCM
 
Kitendo cha kumfukuza Zitto, Dr Slaa na mkaamua kumkaribisha fisadi Lowasa nilijua tu Chadema Kharas
Waarabu wanasema
بالإيمان كل شيء ممكن
Ngoja tusubiri tuone kama itawezekana
 
Hakuna democrasia kila mwaka mwenyekiti yule yule na atakae taka cheo hicho ndio msaliti wa chama ataundiwa zengwe mmm nawaona wazalendo zamu yao kushika kijiti cha chadema
 
NAMNA YA KUOKOA CHADEMA ISIFE
Hakika chama kikuu cha upinzani kinaugua na kiko ICU. Kime ”paralaizi”.
Sio jambo la kufurahisha hata kidogo. Ni msiba wa taifa. Taifa linahitaji upinzani imara na ulio makini ili liweze kusonga mbele. Bahati mbaya sana uongozi wa CHADEMA haswa mwenyekiti wake anaonekana kukata tamaa na kuishiwa mikakati.

Ukisikiliza kauli zake sasa ni za mtu aliyeamua kumwachia mungu! Mkiti wa chama kikuu cha upinzani hapaswi kutoa kauli anazotoa Mbowe hivi sasa. Kauli za “anayetaka kuondoka na aondoke” ni za mtu aliyeshindwa!

Kwa kuwa tupo wengine tunaotaka kuona upinzani ukiimarika ni wajibu wetu kumsaidia Mbowe. Japo kachelewa sana Mbowe kama kiongozi mkuu anapaswa kufanya yafuatayo:

1. Kuitisha mkutano mkuu wa dharura ili kujadili hatma ya chama.
2. Kusitisha mara moja utaratibu wa wabunge kuchangia chama kila mwezi
3. Kutayarisha taarifa yakinifu ya mapato na matumizi ya chama na kuisambaza kwa wanachama na viongozi.
4. Kuvunja mara moja kamati isiyo rasmi. Kamati inayotuhumiwa kuendesha chama kinyemela.
5. Kuacha mara moja tabia ya kutoa maamuzi binafsi kwenye masuala mazito.
6. Kutayarisha mara moja sera za chama kuhusu kilimo, maji, elimu, etc
7. Kutangaza kuwa hatagombea tena kiti kwenye uchaguzi ujao wa chama
8. Kuhakikisha kila mgombea wa chama anahudumiwa bila ubaguzi
9. Kuweka wazi kuwa 2020 nafasi ya mgombea uraisi kwa tiketi ya CDM iko wazi yeyote anaweza kugombea na hatamuunga yeyote mkono.
10. Kutumia ruzuku kujenga ofisi za chama
11. Awaagize viongozi wake waache mara moja kupinga na kukosoa juhudi za serikali ambazo zinawanufaisha wapiga kura.

Haya ndio haswa matatizo yanayofanya viongozi waikimbie CHADEMA na wananchi waidharau CHADEMA.
Ikiwa hatazingatia basi ategemee muda si mrefu kukimbiwa hadi na wajumbe wa Baraza Kuu na Kamati Kuu.
Nawasilisha
Mimi ushauri wangu wamwache tu. Chama si chake?
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom