Namna ya kukoleza nguo nyeusi iliyofifia

ngebo

JF-Expert Member
Sep 8, 2017
1,679
2,105
Hii ishu inatokea sana, unakuta una nguo yako pendwa sana ukiifulia sabuni ya unga tu rangi yake halisi inapotea na inakuwa na weusi uliofifia, mfano jeans nyeusi, au T-shirt nyeusi nk. Hivyo basi kwa wanaofahamu namna za kurudisha weusi kwenye nguo iliyofifia atupe mbinu, binafsi nafahamu ya kutumia black fabric dye, ila sasa sijafanikiwa kuipata kwenye mizunguko yangu, pia mwenye suggestion inapopatikana tujuze.

images%20(4).jpeg
 
Zipo supermarket wanauza nakumbuka kuna GF wangu mzungu alikuwa ananunua na tulikuwa tunaitumia,ila jina lake nimesahau kwakweli.
 
Well, kiuhalisia njia ninayotumia mimi na nayoijua ni kuchanganya kiasi fulani cha chumvi katika maji unayofulia nguo yako hiyo baada ya kuweka sabuni ya unga.

Na hii, inatumika kwa nguo zote zinazochujisha rangi yake halisi.
Nadhani nitakuwa nimesaidia kwa kiasi fulani.
 
Back
Top Bottom