Namna ya kuchangia faini ya Tsh. Milioni 350 waliyohukumiwa kulipa Viongozi wa CHADEMA

Yaani hiyo hela ilikuwa inatakiwa kupatikana ndani ya saa moja tu ili kudhihirisha Chadema imechokwa ni jinsi inavyohangaika kulimaliza hili suala

Pamoja na hamasa zote za kusumbua wananchi lakini hakuna mafanikia peoples power imepotea kabisa
Duuuuh sasa hawa kwa nini wanalia Lia hivyo? Wanahangaika kweli, tatizo mnatumia manguvu kwenye siasa ndio maaana mbafeli kwetu kule karagwe tulipokuwa tukihitaji mtu wa kulima ilikuwa tunawatafuta kabila Fulani hivi....

Tunawalipa hela wanafanya makazi magumu magumu maaana wanatabia ya kutumia nguvu kwa kila japo hawajui kutumia akiri, Wewe siasa ni sayansi, usipotumia sayansi utajikuta unamtukana marekani baada ya kumaliza kumtukana yeye anakuadhibu kwa kutumia sentesi tano kwenye twitter,

anakuacha ukihangaika kupanda ndege kuwasilisha maujumbe ya kuomba radhi, na ukifika kule unapokelewa na mpishi wa ikulu unabaki ukiwa umeambulia mapicha Picha tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maandamano -mfuatano au msururu wa watu wengi wanaotembea pamoja kuelekea mahali ili kutimiza lengo fulani. Tulizuiliwa kuandamana kwa kutembea ila tumeandamana moyoni, tumeandamana mifukoni ili kutimiza lengo na nawaomba pia tuandamane kwenda kupiga kura hapo Octoba ili tumchague kiongozi atakayekuja na sera za TANZANIA YA KIPATO tofauti na TANZANIA YA WANYONGE inayotunyonga kwa njaa na ukosefu wa ajira.

Hali inayoendelea kwa sasa ni ujumbe tosha kuwa mioyo ya watu inaandamana kila siku kupinga kile kinachowakera wananchi.

Huwezi kuuwa upinzani hata siku moja, upinzani upo moyoni.

Screenshot_20200311-114608.png
 
Watanzania laki moja wakitoa shilingi 1000 kila mmoja jumla ni 100000000 milioni 100.. Hapo inaonyesha bado upinzani ni mdogo sana
 
Back
Top Bottom