Nkandi
Member
- Nov 20, 2010
- 83
- 42
Katika maisha haya tunayoishi,niliwahi kuambiwa mafaniko ni matokeo ya utekelezaji wa mawazo na utumiaji wa fursa sahihi katika wakati sahihi,yaani kwa ki ulaya "money follows great ideas", katika kupitia magazeti ya 'kizungu' nikakutana na sentensi hii pia "The starting point of all achievement is desire. Weak desire brings weak results" yenye maana chanzo cha mafanikio ni ile hamu ya kufanikiwa,hamu hafifu uleta matokeo hafifu,yawezekana tafsiri yangu isiwe sawa ila kwa jinsi ilivyo hapa kwetu itakuwa imeeleweka
Kufanikiwa kibiashara katika ulimwengu wa sasa kuna maanisha uwepo wa wazo lenye kuleta suluhisho kwa wengine yaani falsafa ya tatizo lako kipato changu, uwepo wa wazo lenye kurahisisha kazi kwa wengine linaweza kukuhakikishia kukuwa kwa biashara yako kwakuwa kunahakikisha uwepo wa wateja wa uhakika
Uwezekano wa kuwapata wateja unafanya uhitaji wa biashara kusajiliwa kwenye mamlaka mbalimbali ilikuweza kuwa na 'uhai wa kisheria' hapa itategemeana na aina ya biashara ambayo mtu ameamua kuianzisha,uhai wa kisheria unatoa fursa biashara kuwa huru kutafuta fursa sehemu yoyote ile na hapa ndiyo hatua ya biashara inapoanza.
Kuanza kwa biashara hakumaanishi kufanikiwa katika soko husika; siri ya kufanikiwa katika soko ni kufahamu aina ya wateja unaowataka na uliowachagua,kufahamu upatikani wao na mahitaji yao;gharama ya wao kupata huduma,namna unavyoweza kuwahudumia tofauti na wafanyabiashara wengine,namna unavyoweza kuheshimu muda wao na jinsi unavyoweza kuwa 'flexible' katika huduma zako kulingana na aina ya mteja.
'Flexibility' inakuhakikishia wateja wa uhakika kwakuwa kila atakayekuja anajua tatizo lake litapata ufumbuzi.Jukumu la kuitangaza biashara linaweza kuwa dogo kwakuwa waliowahi kuwa wateja wako watakuwa mabalozi wazuri na kukutengnezea 'customer network' ambayo ni muhimu kuliko matangazo.
zipo namna nyingi za kufanikisha biashara, Kwa leo,naomba niishie hapa wanajamii.
maswali na majadiriano kkmarketing61@yahoo.com
Nawasilisha.
Kufanikiwa kibiashara katika ulimwengu wa sasa kuna maanisha uwepo wa wazo lenye kuleta suluhisho kwa wengine yaani falsafa ya tatizo lako kipato changu, uwepo wa wazo lenye kurahisisha kazi kwa wengine linaweza kukuhakikishia kukuwa kwa biashara yako kwakuwa kunahakikisha uwepo wa wateja wa uhakika
Uwezekano wa kuwapata wateja unafanya uhitaji wa biashara kusajiliwa kwenye mamlaka mbalimbali ilikuweza kuwa na 'uhai wa kisheria' hapa itategemeana na aina ya biashara ambayo mtu ameamua kuianzisha,uhai wa kisheria unatoa fursa biashara kuwa huru kutafuta fursa sehemu yoyote ile na hapa ndiyo hatua ya biashara inapoanza.
Kuanza kwa biashara hakumaanishi kufanikiwa katika soko husika; siri ya kufanikiwa katika soko ni kufahamu aina ya wateja unaowataka na uliowachagua,kufahamu upatikani wao na mahitaji yao;gharama ya wao kupata huduma,namna unavyoweza kuwahudumia tofauti na wafanyabiashara wengine,namna unavyoweza kuheshimu muda wao na jinsi unavyoweza kuwa 'flexible' katika huduma zako kulingana na aina ya mteja.
'Flexibility' inakuhakikishia wateja wa uhakika kwakuwa kila atakayekuja anajua tatizo lake litapata ufumbuzi.Jukumu la kuitangaza biashara linaweza kuwa dogo kwakuwa waliowahi kuwa wateja wako watakuwa mabalozi wazuri na kukutengnezea 'customer network' ambayo ni muhimu kuliko matangazo.
zipo namna nyingi za kufanikisha biashara, Kwa leo,naomba niishie hapa wanajamii.
maswali na majadiriano kkmarketing61@yahoo.com
Nawasilisha.