Namna Wazungu walivyotokea duniani

chofachogenda

Senior Member
Oct 6, 2016
104
190
SEHEMU 1: JINSI YA WAZUNGU WALIVYOTOKEA DUNIANI
Binadamu wa sasa alizaliwa Afrika na kutokana na mtu mweusi watu wa aina yote duniani walipatikana . Swali je ni kwa namna gani rangi tofauti za ngozi zao zilipatikana au maumbo tofauti ya sura hata nywele zao zilipatikana?

Ili ni swali ambalo bado halijibiki kwa urahisi lakini sayansi imefikia maendeleo mazuri katika kulijibu swali hili hasa chuo cha Havard ambacho kilijikita kwenye masomo ya jeni au vinasaba. Genetic studies of Havard University ambacho mwaka 2015 kilijikita katika uchunguzi wa mabaki wa binadamu wa sasa (modern human) katika ulaya ya kale.

KUTOKA TUMAI MPAKA OMO 1: KUZALIWA KWA BINADAMU
Kutokana na nadharia ya kisayansi, Dunia iliumbwa takribani miaka bilioni 13 iliyopita.Mpaka miaka milioni 65 iliyopitan kiumbe ambacho kilikuwa kinatawala dunia kilikuwa ni Dinosau ( Dinosaur).Ambapo kutoweka kwao kulitokana na gimba(asteroid) kugongana na hii sayari hivyo kuruhusu kutokea kwa wanyama wadogo

Miaka milioni 10 iliyopita, kiumbe (primates) kilimzaa sokwe kiumbe ambacho kinafanana na binadamu kwa mara ya kwanza katika historia.Hicho kiumbe kilikuwa kinaitwa Tumai na mabaki yake yalipatikana nchini Chad yakiwa na umri wa miaka miloni 7.

Tumai
1549716348754.png

Kutoka Tumai , kiumbe hicho kinachofanana na binadamu kiliendelea kubadilika taratibu ndani ya Afrika kupitia Homo erectus,Homo habilis, Homo naled,Homo rhodesiensis n.k. Mabaki ambayo yanapatikana Mashariki na kusini mwa Afrika.Baadhi ya hao ya binadamu wa mwanzo walisambaa katika mabara mengine lakini walitoweka kutokana na changamoto za kimazingira.

Takribani miaka 200,000 iliyopita , binadamu wa sasa (Homosapiens) alizaliwa akiwa na komwe, kidevu, ubongo na sifa nyingine sinazomtambulisha kama binadamu wa sasa. Hapa tunazungumza kuhusiana na Omo 1 ambaye mabaki yake yalipatikana Kibishi kusini mwa Ethiopia.Hao ndio walikuwa Waafrika wa kwanza wanaume kwa wanawake walioenda kuitwaa dunia.
1549716454405.png

WAAFRIKA WALITAWANYIKA DUNIA NZIMA
Miaka 100,000 iliyopita, Viumbe hawa kutoka Afrika walianza kwenda nje ya bara la Afrika kwa kuingia Palestina/Israel na Yemen. Huyu alikuwa binadamu wa kwanza kuikalia Asia yote. Kwa upande mwingine Afrika Magharibi waafrika wenye maumbo mafupi (Mbilikimo) walitumia mkondo bahari wa Antlantic kufika Brazil miaka 50,000 mpaka 65,000 iliyopita hivyo ndivyo walivyoingia Amerika ya kusini. Kutoka kusini –mashariki ya bara la Asia waafrika waliwasili Australia miaka 50,000 iliyopita na wakavijaza visiwa vya Pacific mpaka Hawaii. Na hatimae waliingia ulaya miaka 40,000 iliyopita na kufika nchi za skandinavia na Uingereza.

Hawa watu weusi kutoka Australia na Pacific waliungana Marekani . Watu weusi ambao waliwasili moja kwa moja kutoka Afrika kwa kiasi kikubwa waliijaza Marekani tangu mwanzo

Hivi ndivyo dunia nzima ilijazwa na watu weusi na kwa maelfu ya miaka kulikuwa na watu weusi tu dunia duniani kote .Swali je wazungu, waarabu na waasia walizaliwaje au walitokeaje?

KAZI MUHIMU YA VITAMIN D
Vitamin D ni element ambayo inawezesha mwili kufyonza calcium ambayo hutumika kutengeneza mifupa. Hata hivyo moja ya hatua muhimu katika utengenezaji wa vitamin D inahitaji miale ya jua.Kama kukiwa na jua la kutosha mwili hutengeneza vitamin D. Il kwa kuwa jua ni kali san Afrika linaweza kuleta madhara kwenye ngozi na kusababisha kansa, kwa hiyo mwili unatengeneza pigment zinazoitwa melanin ili kuilinda ngozi. Watu weusi ni weusi kwa sababu miili yao ilitengenezwa ili kuendana na jua la Afrika .

Melanini inaruhusu kiwango muhimu cha miale ya jua kupenya na kutengeneza vitamin D kwa ajili ya mifupa na wakati huohuo kuilinda ngozi dhidi ya jua kali .

Wakati mtu mweusi alipowasili ulaya magharibi alikutana na hali ya barafu. Kipindi hicho hata Uswisi ilikuwa barafu tupu. Hiyo zama ya barafu (Ice Age) ilikuwa ni miaka 130,000 iliyopita na kuisha miaka 10,000 iliyopita ilikuwa inaitwa wurm glaciation.Baridi lilikuwa kali mno na jua lilikuwa adimu katika mazingira hayo.

Melanin ilizuia hiyo miale kidogo ya jua kupenya kwenye ngozi na vitamin D ikawa inatengenezwa kwa kiwango kidogo sana .Kutokana na upungufu wa vitamin D uliosababishwa Melanin kulitokea ulemavu na vifo vya mapema (premature death).

Kutokana na tafiti iliyofanywa na Clemens TL na wengine mwaka 1982 na Carolina na Bolina na wengine mwaka 2014, inasema kwamba wazungu wanazalisha sana vitamin D Kuliko watu weusi wakiwekwa katika mwanga wa jua ulio sawa. Matokeo yake ili mwili uweze kusurvive na kuendana na mazingira ikabidi iondoe melanin hasa kwenye maeneo ambayo jua lilikuwa adimu………..itaendelea



Wako: Benjamins

Credit: AHHA (African History,Histoire Africaine)
 
Kwa hiyo mkuu unataka kutueleza kwamba ipo siku nasi tutatoweka vije viumbe vingine?
 
Bila shaka kadri muda unavyokwenda, hata sisi (wa aina yetu) tutatoweka watakuja wengine.
 
Kinacho nishangaza ni kwamba unakuta mtu kazaliwa mwaka 1900 au 1800 ananza kujifanya mtafiti anatunga mastory Ya uongo na Kweli kisha anakuja kukwambia mambo yaliyotokea miaka billion kadhaa iliyopita Kama syo kunyweshana chai na sukari guru ni nn.
 
Kinacho nishangaza ni kwamba unakuta mtu kazaliwa mwaka 1900 au 1800 ananza kujifanya mtafiti anatunga mastory Ya uongo na Kweli kisha anakuja kukwambia mambo yaliyotokea miaka billion kadhaa iliyopita Kama syo kunyweshana chai na sukari guru ni nn.

Ni tafiti zinafanyika kisayansi japokuwa hii ni nadharia lakini kidogo ina make sense kuliko ya nyoka anayeongea bustanini
 
Mtazunguka zunguka sana ,usiku na mchana..jua litachomoza na kuzama ila swali litabaki pale pale how Does melanin affects Intelligence ikiwa Black people bado tupo kwenye low Intelligence Continuum....??

Hakuna study iliyofanyika ya kucompare Melanin concentration kwenye blood in relation to Intelligence kwa binadamu....

Hakuna uhusiano wa melanin na uwezo wa kufikiri wa Intelligence ....


We can not relay kwenye concept moja ya kusema mtu mweusi ndo aliyeanza duniani huku idadi nyingi na Race nyeupe zikiwa dominant Inteingently.....

Kuna sababu kubwa lazima iwepo ambayo itafanya mlolongo huo uende sawa....

These whites know the reality ila huwa wanatufariji kwa kutulazimisha na sisi tuamini kuwa ni kweli sisi ndo wa kwanza...but they don't tell us the reality how the other Races emerged....

Or hawatuambii how do we benefit from being the first motherhood creature.....

So what ....?? umekuwa wa kwanza kuja then imekuwaje speciation from your original imekuovertake Intelligence....??

The difference in races we have ni statistical significance kwa mtu anayeitwa Mweusi na mweupe ....

If so , tulikuwa na kwanza kuwepo duniani and the other races originated from us...why do the changes not occuring at present....??


It's sometimes compelling the truth that tries to guess if creation of these different races are highly controlled by other supreme entity....


but...........

Ni kweli kuwa ngozi nyeusi ina melanin circulation kubwa kwenye damu but haimanishi kuwa ngozi nyeupe haina uwezo wa kuishi mazingira yoyote....tena wale ndo wameundergo a wide range of enveronmental diversity kuliko sisi...

Ni race gani inayofanya wide range ya enveronmental habitation kama sio ngozi nyeupe...!!......??

Kuna ngozi nyeusi imefanya wide range ya enveronmental habitation kuzidi ngozi nyeupe...!!.....??


Wao ndo watu wa kwanza kufanya survey ya kuja hata huku tulipo sisi....

It's none sense ku believe kuwa Africans migrated from African continent kwenda Asia an European continent harafu wafike kule washindwe kujua walitoka huku .....does this make sense at ol....???

Kwa hiyo ,how do their changes interms of skin colour zisiwafanye wajue wametoka Africa...?? kwamba walizaaana bila kutunza histori na kushindwa kurudi back kutoa feedback kwamba jamani eee twendeni huku ndo pazuri ngozi inabadilika rangi na mazingira ni mazuri ,lakini cha kushangaza walikaaa kimya wakiwaacha ndugu zao kwenye wimbi la ukimya .....None sense .....no compelling touch to taste the truth encoded....



Nitaendelea kushikilia msimamo wangu kuwa ,African race ina siri nyingi sasa ikihusisha na hizo white race na uwepo wake ni statistical significance kuendeleza uhai katika ulimwengu huu na kuna maelezo mengine muhimu ya kutueleza ukweli ila sio story za kubadilika kwa nyani.....

Hakuna sehemu imeonesha Dinossa walichange kuja kuwa mijusi...wakati mijusi ilikuwepo hata kipindi cha dinosa....!!


This is the very critical question to hurt our mind juu ya kwanini uwepo wetu na utofauti huu katika human race umekuwepo huku ukiwa na wide range ya utaofauti wa Intelligence...
 
JIBU SAHIHI BINADAMU WA KWANZA NA WANYAMA WA KWANZA DUNIANI WANAPATIKA AFRIKA KATIKA ENEO LA AFRIKA MASHARIKI TANZANIA BINADAMU HAWA WALIKUWA NI WANYAMA WALIBADILIKA KUTOKANA HALI YA HEWA YA KIPINDI HICHO MIAKA MILIONI 3 ILIYOPITA NAKUPATA UMBO TULIYONAYO SASA NA RANGI YAO ILIKUWA NYEUSI UTHIBITISHO WA HILI NI KUGUNDULIKA KWA FUVU LA KWANZA LA BINADAMU WA KALE N'GORO NGORO NA KUWEPO MBUGA ZA WANYAMA WENGI WA KILA HAINA KULIKO SEHEMU YOYOTE DUNIANI HII INATHIBITISHWA KUWEPO KWA DINOSAUR MJUSI MKUBWA NA ALIKUWA MNYAMA MKUBWA KULIKO WOTE DUNIANI MPAKA LEO HII AMBAYE ALIPATIKANA MTWARA UTHIBITSHO MWINGINE KAMA NABII NUHU ALIAMBIWA AWABEBE WANYAMA WA KILA AINA KWENYE SAFINA ISINGE WEZEKANA KUPATIKANA KWENYE JANGWA NA SEHEMU KAMA ISRAEL AU MASHARIKI YA KATI KWA AKILI YA KAWAIDA SIMBA CHUI TAI TEMBO CHATU FARU NYATI WAISHI JANGWANI KWELI? HII LA GHARIKA LILITOKEA TANZANIA BAADA YA BINADAMU KUONGEZEKA BAADHI YA JAMII ZA BINADAMU WALIAMUA KUTAFUTA MAENEO MENGINE YA KUISHI HUKO WALIKO ENDA WALIANZA KUBADILIKA RANGI KUTOKANA NA HALI YA HEWA WAKAPATIKANA JAMII YA WACHINA WAINDI WAZUNGU N.K..
 
Hakuna kitu kama hicho kuwa mwadamu wa kwanza alipatikana Tanzania...acha hizo story za darasa la nne mkuu....

Hakuna udhibitisho huo kuwa fuvu la kwanza liligunduliwa Tanzania..

Uongo mkubwa huo...histora ya darasa la nne...
 
Hakuna kitu kama hicho kuwa mwadamu wa kwanza alipatikana Tanzania...acha hizo story za darasa la nne mkuu....

Hakuna udhibitisho huo kuwa fuvu la kwanza liligunduliwa Tanzania..

Uongo mkubwa huo...histora ya darasa la nne...
Huo ndio ukweli ambao hupo wazi haitaji kuwa na IQ kubwa kuhuelewa kama wanyama karibu wote duniani walipatika Tanzania na wengine bado wapo na ukienda makumbusho pale N'goro ngoro utakutana na maumbo tofauti ya wanyama waliotoweka mifupa yao baado hipo huo ndio uthibitisho na binadamu wa kwanza alikuwa Tanzania na ukienda ismila kuna nyenzo walizotumia BINADAMU wa kwanza..
 
Daaaah ...aise we jamaa bana
Huo ndio ukweli ambao hupo wazi haitaji kuwa na IQ kubwa kuhuelewa kama wanyama karibu wote duniani walipatika Tanzania na wengine bado wapo na ukienda makumbusho pale N'goro ngoro utakutana na maumbo tofauti ya wanyama waliotoweka mifupa yao baado hipo huo ndio uthibitisho na binadamu alikuwa Tanzania na ukienda ismila kuna nyenzo walizotumia BINADAMU wa kwanza..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom