Namna Serikali inavyo chukizwa na unafuu wa maisha ya Mtanzania

UMUGHAKA

JF-Expert Member
Sep 1, 2021
2,157
10,718
Nisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane.

Serikali hii ya Tanzania inayoongozwa na viongozi ambao kila siku wanapenda kupiga selfie na picha tamu-tamu wawapo mbele ya Kamera,INACHUKIZWA MNO na unafuu wa maisha ya mtanzania,kwa kifupi serikali hii haitaki kuona watanzania wanaishi maisha yenye unafuu.

Wakati nchi nyingine duniani zikipambana kutokomeza hali ngumu kwa wananchi wao,hali ni tofauti kwa Tanzania ambapo viongozi wameendelea kuwanyonya na kuhakikisha mtanzania anakamuliwa vilivyo kiasi kwamba mpaka wahakikishe unywele unatoa maziwa ili yakawashibishe watawala.
Viongozi wa Tanzania wapenda sharubati na makange ya mbuni hawataki kabisa kusikia ishu ya kubana matumizi,kubana matumizi kwao ni kama matusi ya udharirishaji wa mwanamke mbele ya kadamnasi kutakakopelekea uyajutie maisha mpaka unaingia kaburini.

Hakika ukizungumzia ishu ya kubana matumizi kwa viongozi utajuta kuzaliwa Tanzania na utashughulikiwa kisawasawa na ikiwezekana utapewa kesi ya uhujumu uchumi.
Hawa ndiyo viongozi na serikali ya Tanzania inayopenda kusifiwa kwa nderemo na vifijo huku ukipaza sauti "Mama anaupiga mwingiiiiii.....Mama aunaupiga mwingiiiiii".Ukipaza sauti kwa nguvu ikapaa hata ikavuka vimo vya mlima kilimanjaro,nakuhakikishia ya kwamba,hata kama hukusoma wewe jiandae kupokea barua ya uteuzi ya kuwa mmoja wapo wa wanakwaya wa kusifu na kuabudu au almaarufu kwaya ya mtakatifu Mkuu wa Mkoa wa kigango cha Mkuu wa Wilaya.

Jana wakati nikiwa natafakari mambo ya siku itakayofuata,niliamua kuwasha luninga na kutazama taarifa ya habari iliyokuwa ikirushwa na Azam,basi moja ya taarifa iliyonivuta hasa ni habari iliyohusu gesi ya asili ijulikanayo kama Compressed Natural Gas(CNG).
Sasa kikawaida Gas hii imekuwa mkombozi kwa watanzania baadhi wenye magari.

Unafuu wa Gas hii imewapelekea watanzania wengi kubadili mifumo ya magari yao iliyokuwa ikitumia mafuta na kuweka mifumo ya gas hii.
Sasa nilipoitazama ile habari iliyokuwa ya kichunguzi,ilidai kwamba mashine hiyo ya mgandamizo(compressed)ya kujazia hiyo gesi kwenye magari imeharibika kwa muda usiyojulika itatengenezwa au kutengemaa lini,HAKUNA MAJIBU.

Alinukuliwa mwanamama mmoja akisema "kupitia gesi hii kwa siku natumia Tsh 6000/= tu kwenye mizunguko yangu tofauti na hapo awali nilipokuwa nikitumia mafuta ilinibidi kwa siku nitumie Tsh 20,000/=,hivyo hii ni nafuu kuliko mafuta".

Taarifa hiyo ikaendelea kusema,wakati ambapo Lita 1 ya mafuta kwenye gari inayokwenda Km 10,Gas hiyo yenyewe kwa Kg 1 inakwenda umbali wa Km 15,kwasasa Lita 1 ya Petrol inakadiriwa kwa kiwango cha chini kuwa Tsh 2969/= wakati kwa Gas hiyo ikiwa Kg 1 ni Tsh 1550/=.
Sasa kwa mafuta ya Tsh 30,000/=kwa gari ya kutembea Km 101,kwa upande wa Gas hiyo kwa gharama hiyo hiyo gari hutembea kwa Km 290.

Hivyo kwa upande wa wananchi walipata unafuu mno wa maisha.

Sasa kiroja na kituko ni kwamba,inavyoonekana kuna makusudi kutoka katika upande wa viongozi wa serikali ambao hawataki kusikia kabisa unafuu wa maisha ya mtanzania mpaka kufikia kutoa "AMRI" za kuharibu hizo mashine ili watu warudi kwenye mafuta na tozo na makato yaendelee kuchukua nafasi kama kawaida.
Nilitegemea serikali kwa unafuu huu wa Gesi ya asili ungefungua vituo vingi na kuhimiza wawekezaji binafsi wawe wengi ili kuwafanya watanzania wahamasike kukimbia mafuta ambayo yanapanda bei kila kukicha na kuleta unafuu kwa watanzania lakini kwa serikali imekuwa kinyume chake.

Serikali hii haitaki kabisa kusikia unafuu wa maisha kwa mtanzania na haitokaa iruhusu vituo hivi kujengwa kwa wingi kwasababu nia na madhumuni ni kuona mtanzania anakamuliwa vilivyo na kutoa maziwa hata kama hauna vyanzo vya maziwa ni lazima yatatoka utake usitake.

Ishu ya kubana matumizi ya serikali nilitegemea kuona magari mengi ya viongozi wetu ambao wamejivika majoho ya "Miungu watu" yakitumia mfumo huu wa gesi ili kupunguza gharama za mafuta,lakini hili viongozi wapenda starehe na anasa hawataki kabisa kulisikia.

Tumekuwa ni mashuhuda watu wa nchi jirani namna wanavyonufaika na Bandari yetu nzuri ya Dar es salaam,magari yao na mizigo yao inatumia kushushwa kwenye bandari yetu lakini kwa wenzetu kodi zao za magari ni nafuu mno wakati magari hayo hayo yanaposhushwa Tanzania ukisema ulipe kodi mpaka unashika kichwa na kujuta kwanini umenunua,hii imewafanya watanzania wengi kununua mikweche(used cars) kwasababu Serikali haitaki kabisa kusikia unafuu wa maisha kwa mtanzania.


WATANZANIA WENZANGU,SERIKALI HAIPO KWA AJILI YA KUONA UNAPATA UNAFUU WA MAISHA,HIVYO NIKUSHAURI UKATAFUNE NYASI ZA JUNCAO ILI IWE RAHISI KUKAMULIWA UTOE MAZIWA,TOFAUTI NA HAPO UTAENDELEA KUUMIA WAKATI WA UKAMUAJI.

Nawasilisha.
 
watu wengi Sana wanapenda Sana mambo ya mapenzi,Kula mbususu,sijui kutembea na mke WA mtu,mara unajua Mchepuko wangu bla bla bla!
Full bla blaa jitu zima linaanzisha mada eti mchepuko wangu Mara HV kawa vile alfu unakuta vijana 8000 k wanachekacheka tu kule wapuuz Sana nakuacha kusoma mamb ya maana zeny tija nakuoji vitu vya msingi Kama mleta mada alivyo fanya Kaz yake nzuri Sana nakupongeza Sana bean umugaha mm huwa ndio vitu HV napenda kusoma ya kukozoa na Kutoa way forward CYO kuleta mambo ya michepuko na kina katibu wa masanja

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Uzi unakua na wachangiaji wengi, kama mada iliopo, inavuta watu kutofautiana kimawazo.
Mada iliyopo mtu ajkisha isoma, unaona jamaa kasemea kilio cha wengi, hivyo hawaoni cha kuongeza.

Labda tuwakumbushe hao walioshika mpini, mnakumbushwa na viumbe wenzenu wa Mungu, nanyi mnapaswa kumuogopa Mungu, ingekua inawezekana kubadilishana makoti, alau kwa siku mbili tu, nadhani mleta mada, angeandika ila anajua haiwezekani, ndiyo maana hakuandika.

Ila kwakua wote tumeumbwa na Mungu basi tumuogope Mungu.
 
Nisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane.

Serikali hii ya Tanzania inayoongozwa na viongozi ambao kila siku wanapenda kupiga selfie na picha tamu-tamu wawapo mbele ya Kamera,INACHUKIZWA MNO na unafuu wa maisha ya mtanzania,kwa kifupi serikali hii haitaki kuona watanzania wanaishi maisha yenye unafuu.

Wakati nchi nyingine duniani zikipambana kutokomeza hali ngumu kwa wananchi wao,hali ni tofauti kwa Tanzania ambapo viongozi wameendelea kuwanyonya na kuhakikisha mtanzania anakamuliwa vilivyo kiasi kwamba mpaka wahakikishe unywele unatoa maziwa ili yakawashibishe watawala.
Viongozi wa Tanzania wapenda sharubati na makange ya mbuni hawataki kabisa kusikia ishu ya kubana matumizi,kubana matumizi kwao ni kama matusi ya udharirishaji wa mwanamke mbele ya kadamnasi kutakakopelekea uyajutie maisha mpaka unaingia kaburini.

Hakika ukizungumzia ishu ya kubana matumizi kwa viongozi utajuta kuzaliwa Tanzania na utashughulikiwa kisawasawa na ikiwezekana utapewa kesi ya uhujumu uchumi.
Hawa ndiyo viongozi na serikali ya Tanzania inayopenda kusifiwa kwa nderemo na vifijo huku ukipaza sauti "Mama anaupiga mwingiiiiii.....Mama aunaupiga mwingiiiiii".Ukipaza sauti kwa nguvu ikapaa hata ikavuka vimo vya mlima kilimanjaro,nakuhakikishia ya kwamba,hata kama hukusoma wewe jiandae kupokea barua ya uteuzi ya kuwa mmoja wapo wa wanakwaya wa kusifu na kuabudu au almaarufu kwaya ya mtakatifu Mkuu wa Mkoa wa kigango cha Mkuu wa Wilaya.

Jana wakati nikiwa natafakari mambo ya siku itakayofuata,niliamua kuwasha luninga na kutazama taarifa ya habari iliyokuwa ikirushwa na Azam,basi moja ya taarifa iliyonivuta hasa ni habari iliyohusu gesi ya asili ijulikanayo kama Compressed Natural Gas(CNG).
Sasa kikawaida Gas hii imekuwa mkombozi kwa watanzania baadhi wenye magari.

Unafuu wa Gas hii imewapelekea watanzania wengi kubadili mifumo ya magari yao iliyokuwa ikitumia mafuta na kuweka mifumo ya gas hii.
Sasa nilipoitazama ile habari iliyokuwa ya kichunguzi,ilidai kwamba mashine hiyo ya mgandamizo(compressed)ya kujazia hiyo gesi kwenye magari imeharibika kwa muda usiyojulika itatengenezwa au kutengemaa lini,HAKUNA MAJIBU.

Alinukuliwa mwanamama mmoja akisema "kupitia gesi hii kwa siku natumia Tsh 6000/= tu kwenye mizunguko yangu tofauti na hapo awali nilipokuwa nikitumia mafuta ilinibidi kwa siku nitumie Tsh 20,000/=,hivyo hii ni nafuu kuliko mafuta".

Taarifa hiyo ikaendelea kusema,wakati ambapo Lita 1 ya mafuta kwenye gari inayokwenda Km 10,Gas hiyo yenyewe kwa Kg 1 inakwenda umbali wa Km 15,kwasasa Lita 1 ya Petrol inakadiriwa kwa kiwango cha chini kuwa Tsh 2969/= wakati kwa Gas hiyo ikiwa Kg 1 ni Tsh 1550/=.
Sasa kwa mafuta ya Tsh 30,000/=kwa gari ya kutembea Km 101,kwa upande wa Gas hiyo kwa gharama hiyo hiyo gari hutembea kwa Km 290.

Hivyo kwa upande wa wananchi walipata unafuu mno wa maisha.

Sasa kiroja na kituko ni kwamba,inavyoonekana kuna makusudi kutoka katika upande wa viongozi wa serikali ambao hawataki kusikia kabisa unafuu wa maisha ya mtanzania mpaka kufikia kutoa "AMRI" za kuharibu hizo mashine ili watu warudi kwenye mafuta na tozo na makato yaendelee kuchukua nafasi kama kawaida.
Nilitegemea serikali kwa unafuu huu wa Gesi ya asili ungefungua vituo vingi na kuhimiza wawekezaji binafsi wawe wengi ili kuwafanya watanzania wahamasike kukimbia mafuta ambayo yanapanda bei kila kukicha na kuleta unafuu kwa watanzania lakini kwa serikali imekuwa kinyume chake.

Serikali hii haitaki kabisa kusikia unafuu wa maisha kwa mtanzania na haitokaa iruhusu vituo hivi kujengwa kwa wingi kwasababu nia na madhumuni ni kuona mtanzania anakamuliwa vilivyo na kutoa maziwa hata kama hauna vyanzo vya maziwa ni lazima yatatoka utake usitake.

Ishu ya kubana matumizi ya serikali nilitegemea kuona magari mengi ya viongozi wetu ambao wamejivika majoho ya "Miungu watu" yakitumia mfumo huu wa gesi ili kupunguza gharama za mafuta,lakini hili viongozi wapenda starehe na anasa hawataki kabisa kulisikia.

Tumekuwa ni mashuhuda watu wa nchi jirani namna wanavyonufaika na Bandari yetu nzuri ya Dar es salaam,magari yao na mizigo yao inatumia kushushwa kwenye bandari yetu lakini kwa wenzetu kodi zao za magari ni nafuu mno wakati magari hayo hayo yanaposhushwa Tanzania ukisema ulipe kodi mpaka unashika kichwa na kujuta kwanini umenunua,hii imewafanya watanzania wengi kununua mikweche(used cars) kwasababu Serikali haitaki kabisa kusikia unafuu wa maisha kwa mtanzania.


WATANZANIA WENZANGU,SERIKALI HAIPO KWA AJILI YA KUONA UNAPATA UNAFUU WA MAISHA,HIVYO NIKUSHAURI UKATAFUNE NYASI ZA JUNCAO ILI IWE RAHISI KUKAMULIWA UTOE MAZIWA,TOFAUTI NA HAPO UTAENDELEA KUUMIA WAKATI WA UKAMUAJI.

Nawasilisha.
Umenena ya maana sana sana
 
Serekali yetu haiajiri watendaji ambao ni vichwa ...na ikiwaajiri wanakua wanadhibitiwa sasa hapa matatizo ndio yanapotokea..kunakua hakuna ubunifu,

Hasa kwenye aina ya vyanzo vya kodi
 
Viongozi wabinafsi ,wanajiangalia wao tu hata kama wameshiba, hawawezi kuwaangalia ambao hawajala wawape unafuu, bali ni kuwanyang'anya hata kile kidogo walichonacho
 
Hahah nimecheka hapo mwisho, Mleta mada ukihoji zaidi unajibiwa "Serikali haitakugawia fedha majumbani mwenu"

Nchi hii wananchi hawajui kazi ya serikali, infact wanadhani kazi ya mwananchi ni kumsaidia kiongozi aishi vizuri na afanye anasa zake.
 
Nisikuchoshe na usinichoshe,tusichoshane.

Serikali hii ya Tanzania inayoongozwa na viongozi ambao kila siku wanapenda kupiga selfie na picha tamu-tamu wawapo mbele ya Kamera,INACHUKIZWA MNO na unafuu wa maisha ya mtanzania,kwa kifupi serikali hii haitaki kuona watanzania wanaishi maisha yenye unafuu.

Wakati nchi nyingine duniani zikipambana kutokomeza hali ngumu kwa wananchi wao,hali ni tofauti kwa Tanzania ambapo viongozi wameendelea kuwanyonya na kuhakikisha mtanzania anakamuliwa vilivyo kiasi kwamba mpaka wahakikishe unywele unatoa maziwa ili yakawashibishe watawala.
Viongozi wa Tanzania wapenda sharubati na makange ya mbuni hawataki kabisa kusikia ishu ya kubana matumizi,kubana matumizi kwao ni kama matusi ya udharirishaji wa mwanamke mbele ya kadamnasi kutakakopelekea uyajutie maisha mpaka unaingia kaburini.

Hakika ukizungumzia ishu ya kubana matumizi kwa viongozi utajuta kuzaliwa Tanzania na utashughulikiwa kisawasawa na ikiwezekana utapewa kesi ya uhujumu uchumi.
Hawa ndiyo viongozi na serikali ya Tanzania inayopenda kusifiwa kwa nderemo na vifijo huku ukipaza sauti "Mama anaupiga mwingiiiiii.....Mama aunaupiga mwingiiiiii".Ukipaza sauti kwa nguvu ikapaa hata ikavuka vimo vya mlima kilimanjaro,nakuhakikishia ya kwamba,hata kama hukusoma wewe jiandae kupokea barua ya uteuzi ya kuwa mmoja wapo wa wanakwaya wa kusifu na kuabudu au almaarufu kwaya ya mtakatifu Mkuu wa Mkoa wa kigango cha Mkuu wa Wilaya.

Jana wakati nikiwa natafakari mambo ya siku itakayofuata,niliamua kuwasha luninga na kutazama taarifa ya habari iliyokuwa ikirushwa na Azam,basi moja ya taarifa iliyonivuta hasa ni habari iliyohusu gesi ya asili ijulikanayo kama Compressed Natural Gas(CNG).
Sasa kikawaida Gas hii imekuwa mkombozi kwa watanzania baadhi wenye magari.

Unafuu wa Gas hii imewapelekea watanzania wengi kubadili mifumo ya magari yao iliyokuwa ikitumia mafuta na kuweka mifumo ya gas hii.
Sasa nilipoitazama ile habari iliyokuwa ya kichunguzi,ilidai kwamba mashine hiyo ya mgandamizo(compressed)ya kujazia hiyo gesi kwenye magari imeharibika kwa muda usiyojulika itatengenezwa au kutengemaa lini,HAKUNA MAJIBU.

Alinukuliwa mwanamama mmoja akisema "kupitia gesi hii kwa siku natumia Tsh 6000/= tu kwenye mizunguko yangu tofauti na hapo awali nilipokuwa nikitumia mafuta ilinibidi kwa siku nitumie Tsh 20,000/=,hivyo hii ni nafuu kuliko mafuta".

Taarifa hiyo ikaendelea kusema,wakati ambapo Lita 1 ya mafuta kwenye gari inayokwenda Km 10,Gas hiyo yenyewe kwa Kg 1 inakwenda umbali wa Km 15,kwasasa Lita 1 ya Petrol inakadiriwa kwa kiwango cha chini kuwa Tsh 2969/= wakati kwa Gas hiyo ikiwa Kg 1 ni Tsh 1550/=.
Sasa kwa mafuta ya Tsh 30,000/=kwa gari ya kutembea Km 101,kwa upande wa Gas hiyo kwa gharama hiyo hiyo gari hutembea kwa Km 290.

Hivyo kwa upande wa wananchi walipata unafuu mno wa maisha.

Sasa kiroja na kituko ni kwamba,inavyoonekana kuna makusudi kutoka katika upande wa viongozi wa serikali ambao hawataki kusikia kabisa unafuu wa maisha ya mtanzania mpaka kufikia kutoa "AMRI" za kuharibu hizo mashine ili watu warudi kwenye mafuta na tozo na makato yaendelee kuchukua nafasi kama kawaida.
Nilitegemea serikali kwa unafuu huu wa Gesi ya asili ungefungua vituo vingi na kuhimiza wawekezaji binafsi wawe wengi ili kuwafanya watanzania wahamasike kukimbia mafuta ambayo yanapanda bei kila kukicha na kuleta unafuu kwa watanzania lakini kwa serikali imekuwa kinyume chake.

Serikali hii haitaki kabisa kusikia unafuu wa maisha kwa mtanzania na haitokaa iruhusu vituo hivi kujengwa kwa wingi kwasababu nia na madhumuni ni kuona mtanzania anakamuliwa vilivyo na kutoa maziwa hata kama hauna vyanzo vya maziwa ni lazima yatatoka utake usitake.

Ishu ya kubana matumizi ya serikali nilitegemea kuona magari mengi ya viongozi wetu ambao wamejivika majoho ya "Miungu watu" yakitumia mfumo huu wa gesi ili kupunguza gharama za mafuta,lakini hili viongozi wapenda starehe na anasa hawataki kabisa kulisikia.

Tumekuwa ni mashuhuda watu wa nchi jirani namna wanavyonufaika na Bandari yetu nzuri ya Dar es salaam,magari yao na mizigo yao inatumia kushushwa kwenye bandari yetu lakini kwa wenzetu kodi zao za magari ni nafuu mno wakati magari hayo hayo yanaposhushwa Tanzania ukisema ulipe kodi mpaka unashika kichwa na kujuta kwanini umenunua,hii imewafanya watanzania wengi kununua mikweche(used cars) kwasababu Serikali haitaki kabisa kusikia unafuu wa maisha kwa mtanzania.


WATANZANIA WENZANGU,SERIKALI HAIPO KWA AJILI YA KUONA UNAPATA UNAFUU WA MAISHA,HIVYO NIKUSHAURI UKATAFUNE NYASI ZA JUNCAO ILI IWE RAHISI KUKAMULIWA UTOE MAZIWA,TOFAUTI NA HAPO UTAENDELEA KUUMIA WAKATI WA UKAMUAJI.

Nawasilisha.
𝐁𝐥𝐞𝐬𝐬𝐞𝐝 𝐬𝐚𝐧𝐚

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom