Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,475
- 39,991
Katumiwa ujumbe na afande; ameshindwa kujibu -- akubali au akatae. Ilikuwa ni mfululizo wa SMS
Ungekuwa wewe mdada ungesemaje...???
SMS 1 - Unajua nakuthamini zaidi ya POSHO na MSHAHARA, bila wewe siwezi kuishi ni sawa na kukosa BUNDUKI eneo la tukio lako mpenzi wangu.
SMS 2 - Usiniweke roho juu kama yanavyoniweka maandamano ya CHADEMA
SMS 3 - Nitakuheshimu kama ninavyoliheshimu LINDO, wewe ndio IGP wa moyo wangu, daima nitakuweka mbele kama kama LIGHT MAKER kwenye gwaride. Mbona uko kimya.
SMS 4 - Nijibu basi nipate kufungua JALADA ndani ya moyo wako. Usinifanye moyo ukaenda mbio kama DEFENDER MPYA, ntakuwekea usalama kama msafara wa RAIS; nina RB ya mapenzi.
Ungekuwa wewe mdada ungesemaje...???