EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,091
Kutokana na kukua kwa teknolojia, socialization imekuwa rahisi sana siku hizi.
Tofauti na zamani ambapo njia kuu ya kukutana ilikuwa physical, siku hizi njia kuu ya kukutana na watu imekuwa digital, kwa maana ya kutumia mitandao na njia nyingine zinazoendana na hizo.
Kukutana huku kumekuwa kunapelekea kuanzishwa kwa mahusiano ndani ya mitandao hii. Hata hivyo, pamoja na makutano haya ya mtandao kuongezeka na kuendelea kukua kwa kasi, bado yamekuwa yakikumbana na changamoto nyingi kubwa ikiwa mindset ya watu wengi kuwa kwenye mfumo wa zamani pamoja na kwamba wanapractice mfumo mpya.
Kwa mfano, imekuwa ni aghalabu kwa watu waliokutana online na kuwa wapenzi kutangaza hadharani kuwa wamekutana online, hii inachangiwa sana na baadhi ya watu kudhani kuwa hakuna mahusiano ya kweli yanayopatikana kupitia mitandao.
Sasa wengi wetu hapa tumetumia mitandao kwa muda sasa, na katika muda huo tumeshajikuta kwenye mahusiano mara moja au zaidi ambayo yamekutana na changamoto hizi na zile kwasababu tu yametokea kwenye mtandao, tunaweza kushare changamoto hizo na namna gani ya kukabiliana nazo?
Mada mezani
Tofauti na zamani ambapo njia kuu ya kukutana ilikuwa physical, siku hizi njia kuu ya kukutana na watu imekuwa digital, kwa maana ya kutumia mitandao na njia nyingine zinazoendana na hizo.
Kukutana huku kumekuwa kunapelekea kuanzishwa kwa mahusiano ndani ya mitandao hii. Hata hivyo, pamoja na makutano haya ya mtandao kuongezeka na kuendelea kukua kwa kasi, bado yamekuwa yakikumbana na changamoto nyingi kubwa ikiwa mindset ya watu wengi kuwa kwenye mfumo wa zamani pamoja na kwamba wanapractice mfumo mpya.
Kwa mfano, imekuwa ni aghalabu kwa watu waliokutana online na kuwa wapenzi kutangaza hadharani kuwa wamekutana online, hii inachangiwa sana na baadhi ya watu kudhani kuwa hakuna mahusiano ya kweli yanayopatikana kupitia mitandao.
Sasa wengi wetu hapa tumetumia mitandao kwa muda sasa, na katika muda huo tumeshajikuta kwenye mahusiano mara moja au zaidi ambayo yamekutana na changamoto hizi na zile kwasababu tu yametokea kwenye mtandao, tunaweza kushare changamoto hizo na namna gani ya kukabiliana nazo?
Mada mezani