Ndalilo
JF-Expert Member
- Jan 30, 2013
- 2,937
- 6,293
😂🤣🤣🤣Wakishua hamuezi kuelewa haya mambo
Nilitamani kuitwa tu "wakishua" siku moja, tatizo nguo pekee iliyokuwa inavaliwa na mimi ni kaptula, chini bare juu bare, nakimbiza zangu tairi la gari na kulipanda likiwa kwenye mwendo, ringi la baiskeli naendesha kwa mti, mwendo mdundo, mchana naparamia michongoma kuangua mikwaju ile, kula mpaka unavimbiwa, tengeneza kisu kwa kutumia koa, boksi na mpira wa manati unatengenezea ala ya kisu hiyo, kinatumika kukatia matairi kutoka kwenye ndala, gari la miwaya, weekend tunahamia zetu beach kuruka samasoti na mapira yetu
Sijui kama umenielewa boss!