k.shuku kibosho
JF-Expert Member
- Jun 21, 2015
- 258
- 229
bro umeuwa aise!Saga pilipili kwa wingi kisha jaza kwenye makopo hasa yale ya reds, bavaria8.6 ama grandmalt toboa vitobo vidogovidogo kwa chini kisha ning'iniza na kamba kwenye kila shina la mahindi hasa sehemu wanako pendelea kupitia.
Hapo ngedere akiupalamia mti wa mhindi lile kopo litatikisika na kumwagia pilipili machoni. Atashindwa kuona na kuanza kupuyanga tu akijibamiza huku na kule wakati huo wewe unakuwa na NGONGO/RUNGU lako ni mwendwa wa kuponda vichwa tu! hapo hata akipanda kwenye mti mlenge na manati atapanda hadi kileleni mwa mti, sasa kwakuwa atakuwa haoni ataanguka chini unatwanga rungu.
Ukibahatika kumnasa mkubwa wao usimuue mzimishe kidogo kisha mnyweshe NYAGI kumpiga nusu kaputi. Mchune ngozi ya uso na umvishe kengele kisha muache aende zake kuwatafuta wenzie ambao watamnyanyapaa na kuhama maeneo hayo.
Fanya hivyo kisha rudisha mrejesho hapa.
Ninazo mbinu nyingi sana za kuwasurubu hawa wanyama wachafuzi so i hope this one will workout.
Sent using Jamii Forums mobile app