SoC02 Namna bora ya kulea watoto wa kizazi cha sasa

Stories of Change - 2022 Competition

CK Allan

JF-Expert Member
Aug 14, 2013
2,729
5,917
Wakuu nimerudi Tena katika Story of change,

Naomba Leo niwashirikishe mbinu nzuri za kuwalea watoto katika kipindi hiki Cha utandawazi!

Kwanza nikiri wazi Mimi ni mzazi na mwalimu pia, kwahiyo haya ninayoshauri ni mambo ambayo Binafsi nimeyaona yakifanya kazi kwa ufanisi mkubwa! Kabla sijatoa hizi mbinu hebu tuone kwanza wazazi wengi wanakosea ama kukwama wapi katika kulea watoto!

1. Kuwafanya watoto waogope kufanya makosa kwa kuwa wataadhibiwa!

Naam wazazi wengi huwaambia watoto ole wao wafanye hiki au kile watakoma! Na kweli wanapofanya hivyo walivyoambiwa wasifanye basi wanakoma kweli! Hili ni kosa! Nitasema hapo baadae

2. Kuamini kuwa Kuna mambo ambayo mtoto hajui na hapaswi kujua!!
Wazazi wengi hudhani kuwa watoto wao Kuna mambo hawajui mfano mambo ya mapenzi, uvutaji, kuangalia picha za ngono n.k

Na ndipo siku mzazi anaambiwa mwanae anafanya hiki au kile basi anapata presha anaanguka na kufa! Kwakuwa hakufiria kuwa mwanae anajua jambo Hilo au hata kulifanya.

3. Kutokujua watoto wake kwa undani , tabia zao na kile wanachopendelea ama wasichopenda! Ni ajabu sana baadhi ya wazazi hawajui watoto wao wanapendelea mambo gani na wakati mwingine hata hawajui hisia za watoto wao na kuwalazimisha wafanye mambo ambayo watoto hawayataki na mwishowe wanakuwa disappointed ! Hujawahi kuona mtoto anafanya jambo kwa Siri chuoni analopenda lakini wazazi wanajua yupo anasoma au kufanya jambo Fulani! Na mwishowe wanabaki kushangaa!

Baada ya kuona hayo baadhi ya makosa sasa tuanze na namna Bora ya kuishi na Hawa watoto wa kisasa

1. Mfanye mtoto ajue faida na hasara ya anachokifanya kuliko tu kumwambia ukifanya hiki utanikoma! Mfano kama una bint amefikia umri wa kuvunja ungo Kaa nae kama mzazi mwambie wazi wazi kuwa akifanya mapenzi anaweza kupata ujauzito au magonjwa ya zinaa na pia akipata mimba anaweza kushindwa kutimiza ndoto Kwa wakati husika, lakini pia anaweza kupata madhara wakati wa kujifungua kwakuwa viungo vyake Bado havijakomaa! Hii ni nzuri kuliko tu kumwambia mtoto ole wako upate mimba!! Kumbuka unapomtishia mtoto asifanye jambo Fulani kwa Sababu Yako siku akiwa mbali na wewe au usipokuwepo basi atalifanya hujawahi kuona watoto wanaobanwa na wazazi wao jinsi wanavyojiachia wakiwa mbali na wazazi wao??

2. Mfanye mtoto ajue kuwa Kila anachokifanya Kina faida na hasara kwake yeye mwenyewe! Mara nyingi wazazi wamekuwa wakiwaambia watoto mfano wasome kwa bidii ili waje kuwasaidia ndugu, wadogo zao n.k lakini usahihi ni kumuandaa mtoto kuja kujisaidia mwenyewe! Na hii itamjengea uangalizi wa kufanya mambo bila hata uangalizi! Mwambie mtoto wazi wazi hasara za kutokusoma kwa bidii ikiwezekana Mpe mifano hai na faida zake.. mwambie akitumia muda mwingi kwenye tamthilia anapoteza nini kuliko tu kumwambia sitaki kukuona kwenye TV

3. Mjue mtoto wako vyema! Mwalimu wa kwanza ni wewe mzazi tambua mambo gani ambayo mwanao anaweza kuyafanya, tambua vipaji vyake na uwezo wake na udhaifu wake! Kuna watu wamelazimisha watoto wao kuwa madaktari kumbe wangeweza kuwa waigizaji wazuri! Kumbe wangekuwa mainjinia wazuri n.k
Mzazi mjue mtoto wako na umsapoti!

4 . Usimfiche mtoto kuhusu afya ya uzazi, usipomwambia ukweli Kuna watu watamwambia Tena pengine kwa ubaya! Una mtoto wa kike mwambie yeye ni mzuri! Anavutia na anaweza kutongozwa na wanaume kwa kumlaghai na mambo gani ya kufanya , Kuna wazazi hapa ukiwauliza wameongea lini na watoto wao utashangaa!!

5. Jaribu kwa kadri uwezavyo kujihadhari na tabia zako mbaya mbele ya watoto! Kwamfano kama mke na mume mna ugomvi basi jitahidini kuumaliza chumbani kwenu na watoto wasijue! Kama una mchepuko wako usije kufanya kosa kuuleta nyumbani kisa mwenza wako hayupo! Lakini kama watoto wapo hata kama ni wadogo kwa umri lakini Kuna kitu watajifunza kutoka kwako! Kama una tabia za ulevi na usingependa watoto wako wawe walevi kama wewe basi usinywe na kulewa mbele Yao! Kitaalamu watoto wanajifunza kwanza kwa kuona kwa wazazi wao ndipo huiga kile ambacho wazazi hufanya! Hivyo mambo unayofanya Yana athari kubwa sana Kwa watoto wako.. chanya au hasi!!

6. Mwache mtoto ajifunze kupitia makosa yake! Watoto kwa Namna walivyo na sisi sote tulipitia utoto , kufanya makosa ni sehemu ya ukuaji! Hivyo mtoto anapofanya kosa badala ya kumhukumu na kumkumbusha Kila mara kosa lake ni vyema kumpa nafasi zaidi ya kujifunza kupitia Hilo kosa lake! Unaweza pia kutumia kama kielelezo na sababu ya wewe kukaa nae na kumshauri namna Bora ya kufanya vizuri wakati ujao! Watoto wanafanya vizuri sana wakiaminiwa na kupewa nafasi ya pili!

7. Mzoeze mtoto wako kuishi kutokana na Hali na mazingira ya kipato chako! Kamwe usimpe mtoto Kila kitu ambacho analilia! Mfanye mtoto aridhike na maisha ya kwao, lakini pia aelewe kuwa unafanya Kila uwezavyo kuwatunza vizuri! Hapa simaanishi mzazi uwe bahili! Hapana, Bali mfanye mtoto akubali maisha halisi ya kwao!

8. Nenda na mtoto wako sehemu Yako ya kazi angalau mara moja kwa mwaka, kama wewe ni mkulima basi angalau nenda nae shamba mwanao, hata kama hatashika jembe lakini angalau ataona wapi pesa inapatikana, kama umeajiriwa ofisini basi nenda nae, haijalishi ni shughuli Gani unafanya kama ni ya halali basi wewe mpeleke mtoto aone! Kuna watoto wengi hawajui shughuli wanazofanya wazazi wao na wamekuwa watu wa kupokea zawadi tu Kila mara wazazi wanaporudi, hata hivyo Kuna namna inamjenga mtoto akijua kile mzazi anafanya, ushawahi kuulizwa na mtoto kuhusu kazi Yako? Basi usiishie kumjibu Bali nenda nae kabisa!

9. Chunguza na jua marafiki wa mtoto wako hii itakusaidia kujua tabia ya mtoto wako! Hata kama Kuna tabia ambazo mwanao anakuficha basi kupitia tabia za marafiki zake basi unaweza kujua kwa urahisi tabia ya mwanao! Na pindi unapoona tabia tofauti basi usisite kukaa nae na kumuelewesha na kumsaidia!

10. Badala ya kutoa adhabu akikosea Toa zawadi anapofanya vizuri!! Hii ni mbinu ya mwisho nzuri! Kwa wale wazazi ambao wamekuwa na tabia ya kutoa adhabu Kali kwa watoto wanapokosea basi badili! Anza kwa kumpongeza anapofanya vizuri! Mfano umesafiri kwa wiki kadhaa unaporudi nyumbani mwambie mtoto kuwa unampongeza kwa kuwa mtoto mtii kwa kusaidia kazi ndogo ndogo za nyumbani, kuwahi nyumbani n.k, unaweza pia kumwambia mtoto utampa zawadi Fulani akishika nafasi Fulani katika Darasa lake, badala ya kumuadhibu anapofeli! Kwa kuendelea kumpa motisha anapofanya vizuri basi Tabia hiyo njema inaendelea zaidi!

MWISHO
Lazima tukubali kuwa Dunia inabadilika kwa kasi mzazi ukubali kubadilika na kuongoza watoto kwa uhalisia badala ya hisia..

Tukumbuke kuwa mzazi ni mtoto Mzee! Kwa maana kuwa sehemu zote anazopitia mtoto wewe mzazi umepitia na Kwa hivyo una nafasi kubwa ya kumsaidia mtoto wako ikibidi asipitie mambo mabaya ambayo wewe umepitia!
Daima mkumbushe mwanao kuwa
"KICHAA ANACHEKESHA SANA KAMA HATOKEI KWENYE FAMILIA YENU!"

Asanteni

Najibu maswali kwenye comments
 
Kichaa anachekesha Sana kama hatokei kwenye familia yenu,unamaanisha nn mkuu!???nijambo zito hili mwalimu.
Ndio tumekuwa na tabia ya kuwacheka vichaa mtaani wakiwa wamevua nguo, kuokota makopo n.k..
Lakini nakuambia huyo kichaa akiwa ni kaka au dada, au mama Yako mzazi kabisa huwezi kucheka hata kidogo!!..

Mfundishe mtoto kuelewa kuwa kichaa sio kichekesho Bali ni tatizo ambalo halifai kuwa burudani
 
Wakuu nimerudi Tena katika Story of change,

Naomba Leo niwashirikishe mbinu nzuri za kuwalea watoto katika kipindi hiki Cha utanadawazi!

Kwanza nikiri wazi Mimi ni mzazi na mwalimu pia, kwahiyo haya ninayoshauri ni mambo ambayo Binafsi nimeyaona yakifanya kazi kwa ufanisi mkubwa! Kabla sijatoa hizi mbinu hebu tuone kwanza wazazi wengi wanakosea ama kukwama wapi katika kulea watoto!

1. Kuwafanya watoto waogope kufanya makosa kwa kuwa wataadhibiwa!

Naam wazazi wengi huwaambia watoto ole wao wafanye hiki au kile watakoma! Na kweli wanapofanya hivyo walivyoambiwa wasifanye basi wanakoma kweli! Hili ni kosa! Nitasema hapo baadae

2. Kuamini kuwa Kuna mambo ambayo mtoto hajui na hapaswi kujua!!
Wazazi wengi hudhani kuwa watoto wao Kuna mambo hawajui mfano mambo ya mapenzi, uvutaji, kuangalia picha za ngono n.k

Na ndipo siku mzazi anaambiwa mwanae anafanya hiki au kile basi anapata presha anaanguka na kufa! Kwakuwa hakufiria kuwa mwanae anajua jambo Hilo au hata kulifanya.

3. Kutokujua watoto wake kwa undani , tabia zao na kile wanachopendelea ama wasichopenda! Ni ajabu sana baadhi ya wazazi hawajui watoto wao wanapendelea mambo gani na wakati mwingine hata hawajui hisia za watoto wao na kuwalazimisha wafanye mambo ambayo watoto hawayataki na mwishowe wanakuwa disappointed ! Hujawahi kuona mtoto anafanya jambo kwa Siri chuoni analopenda lakini wazazi wanajua yupo anasoma au kufanya jambo Fulani! Na mwishowe wanabaki kushangaa!

Baada ya kuona hayo baadhi ya makosa sasa tuanze na namna Bora ya kuishi na Hawa watoto wa kisasa

1. Mfanye mtoto ajue faida na hasara ya anachokifanya kuliko tu kumwambia ukifanya hiki utanikoma! Mfano kama una bint amefikia umri wa kuvunja ungo Kaa nae kama mzazi mwambie wazi wazi kuwa akifanya mapenzi anaweza kupata ujauzito au magonjwa ya zinaa na pia akipata mimba anaweza kushindwa kutimiza ndoto Kwa wakati husika, lakini pia anaweza kupata madhara wakati wa kujifungua kwakuwa viungo vyake Bado havijakomaa! Hii ni nzuri kuliko tu kumwambia mtoto ole wako upate mimba!! Kumbuka unapomtishia mtoto asifanye jambo Fulani kwa Sababu Yako siku akiwa mbali na wewe au usipokuwepo basi atalifanya hujawahi kuona watoto wanaobanwa na wazazi wao jinsi wanavyojiachia wakiwa mbali na wazazi wao??

2. Mfanye mtoto ajue kuwa Kila anachokifanya Kina faida na hasara kwake yeye mwenyewe! Mara nyingi wazazi wamekuwa wakiwaambia watoto mfano wasome kwa bidii ili waje kuwasaidia ndugu, wadogo zao n.k lakini usahihi ni kumuandaa mtoto kuja kujisaidia mwenyewe! Na hii itamjengea uangalizi wa kufanya mambo bila hata uangalizi! Mwambie mtoto wazi wazi hasara za kutokusoma kwa bidii ikiwezekana Mpe mifano hai na faida zake.. mwambie akitumia muda mwingi kwenye tamthilia anapoteza nini kuliko tu kumwambia sitaki kukuona kwenye TV

3. Mjue mtoto wako vyema! Mwalimu wa kwanza ni wewe mzazi tambua mambo gani ambayo mwanao anaweza kuyafanya, tambua vipaji vyake na uwezo wake na udhaifu wake! Kuna watu wamelazimisha watoto wao kuwa madaktari kumbe wangeweza kuwa waigizaji wazuri! Kumbe wangekuwa mainjinia wazuri n.k
Mzazi mjue mtoto wako na umsapoti!

4 . Usimfiche mtoto kuhusu afya ya uzazi, usipomwambia ukweli Kuna watu watamwambia Tena pengine kwa ubaya! Una mtoto wa kike mwambie yeye ni mzuri! Anavutia na anaweza kutongozwa na wanaume kwa kumlaghai na mambo gani ya kufanya , Kuna wazazi hapa ukiwauliza wameongea lini na watoto wao utashangaa!!

5. Jaribu kwa kadri uwezavyo kujihadhari na tabia zako mbaya mbele ya watoto! Kwamfano kama mke na mume mna ugomvi basi jitahidini kuumaliza chumbani kwenu na watoto wasijue! Kama una mchepuko wako usije kufanya kosa kuuleta nyumbani kisa mwenza wako hayupo! Lakini kama watoto wapo hata kama ni wadogo kwa umri lakini Kuna kitu watajifunza kutoka kwako! Kama una tabia za ulevi na usingependa watoto wako wawe walevi kama wewe basi usinywe na kulewa mbele Yao! Kitaalamu watoto wanajifunza kwanza kwa kuona kwa wazazi wao ndipo huiga kile ambacho wazazi hufanya! Hivyo mambo unayofanya Yana athari kubwa sana Kwa watoto wako.. chanya au hasi!!

6. Mwache mtoto ajifunze kupitia makosa yake! Watoto kwa Namna walivyo na sisi sote tulipitia utoto , kufanya makosa ni sehemu ya ukuaji! Hivyo mtoto anapofanya kosa badala ya kumhukumu na kumkumbusha Kila mara kosa lake ni vyema kumpa nafasi zaidi ya kujifunza kupitia Hilo kosa lake! Unaweza pia kutumia kama kielelezo na sababu ya wewe kukaa nae na kumshauri namna Bora ya kufanya vizuri wakati ujao! Watoto wanafanya vizuri sana wakiaminiwa na kupewa nafasi ya pili!

7. Mzoeze mtoto wako kuishi kutokana na Hali na mazingira ya kipato chako! Kamwe usimpe mtoto Kila kitu ambacho analilia! Mfanye mtoto aridhike na maisha ya kwao, lakini pia aelewe kuwa unafanya Kila uwezavyo kuwatunza vizuri! Hapa simaanishi mzazi uwe bahili! Hapana, Bali mfanye mtoto akubali maisha halisi ya kwao!

8. Nenda na mtoto wako sehemu Yako ya kazi angalau mara moja kwa mwaka, kama wewe ni mkulima basi angalau nenda nae shamba mwanao, hata kama hatashika jembe lakini angalau ataona wapi pesa inapatikana, kama umeajiriwa ofisini basi nenda nae, haijalishi ni shughuli Gani unafanya kama ni ya halali basi wewe mpeleke mtoto aone! Kuna watoto wengi hawajui shughuli wanazofanya wazazi wao na wamekuwa watu wa kupokea zawadi tu Kila mara wazazi wanaporudi, hata hivyo Kuna namna inamjenga mtoto akijua kile mzazi anafanya, ushawahi kuulizwa na mtoto kuhusu kazi Yako? Basi usiishie kumjibu Bali nenda nae kabisa!

9. Chunguza na jua marafiki wa mtoto wako hii itakusaidia kujua tabia ya mtoto wako! Hata kama Kuna tabia ambazo mwanao anakuficha basi kupitia tabia za marafiki zake basi unaweza kujua kwa urahisi tabia ya mwanao! Na pindi unapoona tabia tofauti basi usisite kukaa nae na kumuelewesha na kumsaidia!

10. Badala ya kutoa adhabu akikosea Toa zawadi anapofanya vizuri!! Hii ni mbinu ya mwisho nzuri! Kwa wale wazazi ambao wamekuwa na tabia ya kutoa adhabu Kali kwa watoto wanapokosea basi badili! Anza kwa kumpongeza anapofanya vizuri! Mfano umesafiri kwa wiki kadhaa unaporudi nyumbani mwambie mtoto kuwa unampongeza kwa kuwa mtoto mtii kwa kusaidia kazi ndogo ndogo za nyumbani, kuwahi nyumbani n.k, unaweza pia kumwambia mtoto utampa zawadi Fulani akishika nafasi Fulani katika Darasa lake, badala ya kumuadhibu anapofeli! Kwa kuendelea kumpa motisha anapofanya vizuri basi Tabia hiyo njema inaendelea zaidi!

MWISHO
Lazima tukubali kuwa Dunia inabadilika kwa kasi mzazi ukubali kubadilika na kuongoza watoto kwa uhalisia badala ya hisia..

Tukumbuke kuwa mzazi ni mtoto Mzee! Kwa maana kuwa sehemu zote anazopitia mtoto wewe mzazi umepitia na Kwa hivyo una nafasi kubwa ya kumsaidia mtoto wako ikibidi asipitie mambo mabaya ambayo wewe umepitia!
Daima mkumbushe mwanao kuwa
"KICHAA ANACHEKESHA SANA KAMA HATOKEI KWENYE FAMILIA YENU!"

Asanteni

Najibu maswali kwenye comments
Nzuri
Nimependa
Shukrani
 
Wakuu nimerudi Tena katika Story of change,

Naomba Leo niwashirikishe mbinu nzuri za kuwalea watoto katika kipindi hiki Cha utanadawazi!

Kwanza nikiri wazi Mimi ni mzazi na mwalimu pia, kwahiyo haya ninayoshauri ni mambo ambayo Binafsi nimeyaona yakifanya kazi kwa ufanisi mkubwa! Kabla sijatoa hizi mbinu hebu tuone kwanza wazazi wengi wanakosea ama kukwama wapi katika kulea watoto!

1. Kuwafanya watoto waogope kufanya makosa kwa kuwa wataadhibiwa!

Naam wazazi wengi huwaambia watoto ole wao wafanye hiki au kile watakoma! Na kweli wanapofanya hivyo walivyoambiwa wasifanye basi wanakoma kweli! Hili ni kosa! Nitasema hapo baadae

2. Kuamini kuwa Kuna mambo ambayo mtoto hajui na hapaswi kujua!!
Wazazi wengi hudhani kuwa watoto wao Kuna mambo hawajui mfano mambo ya mapenzi, uvutaji, kuangalia picha za ngono n.k

Na ndipo siku mzazi anaambiwa mwanae anafanya hiki au kile basi anapata presha anaanguka na kufa! Kwakuwa hakufiria kuwa mwanae anajua jambo Hilo au hata kulifanya.

3. Kutokujua watoto wake kwa undani , tabia zao na kile wanachopendelea ama wasichopenda! Ni ajabu sana baadhi ya wazazi hawajui watoto wao wanapendelea mambo gani na wakati mwingine hata hawajui hisia za watoto wao na kuwalazimisha wafanye mambo ambayo watoto hawayataki na mwishowe wanakuwa disappointed ! Hujawahi kuona mtoto anafanya jambo kwa Siri chuoni analopenda lakini wazazi wanajua yupo anasoma au kufanya jambo Fulani! Na mwishowe wanabaki kushangaa!

Baada ya kuona hayo baadhi ya makosa sasa tuanze na namna Bora ya kuishi na Hawa watoto wa kisasa

1. Mfanye mtoto ajue faida na hasara ya anachokifanya kuliko tu kumwambia ukifanya hiki utanikoma! Mfano kama una bint amefikia umri wa kuvunja ungo Kaa nae kama mzazi mwambie wazi wazi kuwa akifanya mapenzi anaweza kupata ujauzito au magonjwa ya zinaa na pia akipata mimba anaweza kushindwa kutimiza ndoto Kwa wakati husika, lakini pia anaweza kupata madhara wakati wa kujifungua kwakuwa viungo vyake Bado havijakomaa! Hii ni nzuri kuliko tu kumwambia mtoto ole wako upate mimba!! Kumbuka unapomtishia mtoto asifanye jambo Fulani kwa Sababu Yako siku akiwa mbali na wewe au usipokuwepo basi atalifanya hujawahi kuona watoto wanaobanwa na wazazi wao jinsi wanavyojiachia wakiwa mbali na wazazi wao??

2. Mfanye mtoto ajue kuwa Kila anachokifanya Kina faida na hasara kwake yeye mwenyewe! Mara nyingi wazazi wamekuwa wakiwaambia watoto mfano wasome kwa bidii ili waje kuwasaidia ndugu, wadogo zao n.k lakini usahihi ni kumuandaa mtoto kuja kujisaidia mwenyewe! Na hii itamjengea uangalizi wa kufanya mambo bila hata uangalizi! Mwambie mtoto wazi wazi hasara za kutokusoma kwa bidii ikiwezekana Mpe mifano hai na faida zake.. mwambie akitumia muda mwingi kwenye tamthilia anapoteza nini kuliko tu kumwambia sitaki kukuona kwenye TV

3. Mjue mtoto wako vyema! Mwalimu wa kwanza ni wewe mzazi tambua mambo gani ambayo mwanao anaweza kuyafanya, tambua vipaji vyake na uwezo wake na udhaifu wake! Kuna watu wamelazimisha watoto wao kuwa madaktari kumbe wangeweza kuwa waigizaji wazuri! Kumbe wangekuwa mainjinia wazuri n.k
Mzazi mjue mtoto wako na umsapoti!

4 . Usimfiche mtoto kuhusu afya ya uzazi, usipomwambia ukweli Kuna watu watamwambia Tena pengine kwa ubaya! Una mtoto wa kike mwambie yeye ni mzuri! Anavutia na anaweza kutongozwa na wanaume kwa kumlaghai na mambo gani ya kufanya , Kuna wazazi hapa ukiwauliza wameongea lini na watoto wao utashangaa!!

5. Jaribu kwa kadri uwezavyo kujihadhari na tabia zako mbaya mbele ya watoto! Kwamfano kama mke na mume mna ugomvi basi jitahidini kuumaliza chumbani kwenu na watoto wasijue! Kama una mchepuko wako usije kufanya kosa kuuleta nyumbani kisa mwenza wako hayupo! Lakini kama watoto wapo hata kama ni wadogo kwa umri lakini Kuna kitu watajifunza kutoka kwako! Kama una tabia za ulevi na usingependa watoto wako wawe walevi kama wewe basi usinywe na kulewa mbele Yao! Kitaalamu watoto wanajifunza kwanza kwa kuona kwa wazazi wao ndipo huiga kile ambacho wazazi hufanya! Hivyo mambo unayofanya Yana athari kubwa sana Kwa watoto wako.. chanya au hasi!!

6. Mwache mtoto ajifunze kupitia makosa yake! Watoto kwa Namna walivyo na sisi sote tulipitia utoto , kufanya makosa ni sehemu ya ukuaji! Hivyo mtoto anapofanya kosa badala ya kumhukumu na kumkumbusha Kila mara kosa lake ni vyema kumpa nafasi zaidi ya kujifunza kupitia Hilo kosa lake! Unaweza pia kutumia kama kielelezo na sababu ya wewe kukaa nae na kumshauri namna Bora ya kufanya vizuri wakati ujao! Watoto wanafanya vizuri sana wakiaminiwa na kupewa nafasi ya pili!

7. Mzoeze mtoto wako kuishi kutokana na Hali na mazingira ya kipato chako! Kamwe usimpe mtoto Kila kitu ambacho analilia! Mfanye mtoto aridhike na maisha ya kwao, lakini pia aelewe kuwa unafanya Kila uwezavyo kuwatunza vizuri! Hapa simaanishi mzazi uwe bahili! Hapana, Bali mfanye mtoto akubali maisha halisi ya kwao!

8. Nenda na mtoto wako sehemu Yako ya kazi angalau mara moja kwa mwaka, kama wewe ni mkulima basi angalau nenda nae shamba mwanao, hata kama hatashika jembe lakini angalau ataona wapi pesa inapatikana, kama umeajiriwa ofisini basi nenda nae, haijalishi ni shughuli Gani unafanya kama ni ya halali basi wewe mpeleke mtoto aone! Kuna watoto wengi hawajui shughuli wanazofanya wazazi wao na wamekuwa watu wa kupokea zawadi tu Kila mara wazazi wanaporudi, hata hivyo Kuna namna inamjenga mtoto akijua kile mzazi anafanya, ushawahi kuulizwa na mtoto kuhusu kazi Yako? Basi usiishie kumjibu Bali nenda nae kabisa!

9. Chunguza na jua marafiki wa mtoto wako hii itakusaidia kujua tabia ya mtoto wako! Hata kama Kuna tabia ambazo mwanao anakuficha basi kupitia tabia za marafiki zake basi unaweza kujua kwa urahisi tabia ya mwanao! Na pindi unapoona tabia tofauti basi usisite kukaa nae na kumuelewesha na kumsaidia!

10. Badala ya kutoa adhabu akikosea Toa zawadi anapofanya vizuri!! Hii ni mbinu ya mwisho nzuri! Kwa wale wazazi ambao wamekuwa na tabia ya kutoa adhabu Kali kwa watoto wanapokosea basi badili! Anza kwa kumpongeza anapofanya vizuri! Mfano umesafiri kwa wiki kadhaa unaporudi nyumbani mwambie mtoto kuwa unampongeza kwa kuwa mtoto mtii kwa kusaidia kazi ndogo ndogo za nyumbani, kuwahi nyumbani n.k, unaweza pia kumwambia mtoto utampa zawadi Fulani akishika nafasi Fulani katika Darasa lake, badala ya kumuadhibu anapofeli! Kwa kuendelea kumpa motisha anapofanya vizuri basi Tabia hiyo njema inaendelea zaidi!

MWISHO
Lazima tukubali kuwa Dunia inabadilika kwa kasi mzazi ukubali kubadilika na kuongoza watoto kwa uhalisia badala ya hisia..

Tukumbuke kuwa mzazi ni mtoto Mzee! Kwa maana kuwa sehemu zote anazopitia mtoto wewe mzazi umepitia na Kwa hivyo una nafasi kubwa ya kumsaidia mtoto wako ikibidi asipitie mambo mabaya ambayo wewe umepitia!
Daima mkumbushe mwanao kuwa
"KICHAA ANACHEKESHA SANA KAMA HATOKEI KWENYE FAMILIA YENU!"

Asanteni

Najibu maswali kwenye comments
Nikuulize kaswali ka kizushi Mh Mwalimu wetu.

Kwa mfano watoto wakajificha wakavua nguo wakaifanya kama watu wazima. Hapo utasema uwaache wafanye??

Binafsi nimeona wazazi wanaoishi chumba kimoja na watoto.. wakifika shule wanaitana na kurudia kile kitendo...
 
Nikuulize kaswali ka kizushi Mh Mwalimu wetu.

Kwa mfano watoto wakajificha wakavua nguo wakaifanya kama watu wazima. Hapo utasema uwaache wafanye??

Binafsi nimeona wazazi wanaoishi chumba kimoja na watoto.. wakifika shule wanaitana na kurudia kile kitendo...
Okay kama umesoma Kuna sehemu nimeandika kuwa mwambie mtoto wako athari za kufanya hicho kitu! Kwasababu kumbuka umepata tu bahati ya "kuwafuma wakifanya" je umejiuliza ukiwa haupo Yale ambayo wanafanya??

Sasa kwa kukusaidia kutokana na swali lako kwanza usifanye mapenzi mbele ya mtoto hata kama amelala! Kama ukifanya mapenzi watoto wakaona lazima wataiga tu!

Okay sasa kama umewafuma wanafanya je uwache 'wanyanduane?'
Jibu rahisi,
Wao wameACT wewe React! Kwasababu umewaona!!

Narudia Tena sababu ya wewe kuwadhibu ni kwasababu umewaona!
Karibu kwa swali
 
Okay kama umesoma Kuna sehemu nimeandika kuwa mwambie mtoto wako athari za kufanya hicho kitu! Kwasababu kumbuka umepata tu bahati ya "kuwafuma wakifanya" je umejiuliza ukiwa haupo Yale ambayo wanafanya??

Sasa kwa kukusaidia kutokana na swali lako kwanza usifanye mapenzi mbele ya mtoto hata kama amelala! Kama ukifanya mapenzi watoto wakaona lazima wataiga tu!

Okay sasa kama umewafuma wanafanya je uwache 'wanyanduane?'
Jibu rahisi,
Wao wameACT wewe React! Kwasababu umewaona!!

Narudia Tena sababu ya wewe kuwadhibu ni kwasababu umewaona!
Karibu kwa swali
🙏🙏🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom