Nikukumbushe
JF-Expert Member
- Jun 4, 2013
- 2,602
- 408
Hili liko wazi. Halikitaji elimu hata ya ngazi ya cheti kulijua hili.
Namhurumia sana JK,ana wakati mgumu sana. Anashindwa nani awe rais wa JMT kupitia chama chake. Hii ni hatari sana kwa rais wa nchi kuwa njia panda. Rais anakosa hata washauri. Mawaziri wake wametangaza kuutaka urais. Nani atamshauri. Washauri wake hasa makini wanautaka urais.
Miongoni mwao ni Steven Wassira,Mizengo Pinda,Magufuli,Samwel Sitta,Benard Membe,Mwandosya.
Wengine ni manaibu waziri,akiwemo January makamba,Mwigulu Nchemba. Nani atamshauri rais huyu?.
Pia,wapo waliojiuzulu kwa kashfa akiwemo Shamsi Vuai Nahodha,EL,Emmanuel Nchimbi.
Mwaka huu CCM kazi ipo. CCM haiwezi kuvuka salama,haiwezekani kubalance haya yote. Mitihani nii ni misumali ya moto kwa CCM
1.Makundi ya urais. Ni moto unaosubiri kuwaka. Ni suala la muda. Hapa nashauri kitu kimoja,ni bora ccm wachukue maamuzi magumu sasa sio wavute muda mpaka uchaguzi ukaribie. Muda huu wanaweza kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza japo wamechelewa. Hii ni bomu. Ni zaidi ya lile la Yiroshima Nagasaki. Hapa ni suala la muda. Watakuja kukimbiana.
2.Migomo iliyotokea. Huu ni moto mwingine,migomo hii imeathiri wananchi moja kwa moja ukiwemo mgomo wa madereva na madaktari.
3.Ahadi ambazo hazitekelezeki. Mwaka 2010 walitoa ahadi chungu nzima. Ahadi hizi ni mwiba kwa CCM.
4. Utayari wa wananchi kupokea mabadiliko. Wananchi wamepokea mabadiliko kwa kiasi kikubwa. Hili limechangiwa na elimu ya uraia. Zile propaganda za nani katoka wapi,anasali wapi sasa they are no longer active.
5.UKAWA. Huu umoja ni hatari kwa CCM. Kwani hawajawahi hata kufikiria juu ya hili. Zile mbinu za wagawe ili uwatawale now ni historia.
6.Mahakama maalumu. Hapa CCM sio kuwa na mtihani tu,bali wanajuta. Kwa nini,kuna Trade off. Hapa CCM haiwezi kufavour upande mmoja na ikabaki salama. Ikumbukwe kuwa ilani ya CCM inazungumzia uanzishwaji wa mahakama ya hiyo. Wakiianzisha mahakama hiyo watakuwa wameanzisha Vita ya wao na upande fulani. Wasipoianzishe bado ni hatari zaidi.
Ni hayo tu.
Namhurumia sana JK,ana wakati mgumu sana. Anashindwa nani awe rais wa JMT kupitia chama chake. Hii ni hatari sana kwa rais wa nchi kuwa njia panda. Rais anakosa hata washauri. Mawaziri wake wametangaza kuutaka urais. Nani atamshauri. Washauri wake hasa makini wanautaka urais.
Miongoni mwao ni Steven Wassira,Mizengo Pinda,Magufuli,Samwel Sitta,Benard Membe,Mwandosya.
Wengine ni manaibu waziri,akiwemo January makamba,Mwigulu Nchemba. Nani atamshauri rais huyu?.
Pia,wapo waliojiuzulu kwa kashfa akiwemo Shamsi Vuai Nahodha,EL,Emmanuel Nchimbi.
Mwaka huu CCM kazi ipo. CCM haiwezi kuvuka salama,haiwezekani kubalance haya yote. Mitihani nii ni misumali ya moto kwa CCM
1.Makundi ya urais. Ni moto unaosubiri kuwaka. Ni suala la muda. Hapa nashauri kitu kimoja,ni bora ccm wachukue maamuzi magumu sasa sio wavute muda mpaka uchaguzi ukaribie. Muda huu wanaweza kukabiliana na changamoto zitakazojitokeza japo wamechelewa. Hii ni bomu. Ni zaidi ya lile la Yiroshima Nagasaki. Hapa ni suala la muda. Watakuja kukimbiana.
2.Migomo iliyotokea. Huu ni moto mwingine,migomo hii imeathiri wananchi moja kwa moja ukiwemo mgomo wa madereva na madaktari.
3.Ahadi ambazo hazitekelezeki. Mwaka 2010 walitoa ahadi chungu nzima. Ahadi hizi ni mwiba kwa CCM.
4. Utayari wa wananchi kupokea mabadiliko. Wananchi wamepokea mabadiliko kwa kiasi kikubwa. Hili limechangiwa na elimu ya uraia. Zile propaganda za nani katoka wapi,anasali wapi sasa they are no longer active.
5.UKAWA. Huu umoja ni hatari kwa CCM. Kwani hawajawahi hata kufikiria juu ya hili. Zile mbinu za wagawe ili uwatawale now ni historia.
6.Mahakama maalumu. Hapa CCM sio kuwa na mtihani tu,bali wanajuta. Kwa nini,kuna Trade off. Hapa CCM haiwezi kufavour upande mmoja na ikabaki salama. Ikumbukwe kuwa ilani ya CCM inazungumzia uanzishwaji wa mahakama ya hiyo. Wakiianzisha mahakama hiyo watakuwa wameanzisha Vita ya wao na upande fulani. Wasipoianzishe bado ni hatari zaidi.
Ni hayo tu.