Namba ya simu nisiyoifahamu imesajiliwa kwa kutumia kitambulisho changu

Pacbig

JF-Expert Member
Oct 15, 2017
1,095
2,079
Wadau poleni na pongezi kwa mapambano ya kimaisha ya kila siku.

Nikiwa katika harakati za kutuma maombi ya sensa. Nilipomaliza kujaza detail na kuzituma, taarifa kutoka kwenye mfumo ikasema namba yangu tayari imeshatumika (namba ni ya vodacom). Sikuwaza sana maana nilijua shida ni nini. ( sitalisemea hili ili kupunguza maelezo)

Sasa ikabidi nitumie namba nyingine ya tigo. Lakini hii namba nilikuwa sijaikaliri ikabidi nibonyeze *106# kisha nikaingiza namba yangu ya Nida ili nizione namba zilizosajiliwa kupitia hiyo namba yangu ya Nida.

Mimi nina sim card mbili tu ya Vodacom na Tigo, cha kushangaza nikakuta nina namba mbili za Vodacom zilizosajiliwa kwa kutumia namba yangu ya Nida. Namba ya kwanza ndio ninayoitumia, lakini namba ya pili siifahamu.

Nimewasiliana na Vodacom wameniambia nitembelee duka lao lililo karibu na kesho nitaenda. Ila kuna maswali najiuliza.

1. Inawezekanaje mtu akasajili simcard kwa kutumia utambulisho wa mtu mwingine?

2.unaposajili huwa tunaweka alama za vidole ili kuthibitisha kama ni wewe kweli. Sasa hata kama kuna mtu aliipata namba yangu, Alama zangu za vidole alizitoa wapi?

Karibuni kwa majibu na ushauri.

NB nimeipigia hiyo namba inapatikana na nimeongea nae. Nimejaribu kumuuliza hiyo namba aliisajili wapi, lakini hajatoa majibu ya kueleweka.
 
Sometimes kule ulikosajilia walikuibia kopi, au namna nyingine tu, la maana ni kwenda kusajili namba yako na kutoa hiyo nyingine,

Feki zipo za kila aina
 
Wadau poleni na pongezi kwa mapambano ya kimaisha ya kila siku.

Nikiwa katika harakati za kutuma maombi ya sensa. Nilipomaliza kujaza detail na kuzituma, taarifa kutoka kwenye mfumo ikasema namba yangu tayari imeshatumika (namba ni ya vodacom). Sikuwaza sana maana nilijua shida ni nini. ( sitalisemea hili ili kupunguza maelezo)

Sasa ikabidi nitumie namba nyingine ya tigo. Lakini hii namba nilikuwa sijaikaliri ikabidi nibonyeze *106# kisha nikaingiza namba yangu ya Nida ili nizione namba zilizosajiliwa kupitia hiyo namba yangu ya Nida.

Mimi nina sim card mbili tu ya Vodacom na Tigo, cha kushangaza nikakuta nina namba mbili za Vodacom zilizosajiliwa kwa kutumia namba yangu ya Nida. Namba ya kwanza ndio ninayoitumia, lakini namba ya pili siifahamu.

Nimewasiliana na Vodacom wameniambia nitembelee duka lao lililo karibu na kesho nitaenda. Ila kuna maswali najiuliza.

1. Inawezekanaje mtu akasajili simcard kwa kutumia utambulisho wa mtu mwingine?

2.unaposajili huwa tunaweka alama za vidole ili kuthibitisha kama ni wewe kweli. Sasa hata kama kuna mtu aliipata namba yangu, Alama zangu za vidole alizitoa wapi?

Karibuni kwa majibu na ushauri.

NB nimeipigia hiyo namba inapatikana na nimeongea nae. Nimejaribu kumuuliza hiyo namba aliisajili wapi, lakini hajatoa majibu ya kueleweka.
Hata nami, ilitokea hivyo. Nilivyofuatilia, nikagundua kuwa, aliyekuwa anasajiri line yangu, alisajiri na line zingine mbili, ambazo ni zake, kwa kutumia detail zangu. Line hizo, huwa wanaziuza kwa wateja ambao hawana vitambulisho, kwa kumfahamisha kuwa zimeshasajiriwa kwa alama za vidole.
Niliwapigia huduma kwa wateja, wakaniambia niende kwenye ofisi yao,ambako walizifuta hizo line zisizo zangu!
 
Hata nami, ilitokea hivyo. Nilivyofuatilia, nikagundua kuwa, aliyekuwa anasajiri line yangu, alisajiri na line zingine mbili, ambazo ni zake, kwa kutumia detail zangu. Line hizo, huwa wanaziuza kwa wateja ambao hawana vitambulisho, kwa kumfahamisha kuwa zimeshasajiriwa kwa alama za vidole.
Niliwapigia huduma kwa wateja, wakaniambia niende kwenye ofisi yao,ambako walizifuta hizo line zisizo zangu!
Kama ndio hivyo basi nimeshamfahamu wakala aliyefanya huo ujinga.

Vipi niki-mreport polisi?
 
Kama ndio hivyo basi nimeshamfahamu wakala aliyefanya huo ujinga.

Vipi niki-mreport polisi?
Haina haja nenda kajipatie mpunga mrefu kwa kumtisha maana hali yenyewe hiii unaijua ni bora kupata hela kuliko kumsotesha huko alaf utoe hela tena wewe
 
Wadau poleni na pongezi kwa mapambano ya kimaisha ya kila siku.

Nikiwa katika harakati za kutuma maombi ya sensa. Nilipomaliza kujaza detail na kuzituma, taarifa kutoka kwenye mfumo ikasema namba yangu tayari imeshatumika (namba ni ya vodacom). Sikuwaza sana maana nilijua shida ni nini. ( sitalisemea hili ili kupunguza maelezo)

Sasa ikabidi nitumie namba nyingine ya tigo. Lakini hii namba nilikuwa sijaikaliri ikabidi nibonyeze *106# kisha nikaingiza namba yangu ya Nida ili nizione namba zilizosajiliwa kupitia hiyo namba yangu ya Nida.

Mimi nina sim card mbili tu ya Vodacom na Tigo, cha kushangaza nikakuta nina namba mbili za Vodacom zilizosajiliwa kwa kutumia namba yangu ya Nida. Namba ya kwanza ndio ninayoitumia, lakini namba ya pili siifahamu.

Nimewasiliana na Vodacom wameniambia nitembelee duka lao lililo karibu na kesho nitaenda. Ila kuna maswali najiuliza.

1. Inawezekanaje mtu akasajili simcard kwa kutumia utambulisho wa mtu mwingine?

2.unaposajili huwa tunaweka alama za vidole ili kuthibitisha kama ni wewe kweli. Sasa hata kama kuna mtu aliipata namba yangu, Alama zangu za vidole alizitoa wapi?

Karibuni kwa majibu na ushauri.

NB nimeipigia hiyo namba inapatikana na nimeongea nae. Nimejaribu kumuuliza hiyo namba aliisajili wapi, lakini hajatoa majibu ya kueleweka.
Wale mawakala wanaopita mitaani wanatabia mbovu
Ukiwa unasajili laini ukieka kidole wanakwambia imekataa halafu anachukua line nyingine unaeka kidole tena
Kumbe ile laini ya kwanza ilikubali na inakuwa imesajiliwa kwa jina lako

Wanaendaga kuziuza kwa wateja wasiokuwa na vitambulisho
 
Je utajuaje kama umetumika kusajili laini nyengine bila kujua
 
Hata nami, ilitokea hivyo. Nilivyofuatilia, nikagundua kuwa, aliyekuwa anasajiri line yangu, alisajiri na line zingine mbili, ambazo ni zake, kwa kutumia detail zangu. Line hizo, huwa wanaziuza kwa wateja ambao hawana vitambulisho, kwa kumfahamisha kuwa zimeshasajiriwa kwa alama za vidole.
Niliwapigia huduma kwa wateja, wakaniambia niende kwenye ofisi yao,ambako walizifuta hizo line zisizo zangu!
Ndio michezo yao mawakala. Wanakera sana.
 
Back
Top Bottom