Namba 666 kitabu cha UFUNUO 13:18 si chapa ya mpinga Kristo kwa Biblia kama wasemavyo Wasabato

Kamwambie Padre wako hatudanganyiki.

666 ni mamlaka ..sio MTU mmoja....

Yaan Ellen G White alazamishe watu waabudu sanamu?? Awatie kifungoni na kuwaua masikini na Matajiri ,watumwa nawalio huru sababu tu hawana chapa ya mnyama .

Haaaaaaaaaaaa Acheni, Ujinga...666 ni alama ya Mpinga kristo hesabu ya Maneno "Vicarius Filii Dei " ...... Mwana wa Mungu....ambayo Papa ktk kofia yake miaka ile iliandikwa hayo na alisimama km mwana wa Mungu hapa Duniani.

Endeleen kudanganya waumini wenu kwa kutowaruhusu kuja na Biblia Kanisani...

Matokeo yake waumini wa Catholic ndio waumini pekee hapa Duniani ,WASOJUA MAANDIKO ...kwa habari za kiroho mpo na ombwe kubwa la Maandiko ..

Habari njema zitahubiliwa Duniani kote ili kua ushuhuda !!!.View attachment 1411148
Kwahyo unamaanisha mtume Simon Petro ni mpinga Kristu?
 
Anaandika Baba Titus Amigu: (Padri na gwiji/mwamba wa Theolojia).

Mfuatilie usome ujichotee maarifa upate ukweli na kisha ukuweke huru.. .
Wakatoliki hawabahatishi haya mambo..

NAMBA 666 AU 616 ILIYOANDIKWA KWENYE UFU 13:18 HAIMHUSU PAPA ISIPOKUWA ELLEN GOULD WHITE

Imbeni pamoja nami ALLELUYA! Kwa nini? Kwa sababu Mungu amenitendea makuu. Amenisaidia kukitegua kitendawili cha karibu karne mbili sasa, yaani kitendawili cha namba 666. Kwa muda mrefu tangu enzi za akina ELLEN GOULD WHITE, yaani miaka ile ya 1846, namba 666 ya katika Ufu 13:18 imekuwa ikielekezwa kwa majungu na matusi kwa Baba Mtakatifu. Ndugu zanguni, tulikuwa tunazugwa tu. Kumbe, siri ni kwamba ilikuwa inamwelekea mwenyewe aliyekuwa anaelekeza mashambulizi na matusi kwa Baba Mtakatifu, yaani ELLEN GOULD WHITE.

Nina furaha kubwa sana. Nawaalikeni mfurahi pamoja nami. Binafsi, nilikuwa napata taabu sana kujaribu kufumbua kitendawili hicho. Lakini, wakati huo huo, nilikuwa najiuliza kwa nini mashambulizi kwa Baba Mtakatifu ni makali hivyo? Kumbe, sasa tumefumbuliwa. Yote yalikuwa ni mbinu ya kutupoteza watu “maboya” tusijue kwamba namba inamwelekea mwenyewe anayetukana. Kumbe, ilikuwa ni mbinu ile ile ya mwizi kupiga kelele za “Mwizi, mwizi, mwizi huyo!” kusudi watu wamfukuze mtu mwingine na siyo yeye mwenyewe.

Acheni niwakumbusheni mambo. Nadhani nyote mna habari na mashtaka maarufu sana dhidi ya Wakatoliki kwamba namba 666 au 616 inamhusu kiongozi wetu mkuu yaani Papa au Baba Mtakatifu na kwamba namba hiyo imeandikwa kwenye mavazi yake na kofia yake. Zaidi ya hapo kuna madai kwamba namba hii ipo pia katika kompyuta na satelite. Leo nataka niwafunulieni mambo yalivyo.

Hii ni Mada ya Lugha na Hesabu Kidogo
Vijana wangu msishtuke na kuhangaika. Mada hii itahusisha herufi za Kiebrania na Kigiriki lakini zitakuwa chache tu nanyi mtaelewa yote nitakayoandika kwani ni masuala rahisi kuyafuatilia. (Kwa bahati mbaya herufi za Kigiriki zinakataa humu). Papo hapo, kutakuwa na hesabu. Hata hizo hazitawahangaisheni kwani ni hesabu za kujumlisha tu. Leo kumbukeni pia hesabu za Shule ya Msingi tulipokuwa tunatumia tarakimu za Kilatini, kwa mfano, I = 1, V = 5, X= 10, L = 50, C= 100, D = 500 na M = 1000.
Ili tuelewane, nitaanza na historia, kishapo nitakwenda nje ya Biblia ilikohamishiwa namba 666.

Mama ni Historia
Hebu nianze na jibu fupi linalolingana na historia. Wayahudi hujumlisha thamani ya kitarakimu majina ya watu na maneno mbalimbali na kuzaa namba mbalimbali. Kuhesabu kwa namna hii huitwa gematria nako kumetumika katika Ufu 13:18 na kuzaa namba 666 au katika nakala zingine za Biblia namba 616. Swali kubwa ni je, namba hiyo inamhusu nani? Ukweli ni kwamba namba 666 au 616 haimhusu Papa au Baba Mtakatifu hata kidogo. Tena haikuandikwa katika mavazi ya Papa na wala haimo katika kompyuta ama satelite.

Ukweli, kibiblia na kihistoria, ni kwamba namba hiyo ilimhusu na bado inamhusu kiongozi wa dola ya Kirumi zamani zile, yaani Kaisari Nero. Basi, namba 666 au 616 ndiyo hesabu ya jina la Nero aliyekuwa akiwadhulumu Wakristo katika karne ya kwanza ya Ukristo. Hesabu hiyo inapatikana kwa kukokotoa kigematria maneno NERON KAISAR (kwa Kiebrania - נרון קסר) au NERO KAISAR (kwa Kiebrania - נרו קסר) na KAISAR THEOS (kwa Kigiriki).

Jibu refu: Hakuna mahali po pote katika Biblia ambapo msomaji ameombwa kutumia akili isipokuwa hapa. Kwa kuwa ili kuipata hesabu hii kulihitaji kupiga hesabu, wasomaji wote wa kifungu kile walialikwa kupiga hesabu, gematria. Ndipo imeandikwa “Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili na aihesabu hesabu” (Ufu 13:18). Kumbe, kinyume na matumizi ya akili, hapa ndipo mahala wasomaji kadha wa kadha wasipotumia akili yoyote katika kusoma isipokuwa majungu na usingiziaji.

Ndugu yangu, wapo watu chungu nzima wanaoeneza tafsiri kwamba namba 666 au 616 inamhusu Baba Mtakatifu na imeandikwa kwenye mavazi yake kama nilivyosema hapo juu (rejea Ufu 13:18, 15:2). Je, mafundisho hayo yana ukweli? Najijibu mwenyewe: Si ya kweli.

Tusisahau, kitabu cha Ufunuo wa Yohane kina mazingira yake ya kihistoria ambayo ni muhimu katika kuielewa sura ya 13. Mazingira hayo ni ya historia ya Dola ya Kirumi. Wakristo walipokuwa wakidhulumiwa na dola hiyo, mwandishi wa kitabu cha Ufunuo alichukua kalamu na kuandika ili kuwaliwaza ndugu zake aliokuwa akiteseka pamoja nao (rejea Ufu 1:9). Basi, katika kuandika akatumia lugha ya mafumbo ili watesi wasifahamu wanayosemwa. Ndicho kisa, basi, joka kuu lenye pembe na kadhalika linamaanisha Dola ya Kirumi. Mkubwa wa dola hiyo naye akapewa jina la kupanga au jina la kifumbo kwa mtindo wa kucheza na namba za jina lake (gematria).

Ukitaka kupata picha kidogo ya haya, chukulia mfano wa vitabu vya marehemu Shaban Robert. Yeye aliandika mashairi mengi ya kuwatia watu hamasa wapiganie uhuru. Katika mashairi hayo, wananchi anawaita, mathalani, siafu na wakoloni nyoka. Hao siafu wanakazana kumdhuru nyoka. Aidha, kitabu chake cha Kusadikika ni kitabu cha fumbo kinachofumbia hali ya mambo katika hewa ya kikoloni. Kwa hakika wakoloni hawakuambulia lolote katika mashairi na fasihi ya Shaban Robert. Kinyume chao, wananchi walielewa mada husika na “kuwaacha kwenye mataa” wakoloni.

Ndivyo inavyotokea shuleni, mwalimu mbaya kupangwa jina ambalo mwenyewe halijui hata kama litatajwa mbele yake.
Upangaji wa jina la mtu kwa kutumia hesabu ya herufi za jina lake mwenyewe ulikuwa mtindo maarufu wa marabi na ulijulikana kama gematria. Ufu 13:18, si mahali pa kwanza kutumia gematria hata namba kumi na nne ya vizazi vilivyotajwa katika Mt 1:17 ni gematria ya jina Daudi (דוד) kwani d + w + d ni 6 + 4 + 6 = 14. Sasa ni nani katika karne ya kwanza aliyekuwa adui wa Wakristo na jina lake kigematria lilizaa namba 666 au 616? Hili ndilo swali la kuulizana. Alikuwa KAISARI NERO.

Tukitafsiri Biblia kwa usahihi huu, mtesi wa walengwa wa kitabu, aliyekuwa akifumbiwa katika 13:18 kwa kuhesabu jina lake kigematria, hawezi kuwa mtu wa karne ya tano au ya ishirini na moja. Walengwa walikuwa ni Wakristo wa karne ya kwanza na adui yao alikuwa akiishi nao kwa wakati huo huo. Basi, nani alikuwa mtesi maarufu katika mazingira ya karne ya kwanza? Wakati ule alikuwa Kaisari Nero ama Kaisari fulani aliyejidai kuwa Mungu na huyo ndiye kigematria jina lake linazaa namba 666 au 616.

Basi, gematria ikitumika kwa konsonanti za Kiebrania: נרון קסר - NERON KAISAR (yaani Kaisari Neron) au kwa maneno ya Kigiriki: KAISAR THEOS (yaani Kaisari Mungu) tunapata pasipo kuzunguka zunguka namba 666 au 616. Tazama hesabu zenyewe zinavyofanyika. (נרון קסר) r s q n w r n = 200 + 60 + 100 + 50 + 6 + 200 + 50 = 666.
k a i s a r th e o s = 20 + 1 + 10 + 200 + 1 + 100 + 9 + 5 + 70 + 200 = 616.

Angalia vyema. Hii tafsiri ya ‘KAISAR THEOS’ yaani ‘Mungu Kaisari’ ndiyo inayorejewa kwenye Biblia zenye kuandika jumla ya namba 616. Lakini vile vile 616 iliweza kupatikana kwa kuondoa “n” ya mwisho kwenye jina נרון (n w r n) katika Kiebrania. Kwa Wakristo, namba 666 ilipomtaja Neron ilisema pia kwamba ni MPINGA KRISTO kwani alikuwa kinyume cha utimilifu. Kinambari, utimilifu ni namba 777. Kumbe, yeye Kaisari Nero ni upungufu kwani hesabu yake ni 666 ambayo ni 777 kutoa 111.

Basi, kwa kuzingatia mazingira ya kitabu cha Ufunuo namba 666 au 616 haiwezi kusimama kwa ajili ya jina lingine kama Baba Mtakatifu, Mtume Mohamed au Mussolini. Haya ni baadhi ya majina wanayolazimisha watu yafanye hesabu ya 666. Na, kwa hakika, namba hiyo haimo katika mavazi wala kofia (mitra) ya Baba Mtakatifu. Hakuna mtu yeyote anayeweza kuonesha vazi hilo au kofia hiyo kwa ushahidi. Kwani ni vazi gani au kofia ipi? Basi, kama tunautafuta uzima wa milele, aheri tuache majungu na uongo kama huu. Kama ni maandishi, ni mitra yake tu yenye herufi mbili A na W yaani alpha na omega (rejea Ufu 1:8,17).

Acha tuendelee. Wanaombambikizia Baba Mtakatifu namba 666 hudai kuikokotoa nambari hiyo katika majina matatu tofauti: jina la Kilatini VICARIUS FILII DEI (Kaimu wa Mwana wa Mungu), jina la Kigiriki LATEINOS (Mlatini) na jina la Kiebrania ROMIITH (רמיית - Mrumi). Majina hayo huhesabiwa na wanaombambikizia Baba Mtakatifu namba hiyo kama ifuatavyo:

VICARIUS FILII DEI = 5 + 1 + 100 + 0 + 0 + 1 + 5 + 0 + 0 + 1 + 50 + 1 + 1 + 500 + 0 + 1 = 666.
LATEINOS = 30 + 1 + 300 +5 + 10 + 50 + 70 + 200 = 666.

ROMIITH yaani th y y m w r = 400 + 10 + 10 + 40 + 6 + 200 = 666.

Ndugu zangu, kwa misingi halali ya kusoma Biblia hatuwezi kuyapokea majina haya bila kuyafanyia tahakiki ya kihistoria. Bila kurefusha mjadala, majina haya hayajapata kutumiwa na Baba Mtakatifu yeyote, katika historia ya Kanisa sembuse wakati wa karne ya kwanza Baada ya Kristo wakati ambao hata upapa wenyewe ulikuwa haujakua. Mapapa wa karne zile hawakuwa hatari kwa mtu yeyote. Na watu wasio hatari watapewaje majina ya kupanga na ya siri? Wale wasomaji wa kitabu cha Ufunuo wangelielewaje aya ngumu inayotaja kitu kisichojulikana kwa jina hilo? Wangelifanyaje gematria kwa kutumia majina wasiyoyajua?

Aya 13:18 ilizungumzia jina ambalo wasomaji walikuwa wakilijua kama jina la adui yao aliyekuwa akiwadhulumu na si majina ya ndoto au majungu ya karne ya 20 na 21 B.K. Zaidi ya hayo majina mengine yamelazimishwa kihesabu ili jumla ya kiherufi iwe 666. Kwa ushuhuda tazama U ilivyolazimishwa imaanishe tarakimu 5. Katika Kilatini 5 ni V na wala siyo U. Zaidi ya hayo, jina “MLATINI” kama lingelitumika wakati huo, wasomaji wangelielewa kuwataja wakoloni au askari wa kirumi ambao walikuwa wakitawala ulimwengu wa wakati ule.

Hali kadhalika, kama jina “MRUMI” lingelitumika wakati huo, wasomaji wangelielewa kuwataja wakoloni au askari wa kirumi ambao walikuwa wakitawala ulimwengu wa wakati ule. Kwa hoja hizi, majina hayo ya majungu ni ya tangu karne ya 16, Kanisa Katoliki lilipoanza kupingwa kwa ari mpya na uongozi wake kukataliwa.

Nadhani hadi hapa kila mwenye kutaka kujua anajua kwamba majina waliyobuni Wasabato hayatumiwi na Baba Mtakatifu yeyote. Na zaidi ya hayo ni majina ambayo mwandishi wa kitabu cha Ufunuo hakuwa hata na habari nayo katika karne ile ya kwanza B.K. kwa vile alivyokiandika kitabu chake kwa Kigiriki na wala si kwa Kiebrania au Kilatini. Kumbe, kwa kufanya hivyo Wasabato huwa wanainyonga historia na kukizungumzia kitabu cha Ufunuo nje ya muktadha wake wa kihistoria. Hili ni kosa la kusiganisha nyakati za kikalenda (kwa Kiingereza “anachronism”).

Basi, kwa heshima ya Maandiko Matakatifu, tutafsiri namba 666 au 616 kwa gematria asilia na tukomee hapo hapo. Tusiihamishe namba hiyo na kuwapachika watu wasio na hatia. Kufanya hivyo ni kujitowelesha majungu na ni dhambi isiyo na maana yo yote. Lakini, basi namba 666 imetolewa nje ya mazingira ya Biblia na ndipo ilipowekwa sasa. Nami nimefika hapo hapo.

Namba 666 Imehamishiwa Nje ya Biblia

Ni kituko lakini ndivyo ilivyo. Watu wengine hudai kwamba namba hiyo imeandikwa shingoni kwenye nguo za Papa. Huo ndio uongo na usingiziaji usio na aibu kwa sababu nguo hizo hakuna anayeweza kutuonesha wenziwe. Siku moja niliwahi kuambiwa na wainjilisti wawili kwamba namba 666 ipo kwenye bidhaa za siku hizi, yaani kwenye kifungashio, pale inapochorwa mistari mingi mifupi na mirefu na kuandikwa namba kwa chini, na kwa namna hiyo ipo pia kwenye satelite. Siku hiyo niliwakamata kutokujua nilipowadai wanioneshe mfano. Basi, wakaleta baadhi ya bidhaa za kisasa, wakaniambia niangalie ile mistari iliyochorwa katika kifungashio cha kila bidhaa. Hapo walionesha pia mistari miwili miwili inayojitokeza zaidi kwa chini (jambo ambalo si kweli kwa kila bidhaa). Basi, hapo ndipo walipodai kuna namba 666.

Kumbe, huu ulikuwa ujinga wao mkubwa. Ndugu yangu, mistari hiyo, ndiyo bei ya bidhaa hasa kwa zile zinazouzwa „“supermarket. Katika nchi zilizoendelea watu hawaandiki bei shilingi fulani au fulani wakabandika kwenye bidhaa. Badala yake ndiyo hiyo mistari, kadiri ilivyochorwa ndivyo mashine ya kupigia hesabu inavyotambua na kutofautisha bei za bidhaa ambazo mnunuzi amezifikisha kwenye “kaunta” ya kulipia manunuzi. Na tena bei hizo hazikuingizwa katika satelite; zilivyo nyingi hazihusishwi na satelite yoyote.

Basi, niliwaonya wainjilisti wale wasiwadanganye watu kwa kutumia ujinga wao wakati wenyewe pia hawajui mambo ya kisasa. Hatimaye, niliwaambia, kwa uongo wa namna ile, wao si wainjilisti kwani Injili ni Habari Njema ya ukombozi wetu uliotufikia kwa kifo na ufufuko wa Yesu Kristo na wala siyo namba 666 inayodaiwa kuandikwa kwenye nguo za Papa na kuingizwa kwenye satelite kwa njia ya michoro ya bidhaa za kisasa. Kwa kweli niliwaambia kwa kueneza uongo na kuwatia watu hofu kwa kuwatinga, hawakuwa mbali sana na moto wa milele kwa vile wanamtumikia Shetani aliye baba wa uongo. Hapo nikapata mwanya wa kuwaalika watubu kwa haraka. Lakini, badala ya kupokea mafundisho yangu walisema sina Roho Mtakatifu na kuondoka. Waliondoka na hawakurudi tena kwangu. Kumbe, niliwafuma katika kutokujua kwao, yaani ujinga wao. Samahani kwa simulizi hili; majadiliano yetu yaliacha kuwa ya Kikristo.

Safari Ndefu ya Kutegua Kitendawili cha Kale
Kwa vile madai ya kwamba namba 666 inamhusu Baba Mtakatifu yametutoa sote kutoka kwenye Biblia na kutupa kazi ya kumtafuta nani mwingine anaweza kuwa anatajwa na namba hiyo, nilichukua kalamu na kuanza kuchunguza maneno ya wanaotukana kama hayahusiki vile vile. Utafutaji wangu ulizaa matunda mwaka ule ule 1998. Nikategua kitendawili kwa kugundua kwamba kauli za Wasabato wenyewe zilikuwa ndiyo namba 666.

Nilifanyaje? Nilichukua kauli tatu: PONYA SIKU MUHIMU YA SABA (kwa Kiingereza CURE VITAL SEVENTH DAY, kwa Kilatini CURATUS VITALE SABBATA DIES) na WOKOVU, PONYA SIKU YA SABA (kwa Kiingereza SALVATION, CURE SEVENTH DAY, kwa Kilatini SALVUS, CURARE SABBATA DIES) na VUNJA, CHUKIA UPAPA (kwa Kiingereza DEAL AXE, VIE PAPACY). Nilistaajabu sana kuona ndiyo inakuja 666 ndipo mara moja nikaingiza ugunduzi wangu katika kitabu changu KISA CHA IMANI namba 1.

Ni kweli. Kauli mbiu za Wasabato ni namba hiyo hiyo 666. Angalia gematria inavyokwenda:
CURE VITAL SEVENTH DAY = 100 + 5 + 0 + 0 + 5 + 1+ 0 + 0 + 50 + 0 + 0 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 0 + 0 = 666
CURATUS VITALE SABBATA DIES = 100 + 5 + 0 + 0 + 0 + 5 + 0 + 5 + 1 + 0 + 0 + 50 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 1 + 0 + 0 = 666

SALVATION, CURE SEVENTH DAY = 0 + 0 + 50 + 5 + 0 + 0 + 1 + 0 + 0 + 100 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 0 + 0 = 666
SALVUS, CURARE SABBATA DIES = 0 + 0 + 50 + 5 + 5 + 0 + 100 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 1 + 0 + 0 = 666
DEAL AXE VIE PAPACY = 500 + 0 + 0 + 50 + 0 + 1 0 + 0 + 5 + 1 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 100 + 0 = 666

Kuendelea Kutafuta
Basi, kwa kuwa nilikuwa namtafuta nani mwingine anayesemwa na namba 666 au 616, nikagundua kumbe ni hao hao wanaotukana. Lakini, sikukomea hapo mwaka huu 2017 macho yangu yakasaidiwa kuona zaidi. Nilichukua jina la mwasisi wa matusi mwenyewe ELLEN GOULD WHITE ndipo nikashtuka kabisa kumbe ni namba 666. Kwa kisa hiki, leo nawaomba tuimbe alleluya pamoja.

ALLELUYA! KUMBE NAMBA 666 NI ELLEN GOULD WHITE MWENYEWE
Sasa nawapeni habari njema kabisa. Tusi la namba 666 limefumbua macho yangu kwa namna ya ajabu na sasa nawatangazia wote nilichokigundua ili kiwafumbue macho ninyi pia. Kifupi, nimefikishwa kwenye ugunduzi huo kwa kupitia tahadhari ya wahenga. Wao walisema, “Unapokula na kipofu, usimguse kipofu mkono!” Msidanganyike tena, namba 666 ni ELLEN GOULD WHITE mwenyewe.

Nawasimulieni. Kwa kuzidi kutukana, niliwatazama watukanaji nione kama matusi hayawahusu wenyewe. Nikagundua kumbe ndiyo hivyo hivyo. Kumbe, wakati mwingine heri utukanwe maana waweza kufunguliwa mlango kwa jambo jema fulani. Basi, natangaza kadamnasi kwamba tusi la namba 666 limekuwa tusi la neema na heri sana kwetu Wakatoliki, tulionyanyasika kwalo kwa muda mrefu. Linawahusu wanaotutukana hao hao. Kumbe, walikuwa wanapiga kelele za “Mwizi, mwizi!“ ili kutupoteza maboya tu. Wezi ni wenyewe.

Tuamke. Jamani, Bi Ellen Gould White alikuwa anapiga kelele na kutukana kusudi tusishughulike na jina lake. Wafuasi wake wakadakia mbinu hiyo hiyo. Kumbe, Wasabato hukazania namba 666 imwelekee Baba Mtakatifu kwa sababu walitaka tusijue kwamba namba 666 inamwelekea “nabii” wao ELLEN GOULD WHITE! Walitaka tukamsake sungura katika kichaka kingine. Kumbe, Ufu 13:18 inamtaja Bi Ellen White moja kwa moja kama mnyama ambaye jina lake ukilikokotoa linakuja moja kwa moja kwenye namba 666. Yaani linakuja 666 taslimu!

Je, unaniuliza kwa vipi? Ni hivi ifuatavyo. Ukiliandika jina la Bi ELLEN WHITE pamoja na jina la asili yake GOULD unakuja kwenye namba 666 juu ya alama. Nifuatilie vyema hapa kusudi tukokotoe tarakimu pamoja. Lakini, angalia vyema, jambo lile la kuhitajika hekima, linahusisha pia kuirudisha “W” ya WHITE kwenye uasilia wake yaani V maradufu (kwa Kiingereza “double v”). Kwa taarifa yako, tangu kale “W” ni “V” mbili na ni kwa sababu ya asili hiyo Wajerumani huitamka “W” kama “V”. Umeshanielewa uzuri? Kama umeshanielewa, sasa tazama “gematria“ inavyokubali:

E L L E N G O U L D W H I T E
0+ 50 + 50 + 0 + 0 + 0 + 0 + 5 + 50 + 500+ 10+0+1+0+0 = 666

Je, unaona jinsi jina la Bi Ellen White linavyokubali kama jina la mnyama yule? Yaani sawa sawa pasipo kuacha mashaka yoyote. Kinyume chake, jiulize ni Baba Mtakatifu gani mwenye jina kama hilo? Maskini, Wasabato walisahau jambo hili la kimahesabu! Lakini nadhani wanalifahamu na ndiyo maana hufanya juhudi kubwa kulikoneshea tusi la namba 666 kwa Baba Mtakatifu. Ni janja yao lakini sasa ipo hadharani.

Narudia. Wanachofanya Wasabato ni mbinu ya kawaida tu, yaani kwamba ukitaka watu wasikuangalie wewe elekeza umakini wao kwa mtu mwingine au kitu tofauti. Ndipo, badala ya watu kuelekeza umakini kwenye jina “ELLEN GOULD WHITE” huzugwa waelekeze kwenye majina ya kubuni ya “VICARIUS FILII DEI”, “LATEINOS” na “ROMIITH”, majina yasiyo na maana yoyote kihistoria na muktadha wa kitabu cha Ufunuo.

Je, umeona eh! Kumbe, mambo yako kwenye majina “ELLEN GOULD WHITE”. Namba 666 inakubali taslimu kabisa. Chukua hii!

Hatima

Naona imetosha, nanyi, bila shaka, mnaniambia kwa Kiingereza “Stop, it is enough and clear!” kwa maana ya “Acha inatosha na imeeleweka!” Alamsiki!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi sio Msabato,ila na Catholics hamko safe.But overall,Wasabato faithwise ni better.Wana heresies chache ambazo kimsingi haziendani na Biblia.

1.Issue ya Ellen G.White is their invention,it is not biblical.
2.Kimsingi Salvation hawaikubali na sio doctrine yao.
3.Kimsingi pia Roho Mtakatifu hapewi uzito sana katika mafundisho yao,na mambo kama ujazo wa Roho Mtakatifu sio doctrine yao.
4.Sheria ya vyakula haipo tena baada ya Neema,wao bado wanaing'ang'ania.

Ninyi Wakatoliki on the other hand mnayo mafundisho mengi,mengi,mengi sana potofu.Infact binafsi sitambui the Catholic faith kama a Christian faith.You are much closer to Muslims than Christians.Msomaji mzuri wa Biblia na mwanafunzi wa kweli wa Bwana Yesu anatambua how far away the Catholic faith is from true Christianity.

Clip ifuatayo ya Pope Francis shows clearly how the Roman Catholic Papal Institution has contributed towards heresy in other so called denominations.Infact ametaja some of your false teachings.That is why the Bible calls the Roman Catholic Papal Institution "Mother of Harlots" and the other denominations "Harlots"(Revelation 17). Ni ukweli mchungu ambao hata Pope Francis ameukiri.Watch and listen to the clip below.

Mimi sio Msabato,ila na Catholics hamko safe.Mnayo mafundisho mengi sana potofu.Infact binafsi sitambui the Catholic faith kama a Christian faith.You are much closer to Muslims than Christians,nadhani it is by design.Msomaji mzuri wa Biblia na mwanafunzi mzuri wa Bwana Yesu anatambua how far away the Catholic faith is from true Christianity.

Clip ifuatayo ya Pope Francis shows clearly how the Roman Catholic Papal Institution has contributed towards heresy in other so called denominations.That is why the Bible calls the Roman Catholic Papal Institution the "Mother of Harlots" and the other denominations "Harlots." Ni ukweli mchungu ambao hata Pope Francis ameukiri.Watch and listen to the clip below👇.

 
Soma vitabu vya Ranko Stefanovic, Revelation of Jesus Christ, na Plain Revelation (google utaviona). Ni vizuri sda wote watanzania, wanaojua kiingereza kuvisoma hivi vitabu. Ranko Stefanovic amepatia vizuri zaidi (sehemu nyingi sana) kuliko Uriah Smith, kwenye kitabu chake cha Daniel and the Revelation.

Ukisoma vitabu hivyo vya Ranko Stefanovic, utaelewa vizuri sana sana sana kuhusu kitabu cha Ufunuo, na 666. Kuna sehemu chache sana ana kosea: 1) Parapanda ya 5 na 6 ina include pia majeshi ya waarabu na waturuki. 2) Kuto kupatikana kwa tiara yenye title ya Vicarius Filii Dei haimaanishi kwamba title hiyo haipo. Title hiyo ni mfano wa kujikweza kwa mwanadamu dhidi ya Mungu. Kwa hiyo title hiyo ni aina ya 666. Haijalishi namba zake zinakuwa au haziwi 666 (ingawa incidentally zina kuwa 666).

Ranko Stefanovic amepatia sana zaidi ya mafundisho ya sda wenzake kuhusu story ya kuanguka kwa Shetani kutoka mbinguni. Ila naona ana ogopa kuwa muwazi kusema kwamba Shetani alianguka baada ya wiki ya uumbaji. Kwa sababu akisema wazi atakuwa anapingana na mafundisho ya sda wenzake.

Mapungufu ya mafundisho ya kanisa la sda ni haya:

1) Shetani na malaika zake hawa kuanguka kabla ya wiki ya uumbaji. Kwa sababu malaika wote (including Lucifer, ambae baadae ali muasi Mungu) waliumbwa siku ya pili ya wiki ya uumbaji.

2) Hakuna viumbe wengine kama binadamu kwenye sayari nyingine (kama sda wengi wanavyo fundisha).

3) Wabatize kwa staili waliyoitumia mitume wa Yesu, mtu ana inama kidogo kwa mbele, huku amesimama, huku akidumbukia kabisa kwenye maji. Wasibatize kwa staili ya mtu kalala kwa mgongo, wana mshika na kumdumbukiza kwenye maji.

4) Wasi wapinge sda wenzao, wanao sema kwamba Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles. Kwa sababu kiukweli Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles.

5) Wakubali kwamba hawa hodhi ukanisa wa kweli, na kwamba endapo kuna wasabato wanaofuata biblia ambao sio sda, wasabato hao hawana tatizo.

6) Waumini wa sda wawe pia na tabia nzuri kwenye maisha yao.

7) Baadhi ya mafundisho ya mama Ellen White ni maoni yake, na sio vitu alivyo viona kwenye maono (visions). Kwa hiyo baadhi ya mafundisho yake yanaweza yasiwe sahihi. Of course mama Ellen White yuko sahihi kwenye mafundisho yake mengi.

Sda wako sahihi kabisa kabisa kabisa kwamba sabato ni siku ya saba (Jumamosi), na kwamba Bwana Yesu Kristo hakubadilisha siku ya sabato. Na kwamba mpinga Kristo ndiye aliebadilisha siku ya sabato kutoka siku ya saba kwenda siku ya kwanza ya wiki.

Moral of the story ni: Mkristo yeyote anatakiwa kusikiliza mafundisho yanayoendana na biblia, usisikilize mafundisho ambayo hayafuati mafundisho ya biblia (hata kama ni mafundisho ya dhehebu lako).

Any way tuendelee na shughuli zetu za maisha hadi siku ya mwisho ya dunia, wakati huo huo tukiendelea kumkumbuka Bwana Yesu Kristo hadi siku hiyo atakapo rudi.
 
Soma vitabu vya Ranko Stefanovic, Revelation of Jesus Christ, na Plain Revelation (google utaviona). Ni vizuri sda wote watanzania, wanaojua kiingereza kuvisoma hivi vitabu. Ranko Stefanovic amepatia vizuri zaidi (sehemu nyingi sana) kuliko Uriah Smith, kwenye kitabu chake cha Daniel and the Revelation.

Ukisoma vitabu hivyo vya Ranko Stefanovic, utaelewa vizuri sana sana sana kuhusu kitabu cha Ufunuo, na 666. Kuna sehemu chache sana ana kosea: 1) Parapanda ya 5 na 6 ina include pia majeshi ya waarabu na waturuki. 2) Kuto kupatikana kwa tiara yenye title ya Vicarius Filii Dei haimaanishi kwamba title hiyo haipo. Title hiyo ni mfano wa kujikweza kwa mwanadamu dhidi ya Mungu. Kwa hiyo title hiyo ni aina ya 666. Haijalishi namba zake zinakuwa au haziwi 666 (ingawa incidentally zina kuwa 666).

Ranko Stefanovic amepatia sana zaidi ya mafundisho ya sda wenzake kuhusu story ya kuanguka kwa Shetani kutoka mbinguni. Ila naona ana ogopa kuwa muwazi kusema kwamba Shetani alianguka baada ya wiki ya uumbaji. Kwa sababu akisema wazi atakuwa anapingana na mafundisho ya sda wenzake.

Mapungufu ya mafundisho ya kanisa la sda ni haya:

1) Shetani na malaika zake hawa kuanguka kabla ya wiki ya uumbaji. Kwa sababu malaika wote (including Lucifer, ambae baadae ali muasi Mungu) waliumbwa siku ya pili ya wiki ya uumbaji.

2) Hakuna viumbe wengine kama binadamu kwenye sayari nyingine (kama sda wengi wanavyo fundisha).

3) Wabatize kwa staili waliyoitumia mitume wa Yesu, mtu ana inama kidogo kwa mbele, huku amesimama, huku akidumbukia kabisa kwenye maji. Wasibatize kwa staili ya mtu kalala kwa mgongo, wana mshika na kumdumbukiza kwenye maji.

4) Wasi wapinge sda wenzao, wanao sema kwamba Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles. Kwa sababu kiukweli Yesu alizaliwa during the Feast of Tabernacles.

5) Wakubali kwamba hawa hodhi ukanisa wa kweli, na kwamba endapo kuna wasabato wanaofuata biblia ambao sio sda, wasabato hao hawana tatizo.

6) Waumini wa sda wawe pia na tabia nzuri kwenye maisha yao.

7) Baadhi ya mafundisho ya mama Ellen White ni maoni yake, na sio vitu alivyo viona kwenye maono (visions). Kwa hiyo baadhi ya mafundisho yake yanaweza yasiwe sahihi. Of course mama Ellen White yuko sahihi kwenye mafundisho yake mengi.

Sda wako sahihi kabisa kabisa kabisa kwamba sabato ni siku ya saba (Jumamosi), na kwamba Bwana Yesu Kristo hakubadilisha siku ya sabato. Na kwamba mpinga Kristo ndiye aliebadilisha siku ya sabato kutoka siku ya saba kwenda siku ya kwanza ya wiki.

Moral of the story ni: Mkristo yeyote anatakiwa kusikiliza mafundisho yanayoendana na biblia, usisikilize mafundisho ambayo hayafuati mafundisho ya biblia (hata kama ni mafundisho ya dhehebu lako).

Any way tuendelee na shughuli zetu za maisha hadi siku ya mwisho ya dunia, wakati huo huo tukiendelea kumkumbuka Bwana Yesu Kristo hadi siku hiyo atakapo rudi.
Huyo kaunda conspiracy theories zake, sasa kama huna fikra huru utachukulia poa kama ndiyo ukweli.
 
Anaandika Baba Titus Amigu: (Padri na gwiji/mwamba wa Theolojia).

Mfuatilie usome ujichotee maarifa upate ukweli na kisha ukuweke huru.. .
Wakatoliki hawabahatishi haya mambo..

NAMBA 666 AU 616 ILIYOANDIKWA KWENYE UFU 13:18 HAIMHUSU PAPA ISIPOKUWA ELLEN GOULD WHITE

Imbeni pamoja nami ALLELUYA! Kwa nini? Kwa sababu Mungu amenitendea makuu. Amenisaidia kukitegua kitendawili cha karibu karne mbili sasa, yaani kitendawili cha namba 666. Kwa muda mrefu tangu enzi za akina ELLEN GOULD WHITE, yaani miaka ile ya 1846, namba 666 ya katika Ufu 13:18 imekuwa ikielekezwa kwa majungu na matusi kwa Baba Mtakatifu. Ndugu zanguni, tulikuwa tunazugwa tu. Kumbe, siri ni kwamba ilikuwa inamwelekea mwenyewe aliyekuwa anaelekeza mashambulizi na matusi kwa Baba Mtakatifu, yaani ELLEN GOULD WHITE.

Nina furaha kubwa sana. Nawaalikeni mfurahi pamoja nami. Binafsi, nilikuwa napata taabu sana kujaribu kufumbua kitendawili hicho. Lakini, wakati huo huo, nilikuwa najiuliza kwa nini mashambulizi kwa Baba Mtakatifu ni makali hivyo? Kumbe, sasa tumefumbuliwa. Yote yalikuwa ni mbinu ya kutupoteza watu “maboya” tusijue kwamba namba inamwelekea mwenyewe anayetukana. Kumbe, ilikuwa ni mbinu ile ile ya mwizi kupiga kelele za “Mwizi, mwizi, mwizi huyo!” kusudi watu wamfukuze mtu mwingine na siyo yeye mwenyewe.

Acheni niwakumbusheni mambo. Nadhani nyote mna habari na mashtaka maarufu sana dhidi ya Wakatoliki kwamba namba 666 au 616 inamhusu kiongozi wetu mkuu yaani Papa au Baba Mtakatifu na kwamba namba hiyo imeandikwa kwenye mavazi yake na kofia yake. Zaidi ya hapo kuna madai kwamba namba hii ipo pia katika kompyuta na satelite. Leo nataka niwafunulieni mambo yalivyo.

Hii ni Mada ya Lugha na Hesabu Kidogo
Vijana wangu msishtuke na kuhangaika. Mada hii itahusisha herufi za Kiebrania na Kigiriki lakini zitakuwa chache tu nanyi mtaelewa yote nitakayoandika kwani ni masuala rahisi kuyafuatilia. (Kwa bahati mbaya herufi za Kigiriki zinakataa humu). Papo hapo, kutakuwa na hesabu. Hata hizo hazitawahangaisheni kwani ni hesabu za kujumlisha tu. Leo kumbukeni pia hesabu za Shule ya Msingi tulipokuwa tunatumia tarakimu za Kilatini, kwa mfano, I = 1, V = 5, X= 10, L = 50, C= 100, D = 500 na M = 1000.
Ili tuelewane, nitaanza na historia, kishapo nitakwenda nje ya Biblia ilikohamishiwa namba 666.

Mama ni Historia
Hebu nianze na jibu fupi linalolingana na historia. Wayahudi hujumlisha thamani ya kitarakimu majina ya watu na maneno mbalimbali na kuzaa namba mbalimbali. Kuhesabu kwa namna hii huitwa gematria nako kumetumika katika Ufu 13:18 na kuzaa namba 666 au katika nakala zingine za Biblia namba 616. Swali kubwa ni je, namba hiyo inamhusu nani? Ukweli ni kwamba namba 666 au 616 haimhusu Papa au Baba Mtakatifu hata kidogo. Tena haikuandikwa katika mavazi ya Papa na wala haimo katika kompyuta ama satelite.

Ukweli, kibiblia na kihistoria, ni kwamba namba hiyo ilimhusu na bado inamhusu kiongozi wa dola ya Kirumi zamani zile, yaani Kaisari Nero. Basi, namba 666 au 616 ndiyo hesabu ya jina la Nero aliyekuwa akiwadhulumu Wakristo katika karne ya kwanza ya Ukristo. Hesabu hiyo inapatikana kwa kukokotoa kigematria maneno NERON KAISAR (kwa Kiebrania - נרון קסר) au NERO KAISAR (kwa Kiebrania - נרו קסר) na KAISAR THEOS (kwa Kigiriki).

Jibu refu: Hakuna mahali po pote katika Biblia ambapo msomaji ameombwa kutumia akili isipokuwa hapa. Kwa kuwa ili kuipata hesabu hii kulihitaji kupiga hesabu, wasomaji wote wa kifungu kile walialikwa kupiga hesabu, gematria. Ndipo imeandikwa “Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na akili na aihesabu hesabu” (Ufu 13:18). Kumbe, kinyume na matumizi ya akili, hapa ndipo mahala wasomaji kadha wa kadha wasipotumia akili yoyote katika kusoma isipokuwa majungu na usingiziaji.

Ndugu yangu, wapo watu chungu nzima wanaoeneza tafsiri kwamba namba 666 au 616 inamhusu Baba Mtakatifu na imeandikwa kwenye mavazi yake kama nilivyosema hapo juu (rejea Ufu 13:18, 15:2). Je, mafundisho hayo yana ukweli? Najijibu mwenyewe: Si ya kweli.

Tusisahau, kitabu cha Ufunuo wa Yohane kina mazingira yake ya kihistoria ambayo ni muhimu katika kuielewa sura ya 13. Mazingira hayo ni ya historia ya Dola ya Kirumi. Wakristo walipokuwa wakidhulumiwa na dola hiyo, mwandishi wa kitabu cha Ufunuo alichukua kalamu na kuandika ili kuwaliwaza ndugu zake aliokuwa akiteseka pamoja nao (rejea Ufu 1:9). Basi, katika kuandika akatumia lugha ya mafumbo ili watesi wasifahamu wanayosemwa. Ndicho kisa, basi, joka kuu lenye pembe na kadhalika linamaanisha Dola ya Kirumi. Mkubwa wa dola hiyo naye akapewa jina la kupanga au jina la kifumbo kwa mtindo wa kucheza na namba za jina lake (gematria).

Ukitaka kupata picha kidogo ya haya, chukulia mfano wa vitabu vya marehemu Shaban Robert. Yeye aliandika mashairi mengi ya kuwatia watu hamasa wapiganie uhuru. Katika mashairi hayo, wananchi anawaita, mathalani, siafu na wakoloni nyoka. Hao siafu wanakazana kumdhuru nyoka. Aidha, kitabu chake cha Kusadikika ni kitabu cha fumbo kinachofumbia hali ya mambo katika hewa ya kikoloni. Kwa hakika wakoloni hawakuambulia lolote katika mashairi na fasihi ya Shaban Robert. Kinyume chao, wananchi walielewa mada husika na “kuwaacha kwenye mataa” wakoloni.

Ndivyo inavyotokea shuleni, mwalimu mbaya kupangwa jina ambalo mwenyewe halijui hata kama litatajwa mbele yake.
Upangaji wa jina la mtu kwa kutumia hesabu ya herufi za jina lake mwenyewe ulikuwa mtindo maarufu wa marabi na ulijulikana kama gematria. Ufu 13:18, si mahali pa kwanza kutumia gematria hata namba kumi na nne ya vizazi vilivyotajwa katika Mt 1:17 ni gematria ya jina Daudi (דוד) kwani d + w + d ni 6 + 4 + 6 = 14. Sasa ni nani katika karne ya kwanza aliyekuwa adui wa Wakristo na jina lake kigematria lilizaa namba 666 au 616? Hili ndilo swali la kuulizana. Alikuwa KAISARI NERO.

Tukitafsiri Biblia kwa usahihi huu, mtesi wa walengwa wa kitabu, aliyekuwa akifumbiwa katika 13:18 kwa kuhesabu jina lake kigematria, hawezi kuwa mtu wa karne ya tano au ya ishirini na moja. Walengwa walikuwa ni Wakristo wa karne ya kwanza na adui yao alikuwa akiishi nao kwa wakati huo huo. Basi, nani alikuwa mtesi maarufu katika mazingira ya karne ya kwanza? Wakati ule alikuwa Kaisari Nero ama Kaisari fulani aliyejidai kuwa Mungu na huyo ndiye kigematria jina lake linazaa namba 666 au 616.

Basi, gematria ikitumika kwa konsonanti za Kiebrania: נרון קסר - NERON KAISAR (yaani Kaisari Neron) au kwa maneno ya Kigiriki: KAISAR THEOS (yaani Kaisari Mungu) tunapata pasipo kuzunguka zunguka namba 666 au 616. Tazama hesabu zenyewe zinavyofanyika. (נרון קסר) r s q n w r n = 200 + 60 + 100 + 50 + 6 + 200 + 50 = 666.
k a i s a r th e o s = 20 + 1 + 10 + 200 + 1 + 100 + 9 + 5 + 70 + 200 = 616.

Angalia vyema. Hii tafsiri ya ‘KAISAR THEOS’ yaani ‘Mungu Kaisari’ ndiyo inayorejewa kwenye Biblia zenye kuandika jumla ya namba 616. Lakini vile vile 616 iliweza kupatikana kwa kuondoa “n” ya mwisho kwenye jina נרון (n w r n) katika Kiebrania. Kwa Wakristo, namba 666 ilipomtaja Neron ilisema pia kwamba ni MPINGA KRISTO kwani alikuwa kinyume cha utimilifu. Kinambari, utimilifu ni namba 777. Kumbe, yeye Kaisari Nero ni upungufu kwani hesabu yake ni 666 ambayo ni 777 kutoa 111.

Basi, kwa kuzingatia mazingira ya kitabu cha Ufunuo namba 666 au 616 haiwezi kusimama kwa ajili ya jina lingine kama Baba Mtakatifu, Mtume Mohamed au Mussolini. Haya ni baadhi ya majina wanayolazimisha watu yafanye hesabu ya 666. Na, kwa hakika, namba hiyo haimo katika mavazi wala kofia (mitra) ya Baba Mtakatifu. Hakuna mtu yeyote anayeweza kuonesha vazi hilo au kofia hiyo kwa ushahidi. Kwani ni vazi gani au kofia ipi? Basi, kama tunautafuta uzima wa milele, aheri tuache majungu na uongo kama huu. Kama ni maandishi, ni mitra yake tu yenye herufi mbili A na W yaani alpha na omega (rejea Ufu 1:8,17).

Acha tuendelee. Wanaombambikizia Baba Mtakatifu namba 666 hudai kuikokotoa nambari hiyo katika majina matatu tofauti: jina la Kilatini VICARIUS FILII DEI (Kaimu wa Mwana wa Mungu), jina la Kigiriki LATEINOS (Mlatini) na jina la Kiebrania ROMIITH (רמיית - Mrumi). Majina hayo huhesabiwa na wanaombambikizia Baba Mtakatifu namba hiyo kama ifuatavyo:

VICARIUS FILII DEI = 5 + 1 + 100 + 0 + 0 + 1 + 5 + 0 + 0 + 1 + 50 + 1 + 1 + 500 + 0 + 1 = 666.
LATEINOS = 30 + 1 + 300 +5 + 10 + 50 + 70 + 200 = 666.

ROMIITH yaani th y y m w r = 400 + 10 + 10 + 40 + 6 + 200 = 666.

Ndugu zangu, kwa misingi halali ya kusoma Biblia hatuwezi kuyapokea majina haya bila kuyafanyia tahakiki ya kihistoria. Bila kurefusha mjadala, majina haya hayajapata kutumiwa na Baba Mtakatifu yeyote, katika historia ya Kanisa sembuse wakati wa karne ya kwanza Baada ya Kristo wakati ambao hata upapa wenyewe ulikuwa haujakua. Mapapa wa karne zile hawakuwa hatari kwa mtu yeyote. Na watu wasio hatari watapewaje majina ya kupanga na ya siri? Wale wasomaji wa kitabu cha Ufunuo wangelielewaje aya ngumu inayotaja kitu kisichojulikana kwa jina hilo? Wangelifanyaje gematria kwa kutumia majina wasiyoyajua?

Aya 13:18 ilizungumzia jina ambalo wasomaji walikuwa wakilijua kama jina la adui yao aliyekuwa akiwadhulumu na si majina ya ndoto au majungu ya karne ya 20 na 21 B.K. Zaidi ya hayo majina mengine yamelazimishwa kihesabu ili jumla ya kiherufi iwe 666. Kwa ushuhuda tazama U ilivyolazimishwa imaanishe tarakimu 5. Katika Kilatini 5 ni V na wala siyo U. Zaidi ya hayo, jina “MLATINI” kama lingelitumika wakati huo, wasomaji wangelielewa kuwataja wakoloni au askari wa kirumi ambao walikuwa wakitawala ulimwengu wa wakati ule.

Hali kadhalika, kama jina “MRUMI” lingelitumika wakati huo, wasomaji wangelielewa kuwataja wakoloni au askari wa kirumi ambao walikuwa wakitawala ulimwengu wa wakati ule. Kwa hoja hizi, majina hayo ya majungu ni ya tangu karne ya 16, Kanisa Katoliki lilipoanza kupingwa kwa ari mpya na uongozi wake kukataliwa.

Nadhani hadi hapa kila mwenye kutaka kujua anajua kwamba majina waliyobuni Wasabato hayatumiwi na Baba Mtakatifu yeyote. Na zaidi ya hayo ni majina ambayo mwandishi wa kitabu cha Ufunuo hakuwa hata na habari nayo katika karne ile ya kwanza B.K. kwa vile alivyokiandika kitabu chake kwa Kigiriki na wala si kwa Kiebrania au Kilatini. Kumbe, kwa kufanya hivyo Wasabato huwa wanainyonga historia na kukizungumzia kitabu cha Ufunuo nje ya muktadha wake wa kihistoria. Hili ni kosa la kusiganisha nyakati za kikalenda (kwa Kiingereza “anachronism”).

Basi, kwa heshima ya Maandiko Matakatifu, tutafsiri namba 666 au 616 kwa gematria asilia na tukomee hapo hapo. Tusiihamishe namba hiyo na kuwapachika watu wasio na hatia. Kufanya hivyo ni kujitowelesha majungu na ni dhambi isiyo na maana yo yote. Lakini, basi namba 666 imetolewa nje ya mazingira ya Biblia na ndipo ilipowekwa sasa. Nami nimefika hapo hapo.

Namba 666 Imehamishiwa Nje ya Biblia

Ni kituko lakini ndivyo ilivyo. Watu wengine hudai kwamba namba hiyo imeandikwa shingoni kwenye nguo za Papa. Huo ndio uongo na usingiziaji usio na aibu kwa sababu nguo hizo hakuna anayeweza kutuonesha wenziwe. Siku moja niliwahi kuambiwa na wainjilisti wawili kwamba namba 666 ipo kwenye bidhaa za siku hizi, yaani kwenye kifungashio, pale inapochorwa mistari mingi mifupi na mirefu na kuandikwa namba kwa chini, na kwa namna hiyo ipo pia kwenye satelite. Siku hiyo niliwakamata kutokujua nilipowadai wanioneshe mfano. Basi, wakaleta baadhi ya bidhaa za kisasa, wakaniambia niangalie ile mistari iliyochorwa katika kifungashio cha kila bidhaa. Hapo walionesha pia mistari miwili miwili inayojitokeza zaidi kwa chini (jambo ambalo si kweli kwa kila bidhaa). Basi, hapo ndipo walipodai kuna namba 666.

Kumbe, huu ulikuwa ujinga wao mkubwa. Ndugu yangu, mistari hiyo, ndiyo bei ya bidhaa hasa kwa zile zinazouzwa „“supermarket. Katika nchi zilizoendelea watu hawaandiki bei shilingi fulani au fulani wakabandika kwenye bidhaa. Badala yake ndiyo hiyo mistari, kadiri ilivyochorwa ndivyo mashine ya kupigia hesabu inavyotambua na kutofautisha bei za bidhaa ambazo mnunuzi amezifikisha kwenye “kaunta” ya kulipia manunuzi. Na tena bei hizo hazikuingizwa katika satelite; zilivyo nyingi hazihusishwi na satelite yoyote.

Basi, niliwaonya wainjilisti wale wasiwadanganye watu kwa kutumia ujinga wao wakati wenyewe pia hawajui mambo ya kisasa. Hatimaye, niliwaambia, kwa uongo wa namna ile, wao si wainjilisti kwani Injili ni Habari Njema ya ukombozi wetu uliotufikia kwa kifo na ufufuko wa Yesu Kristo na wala siyo namba 666 inayodaiwa kuandikwa kwenye nguo za Papa na kuingizwa kwenye satelite kwa njia ya michoro ya bidhaa za kisasa. Kwa kweli niliwaambia kwa kueneza uongo na kuwatia watu hofu kwa kuwatinga, hawakuwa mbali sana na moto wa milele kwa vile wanamtumikia Shetani aliye baba wa uongo. Hapo nikapata mwanya wa kuwaalika watubu kwa haraka. Lakini, badala ya kupokea mafundisho yangu walisema sina Roho Mtakatifu na kuondoka. Waliondoka na hawakurudi tena kwangu. Kumbe, niliwafuma katika kutokujua kwao, yaani ujinga wao. Samahani kwa simulizi hili; majadiliano yetu yaliacha kuwa ya Kikristo.

Safari Ndefu ya Kutegua Kitendawili cha Kale
Kwa vile madai ya kwamba namba 666 inamhusu Baba Mtakatifu yametutoa sote kutoka kwenye Biblia na kutupa kazi ya kumtafuta nani mwingine anaweza kuwa anatajwa na namba hiyo, nilichukua kalamu na kuanza kuchunguza maneno ya wanaotukana kama hayahusiki vile vile. Utafutaji wangu ulizaa matunda mwaka ule ule 1998. Nikategua kitendawili kwa kugundua kwamba kauli za Wasabato wenyewe zilikuwa ndiyo namba 666.

Nilifanyaje? Nilichukua kauli tatu: PONYA SIKU MUHIMU YA SABA (kwa Kiingereza CURE VITAL SEVENTH DAY, kwa Kilatini CURATUS VITALE SABBATA DIES) na WOKOVU, PONYA SIKU YA SABA (kwa Kiingereza SALVATION, CURE SEVENTH DAY, kwa Kilatini SALVUS, CURARE SABBATA DIES) na VUNJA, CHUKIA UPAPA (kwa Kiingereza DEAL AXE, VIE PAPACY). Nilistaajabu sana kuona ndiyo inakuja 666 ndipo mara moja nikaingiza ugunduzi wangu katika kitabu changu KISA CHA IMANI namba 1.

Ni kweli. Kauli mbiu za Wasabato ni namba hiyo hiyo 666. Angalia gematria inavyokwenda:
CURE VITAL SEVENTH DAY = 100 + 5 + 0 + 0 + 5 + 1+ 0 + 0 + 50 + 0 + 0 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 0 + 0 = 666
CURATUS VITALE SABBATA DIES = 100 + 5 + 0 + 0 + 0 + 5 + 0 + 5 + 1 + 0 + 0 + 50 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 1 + 0 + 0 = 666

SALVATION, CURE SEVENTH DAY = 0 + 0 + 50 + 5 + 0 + 0 + 1 + 0 + 0 + 100 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 0 + 0 = 666
SALVUS, CURARE SABBATA DIES = 0 + 0 + 50 + 5 + 5 + 0 + 100 + 5 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 500 + 1 + 0 + 0 = 666
DEAL AXE VIE PAPACY = 500 + 0 + 0 + 50 + 0 + 1 0 + 0 + 5 + 1 + 0 + 0 + 0 + 0 + 0 + 100 + 0 = 666

Kuendelea Kutafuta
Basi, kwa kuwa nilikuwa namtafuta nani mwingine anayesemwa na namba 666 au 616, nikagundua kumbe ni hao hao wanaotukana. Lakini, sikukomea hapo mwaka huu 2017 macho yangu yakasaidiwa kuona zaidi. Nilichukua jina la mwasisi wa matusi mwenyewe ELLEN GOULD WHITE ndipo nikashtuka kabisa kumbe ni namba 666. Kwa kisa hiki, leo nawaomba tuimbe alleluya pamoja.

ALLELUYA! KUMBE NAMBA 666 NI ELLEN GOULD WHITE MWENYEWE
Sasa nawapeni habari njema kabisa. Tusi la namba 666 limefumbua macho yangu kwa namna ya ajabu na sasa nawatangazia wote nilichokigundua ili kiwafumbue macho ninyi pia. Kifupi, nimefikishwa kwenye ugunduzi huo kwa kupitia tahadhari ya wahenga. Wao walisema, “Unapokula na kipofu, usimguse kipofu mkono!” Msidanganyike tena, namba 666 ni ELLEN GOULD WHITE mwenyewe.

Nawasimulieni. Kwa kuzidi kutukana, niliwatazama watukanaji nione kama matusi hayawahusu wenyewe. Nikagundua kumbe ndiyo hivyo hivyo. Kumbe, wakati mwingine heri utukanwe maana waweza kufunguliwa mlango kwa jambo jema fulani. Basi, natangaza kadamnasi kwamba tusi la namba 666 limekuwa tusi la neema na heri sana kwetu Wakatoliki, tulionyanyasika kwalo kwa muda mrefu. Linawahusu wanaotutukana hao hao. Kumbe, walikuwa wanapiga kelele za “Mwizi, mwizi!“ ili kutupoteza maboya tu. Wezi ni wenyewe.

Tuamke. Jamani, Bi Ellen Gould White alikuwa anapiga kelele na kutukana kusudi tusishughulike na jina lake. Wafuasi wake wakadakia mbinu hiyo hiyo. Kumbe, Wasabato hukazania namba 666 imwelekee Baba Mtakatifu kwa sababu walitaka tusijue kwamba namba 666 inamwelekea “nabii” wao ELLEN GOULD WHITE! Walitaka tukamsake sungura katika kichaka kingine. Kumbe, Ufu 13:18 inamtaja Bi Ellen White moja kwa moja kama mnyama ambaye jina lake ukilikokotoa linakuja moja kwa moja kwenye namba 666. Yaani linakuja 666 taslimu!

Je, unaniuliza kwa vipi? Ni hivi ifuatavyo. Ukiliandika jina la Bi ELLEN WHITE pamoja na jina la asili yake GOULD unakuja kwenye namba 666 juu ya alama. Nifuatilie vyema hapa kusudi tukokotoe tarakimu pamoja. Lakini, angalia vyema, jambo lile la kuhitajika hekima, linahusisha pia kuirudisha “W” ya WHITE kwenye uasilia wake yaani V maradufu (kwa Kiingereza “double v”). Kwa taarifa yako, tangu kale “W” ni “V” mbili na ni kwa sababu ya asili hiyo Wajerumani huitamka “W” kama “V”. Umeshanielewa uzuri? Kama umeshanielewa, sasa tazama “gematria“ inavyokubali:

E L L E N G O U L D W H I T E
0+ 50 + 50 + 0 + 0 + 0 + 0 + 5 + 50 + 500+ 10+0+1+0+0 = 666

Je, unaona jinsi jina la Bi Ellen White linavyokubali kama jina la mnyama yule? Yaani sawa sawa pasipo kuacha mashaka yoyote. Kinyume chake, jiulize ni Baba Mtakatifu gani mwenye jina kama hilo? Maskini, Wasabato walisahau jambo hili la kimahesabu! Lakini nadhani wanalifahamu na ndiyo maana hufanya juhudi kubwa kulikoneshea tusi la namba 666 kwa Baba Mtakatifu. Ni janja yao lakini sasa ipo hadharani.

Narudia. Wanachofanya Wasabato ni mbinu ya kawaida tu, yaani kwamba ukitaka watu wasikuangalie wewe elekeza umakini wao kwa mtu mwingine au kitu tofauti. Ndipo, badala ya watu kuelekeza umakini kwenye jina “ELLEN GOULD WHITE” huzugwa waelekeze kwenye majina ya kubuni ya “VICARIUS FILII DEI”, “LATEINOS” na “ROMIITH”, majina yasiyo na maana yoyote kihistoria na muktadha wa kitabu cha Ufunuo.

Je, umeona eh! Kumbe, mambo yako kwenye majina “ELLEN GOULD WHITE”. Namba 666 inakubali taslimu kabisa. Chukua hii!

Hatima

Naona imetosha, nanyi, bila shaka, mnaniambia kwa Kiingereza “Stop, it is enough and clear!” kwa maana ya “Acha inatosha na imeeleweka!” Alamsiki!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nieleweshe. Je w=10? Au mimi sielewi

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom