Idd Ninga
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 5,134
- 4,293
Haja yangu ni kuliona jimbo la Arusha mjini likiwa Geneva ya kweli ya Afrika,kuigeuza na kuifanya Arusha kuwa makao makuu ya utalii Afrika ya mashariki na kati na kuweka mikakati na mipango na wadau wa utalii katika jimbo hili kuhakikisha utalii unatangazwa na vijana wanapata ajira ya uhakika kupitia sekta hii mama katika jimbo hili.
Nitahakikisha haki na usawa unapatikana kwa wafanyakazi wa jimbo hili,nitwaunganisha na kutengeneza vyama vya wafanyakazi vitakavyokuwa na sauti yenye nguvu na itakayosikika na kufanyiwa kazi na serikali,wafanyakazi wa chini nitawahakikishia wanajiona kuwa ni sehemu ya watu wanaostahili kupata haki zao,malipo yao ya zaida,mikataba yenye nguvu katika kazi,nitawatengenezea mazingira ya kuwa sehemu ya jamii inayosikilizwa nchini Tanzania.
Nitaanzisha mpango wa vijana kujiendeleza kielimu na kuanzisha masomo ya jioni kwa ajili yao kwa ajili ya kuwaandaa kuwa wataalamu watakaoendesha maisha yao na kufikia viwango vya juu vya elimu,elimu ya watu wazima itaimarishwa katika misingi rahisi,watoto na wanafunzi wasiokuwa na uwezo wa kupata mahitaji ya shule watapata kupitia mfuko maalumu utakaotengenezwa kwa ajili yao.
Nitahakikisha serikali inaboresha mazingira ya upatikanaji wa matibabu kwa wakazi wa Arusha mjini,madawa yafike kwa wakati na bima maalumu ianzishwe kwa ajili ya watu masikini na wasiokuwa na uwezo.
Kama mbunge wa Arusha mjini,nitaweka mkakati wa kuzungumza na watu wangu kila mwisho wa mwezi,mazungumzo ambayo yatakua ni mazungumzo ya wazi na kila mtu atakua na uhuru wa kuuliza au kutolea maoni chochote katika jimbo langu.
Nitaunganisha taasisi na asasi zote za maendeleo,kina mama,watoto,kina baba na vijana kwa ajili ya kupata fursa mbalimbali zitakazotokea,itakua Arusha ya uwazi,Arusha ya fursa,Arusha ya maendeleo,Arusha ya mfano.
Ni wakati wa mabadiliko katika jimbo la Arusha mjini,ni wakati wa vijana wachapakazi wasio na maneno,ni wakati wa kuileta Arusha pamoja.
Natangaza nia rasmi ya kugombea ubunge jimbo la Arusha mjini.
Asanteni.
Idd Ninga.
Arusha Mjini
04.07.2020
Nitahakikisha haki na usawa unapatikana kwa wafanyakazi wa jimbo hili,nitwaunganisha na kutengeneza vyama vya wafanyakazi vitakavyokuwa na sauti yenye nguvu na itakayosikika na kufanyiwa kazi na serikali,wafanyakazi wa chini nitawahakikishia wanajiona kuwa ni sehemu ya watu wanaostahili kupata haki zao,malipo yao ya zaida,mikataba yenye nguvu katika kazi,nitawatengenezea mazingira ya kuwa sehemu ya jamii inayosikilizwa nchini Tanzania.
Nitaanzisha mpango wa vijana kujiendeleza kielimu na kuanzisha masomo ya jioni kwa ajili yao kwa ajili ya kuwaandaa kuwa wataalamu watakaoendesha maisha yao na kufikia viwango vya juu vya elimu,elimu ya watu wazima itaimarishwa katika misingi rahisi,watoto na wanafunzi wasiokuwa na uwezo wa kupata mahitaji ya shule watapata kupitia mfuko maalumu utakaotengenezwa kwa ajili yao.
Nitahakikisha serikali inaboresha mazingira ya upatikanaji wa matibabu kwa wakazi wa Arusha mjini,madawa yafike kwa wakati na bima maalumu ianzishwe kwa ajili ya watu masikini na wasiokuwa na uwezo.
Kama mbunge wa Arusha mjini,nitaweka mkakati wa kuzungumza na watu wangu kila mwisho wa mwezi,mazungumzo ambayo yatakua ni mazungumzo ya wazi na kila mtu atakua na uhuru wa kuuliza au kutolea maoni chochote katika jimbo langu.
Nitaunganisha taasisi na asasi zote za maendeleo,kina mama,watoto,kina baba na vijana kwa ajili ya kupata fursa mbalimbali zitakazotokea,itakua Arusha ya uwazi,Arusha ya fursa,Arusha ya maendeleo,Arusha ya mfano.
Ni wakati wa mabadiliko katika jimbo la Arusha mjini,ni wakati wa vijana wachapakazi wasio na maneno,ni wakati wa kuileta Arusha pamoja.
Natangaza nia rasmi ya kugombea ubunge jimbo la Arusha mjini.
Asanteni.
Idd Ninga.
Arusha Mjini
04.07.2020