Kipindi hiki cha uchaguzi, nimeona mabadiliko katika utendaji wa jeshi la polisi kitu ambacho kimenifanya niandike hii post kulipongeza. Kutokana na vurugu ambazo zimekwishatokea, ni wazi raia wengi wangekuwa wameshapoteza maisha au kutiwa vilema vya maisha.
Lakini nimeona kuwa polisi wameonesha kubadilika sana! Kama ni mafunzo ndio yaliyowabadilisha, waendelee kufunzwa kutenda kazi kiustaarabu kama ambavyo wameweza kufanya. Kumbe inawezekana kwa jeshi letu la polisi kutoa ulinzi hata kama raia wana fujo kiasi gani bila kutumia risasi za moto au kuwajeruhi raia vibaya na hata kuwatia vilema vya bure. Nilikuwa nimeshaondoa imani yangu kwa jeshi la polisi hasa pale walipokuwa wakiwapiga raia bila sababu za msingi lakini sasa naanza tena kuirudisha. Miaka ya huko nyuma haikuwa hivi. Kilichobaki ni kupiga vita rushwa na kubambikia watu wasio na hatia kesi.
Hongera jeshi letu la polisi!
Lakini nimeona kuwa polisi wameonesha kubadilika sana! Kama ni mafunzo ndio yaliyowabadilisha, waendelee kufunzwa kutenda kazi kiustaarabu kama ambavyo wameweza kufanya. Kumbe inawezekana kwa jeshi letu la polisi kutoa ulinzi hata kama raia wana fujo kiasi gani bila kutumia risasi za moto au kuwajeruhi raia vibaya na hata kuwatia vilema vya bure. Nilikuwa nimeshaondoa imani yangu kwa jeshi la polisi hasa pale walipokuwa wakiwapiga raia bila sababu za msingi lakini sasa naanza tena kuirudisha. Miaka ya huko nyuma haikuwa hivi. Kilichobaki ni kupiga vita rushwa na kubambikia watu wasio na hatia kesi.
Hongera jeshi letu la polisi!